" Ujumbe wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa watembelea Kituo cha Tafiti za Kilimo " 

" Ujumbe wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa watembelea Kituo cha Tafiti za Kilimo " 
" Ujumbe wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa watembelea Kituo cha Tafiti za Kilimo " 
" Ujumbe wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa watembelea Kituo cha Tafiti za Kilimo " 
" Ujumbe wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa watembelea Kituo cha Tafiti za Kilimo " 
" Ujumbe wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa watembelea Kituo cha Tafiti za Kilimo " 

Leo Alhamisi, Wizara ya Vijana na Michezo kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo na kuboresha Ardhi, zimeandaa ziara ya kutembelea Kituo cha kijimbo  cha chakula na Malisho kinachohusiana na  Kituo cha Tafiti kilichopo Wizara ya Kilimo, kwa Ushirikiano wa idadi ya wajumbe walioshiriki katika Udhamini wa Gamal Abd El Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa  kwa toleo lake la pili, chini ya kauli mbiu " Ushirikiano wa Kusini-Kusini " kwa ushirikiano na Chuo cha kitaifa cha Mafunzo, Wizara ya Mambo ya Nje na taasisi kadha za kitaifa,pamoja na Ufadhili wa Rais. Abd El Fatah El-Sisi, kwa ushirikiano wa viongozi wa vijana 100 kutoka nchi 50 kwenye mabara matatu (Afrika - Asia - Amerika ya Kusini ), mnamo kipindi cha 1 hadi 16 Juni.

Wajumbe hao  wakati wa kufika kwao  walikaribishwa na  Prof. Dkt. Saad Moussa - Msimamizi Mkuu wa Mahusiano ya Kilimo cha Nje, Prof. Dk. Adel Abd El Azim,   wakili wa Kituo cha Tafiti za Kilimo kwa Masuala ya miongozo, na Prof. Maher Al-Maghraby, Mkurugenzi Mtendaji wa Mradi wa Mashamba ya Pamoja na Nchi za Afrika.

wakati wa ziara hiyo, ujumbe uliangalia  shughuli muhimu zaidi za kituo , programu za kiutafiti  na kimawasiliano pamoja na watafiti wa mabara matatu "  Afrika ,  Asia na  America ya Kusini. vilevile , ujumbe ulipata maelezo juu ya kituo cha tafiti na jukumu lake katika kuimarisha na kuendeleza kilimo nchini Misri ambapo  wakati wa mkutano imeshatoa onesho la kufafanua  shughuli za mradi wa mashamba ya pamoja ya kimisri, yaliyofanyika katika nchi za Afrika .

Kwa upande wake , Msimamizi wa Mahusiano ya Kilimo cha Nje Dkt.Saad Moussa alisema kwamba  kilimo cha Misri kilishuhudia maendeleo  yasiyo na kifani katika Kiwango cha kitaifa   ndani ya Misri katika zama ya Rais Abd El Fatah El-Sisi, na Misri ilifanikiwa kuimarisha ushirikiano wa kilimo  pamoja na nchi za Afrika na kurudi  katika nafasi yake ya uongozi, haswa wakati wa  uongozi wake kwa  Umoja wa Afrika, ambapo Rais El-Sisi amebeba matatizo ya Afrika na kufanya juu chini ili  kuyatatua Kwa hivyo, upanuzi wa mradi wa kuanzisha mashamba ya pamoja na nchi za Afrika ulikuwa mojawapo ya miradi ya maendeleo iliyofanikiwa kuchangia programu za Maendeleo Endelevu katika nchi za Afrika,  pamoja na kuwasilisha  ujuzi wa kilimo wa Misri kwa ndugu waafrika, ambapo mradi wa kuanzisha mashamba ya pamoja na nchi za Afrika umeendelea kwa njia inayoonekana katika hali halisi tangu miaka iliyopita  pamoja na kutekeleza  malengo muhimu ya  mikakati yanayohusiana na kuongeza uzalishaji , kuwasilisha  Teknolojia na kutumia tafiti za kisasa kupitia kujenga uwezo na kuendeleza maeneo ya logistiki  ili kuimarisha  uwekezaji.

wakili wa Kituo cha Tafiti za Kilimo Dkt.Adel Abd El Azim aligusia shughuli za kituo kupitia kufuatilia  malisho yanayozalishwa ndani  na kuagizwa kutoka nje , kuboresha na kufanya upya njia ya uchambuzi ili kuzuia udanganyifu, kudhibitisha kitaifa  na  kimataifa na   kusaidia watafiti wa vyuo vikuu na  vituo vya Tafiti katika  shughuli zao za utafiti, kutekeleza programu za mafunzo kwa watafiti na mafundi katika nyanja  za uchambuzi mbalimbali .

Mwishoni mwa mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Mradi wa Mashamba ya Pamoja na Nchi za Afrika Dkt. " Maher Al-Maghraby "  alitoa onesho la kina lililosajiliwa  kwa vituo na shughuli za Mradi wa Mashamba ya Pamoja ya kimisri, haswa yale yatakayoendelea kuanzishwa mnamo kipindi kijacho.  pamoja na kujibu  maswali yaliyoulizwa na wajumbe,  ambayo miongoni mwao ni  athari za Covid 19 katika maendeleo ya kilimo, jinsi ya kugundua mbinu za kisasa kwa lengo la  kuendeleza programu na shughuli za kilimo kwa ujumla.

 

Inatakiwa kutajwa  kuwa Udhamini   wa Nasser wa Uongozi   wa Kimataifa  ni mwendelezo  wa juhudi za nchi ya Misri baada ya uongozi wake wa Umoja wa Afrika wakati  wa 2019 kutekeleza jukumu lake  katika kuimarisha mchango wa vijana waafrika  kwa  kutoa aina zote za misaada,  kujiwezesha  na mafunzo pia.

pamoja na kuwawezesha katika vyeo  vya uongozi na kufaidika kwa  uwezo na mawazo yao. vilevile , huzingatiwa mojawapo ya njia ya kutekeleza Mtazamo  wa Misri 2030 na  Misingi kumi ya Shirika la Mshikamano Afro-Asia na  Ajenda ya Afrika 2063, Malengo ya Maendeleo  Endelevu ya 2030, Ushirikiano wa Kusini- Kusini , Mwenendo  wa Umoja wa Afrika kuhusu uwekezaji kwa vijana na Hati ya Vijana wa Afrika.