Misri ni Lango la Kiafrika kwa Kupita China

Misri ni Lango la Kiafrika kwa Kupita China

Imetafsiriwa na/ Mahmoud Ragab
Imehaririwa na/ Fatma Elsayed

Katika maadhimisho ya miaka 72 ya kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China. tunakumbuka hatua muhimu zaidi za maendeleo ya uhusiano wa Misri na China, ambapo Misri ni nchi ya ishirini na tatu kutambua Jamhuri ya Watu wa China na ya kwanza katika nchi za Kiarabu na Afrika.

 Katika Aprili 1955, Kiongozi Gamal Abdel Nasser na kiongozi wa China Xu Enlai, Waziri Mkuu wa kwanza wa Jamhuri ya Watu wa China, walikutana huko Bandung, Indonesia, wakati wa mkutano wa kilele wa Afrika na Asia; ili kujadili njia za ushirikiano kati yao.

 Na katika Mei 1956, uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili ulianza baada ya serikali ya Misri na China zimetoa taarifa ya pamoja kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia katika ngazi ya wabalozi wa nchi hizo mbili.Hatua hiyo ilikuwa nukta muhimu zaidi katika  uhusiano wa Mataifa ya China.Ambapo Jukumu la upainia la Misri lilikuwa katika ngazi za Waarabu na Waafrika
zilikuwa na athari kubwa katika uwanja wa kimataifa, na baadaye kutambuliwa kwa Jamhuri ya Watu wa Uchina.

 Mnamo Julai 1956, China iliunga mkono uamuzi wa Rais Gamal Abdel Nasser wa kutaifisha mfereji wa Suez.Pia ilishutuma  adui tatu dhidi ya Misri.Uungaji mkono na uungwaji mkono wa watu wa China kwa Misri ulionekana wakati moja ya maandamano makubwa zaidi yalifanyika nchini China kushutumu uchokozi na kusaidia mapambano ya watu wa Misri.

 Misri pia ilitaka kupata suluhu ya mzozo wakati wa Vita vya India-China mwaka 1962, na Rais Abdel Nasser alikuwa akiwasiliana mara kwa mara na Chou Enlai na Lal Bahadur Shastri, Waziri Mkuu wa India.

 Xu Enlai pia alitembelea Misri Desemba 1963, ambapo alifanya mazungumzo na Rais Gamal Abdel Nasser na kutoa hotuba  akasema: "Hii ni mara ya kwanza ninatembelea Jamhuri ya Muungano wa Kiarabu na mara ya kwanza nimetembelea Bara la Afrika ,  na ningependa kueleza  niaba ya watu wa China.” Salamu na heshima kubwa kwa watu wa Jamhuri ya Muungano wa Kiarabu."

 Uhusiano kati ya nchi hizi mbili na ushirikiano katika nyanja mbalimbali uliendelea kwa  kubadilishana ziara za hali ya juu na kubadilishana wajumbe wa wanafunzi, kitaaluma, kiutamaduni na wengine.

 Kwa upande wa uchumi , China ni mshirika mkubwa wa kibiashara wa Misri, na Misri inachukuliwa kuwa mshirika wa tatu wa biashara wa China barani Afrika. Pia  Kiwango cha kubadilishana biashara kati ya nchi hizo mbili kiliongezeka kutoka 12.2 dola milioni  mwaka 1954 hadi 452 dola milioni  mwaka 1955,  kisha zaidi ya 10 mabilioni ya dola mwaka 2013  yaani, imeongezeka takribani mara elfu moja katika kipindi cha miaka sitini.


 Mratibu wa lugha ya kiswahili/ Tasneem Hamdy