Josip Broz Tito

Josip Broz Tito
Josip Broz Tito
Josip Broz Tito
Josip Broz Tito
Josip Broz Tito
Josip Broz Tito
Josip Broz Tito
Josip Broz Tito
Josip Broz Tito

Josip Tito amezaliwa tarehe Mei 7, 1892, katika kijiji cha Kumrovec karibu na mji mkuu wa Croatia Zagreb, naye ni  mtoto wa saba wa baba wa Croatia na mama wa Slovenia aitwaye Marija. Tito alijiunga kwa shule ya msingi mwaka 1900 na hakumaliza elimu yake kutokana na umaskini, mnamo mwaka 1907, Tito alisafiri hadi jiji akitafutia kazi hadi kupata alichotaka katika moja ya viwanda huko Sisak, Kuanzia 1908-1913 alijishughulisha na taaluma ya uhunzi, hadi alipoandikishwa katika Jeshi la Austro-Hungarian mnamo 1913, alimaliza mafunzo ya afisa asiye na kamisheni na mara baada ya kuzuka kwa Vita vya Kwanza vya Dunia, alitumwa kupigana huko Budapest,Miaka miwili baada ya vita,alitumwa kwa Eneo la Mashariki la Mapigano kwa kupigana dhidi ya Warusi, lakini alijeruhiwa katika moja ya vita na alitekwa na vikosi vya Urusi.

Josip Tito alikaa karibu miezi kumi na tatu katika hospitali ya Urusi akipokea matibabu, na baada ya kupona alipelekwa kwenye kambi ya watekwa huko Ural, ambapo wafungwa walimchagua kama kiongozi wao. Mara moja baada ya kuzuka Mapinduzi ya Bolshevik yaliyoongozwa na Vladimir Lenin mwaka 1917, yaliyokuwa na lengo la kuupindua utawala na kutekeleza ukomunisti nchini humo, jela hiyo ilishambuliwa na wafungwa wote kuachiwa huru. Na miongoni mwao alikuwa Josip Tito, aliyeanza kuunda mwamko mpya wa kisiasa, na kutoka hapa upendo wake kwa ukomunisti ukazidi, na alipendezwa sana na sera ya Vladimir Lenin, na maoni ya mapinduzi ya Bolshevik, yaliyolenga kupata uhuru, usawa, na mgawanyiko wa utaifa na ukabila, unaoteseka na nchi yake ya Yugoslavia, Aliazimia kutekeleza kanuni hizi katika nchi yake, kuunganisha safu zake, na kuinua msimamo wake kati ya mataifa msisitizo wake huo ulimsukuma kupigana vita vingi.

 Tito alijiunga na Walinzi Wekundu na kujiunga na Chama cha Kikomunisti cha Urusi ili kukabiliana na serikali ya Urusi katika mwaka 1918, Na alishiriki katika mapinduzi ya Bolshevik, na haukupita muda mrefu kabla ya kukamatwa tena, lakini alifanikiwa kutoroka na kushiriki katika maandamano huko Saint Petersburg, lakini akakamatwa tena na kufungwa katika ngome ya Paul Peter, Na iliamuliwa kumfukuza nje ya nchi, na katikati ya barabara, Tito aliruka kutoka kwa gari moshi na kukimbia, Na alijificha pamoja na familia ya Warusi huko Omsk, Siberia, na huko alikutana na mke wake, Pelagia Belousova.

Alirudi katika nchi yake na kujiunga na Chama cha Kikomunisti cha Yugoslavia katika mwaka 1920, kilichoongeza nafasi yake nchini na kushinda katika uchaguzi uliofanyika kwa viti 59 baada ya mafanikio ya mapinduzi ya Bolshevik kupindua utawala wa Urusi , na kuanzishwa kwa Ukomunisti kwenye uwanja wa kisiasa. Na Wakati huo, Wakomunisti walifurahia uhuru mkubwa zaidi kuliko hapo awali katika kutekeleza shughuli zao za kisiasa, kutokana na kutawala kwa Umoja wa Kisovyeti - mkuu wa ukomunisti - nchini, Lakini ghafla hali ilibadilika na kuwa kinyume, na mauaji ya mwanasiasa Milorad Drachkovitch, ambapo tuhuma zilirushwa kwa Wakomunisti,Vyama vya Kikomunisti vilipigwa marufuku na kuanza Wakomunisti walifukuzwa na kutiwa gerezani, na wengi wao hata waliuawa.

Na kwa kuendelea kule kubanwa suala la wakomunisti, Tito aliamua kuhamia mji wa Trojstvo, na mbali na ulimwengu wa siasa.Na Huko, alianza kuandika, lakini hakuweza kukaa mbali, kwa hiyo alianza tena shughuli yake ya siri ya ukomunisti,na Alianzisha tawi la Chama cha Kikomunisti cha Yugoslavia huko Zagreb, na hivi karibuni alifichuliwa na kufungwa kwa miaka mitano, Na Huko Tito alikutana na mwenzake wake Musa Bijadi, na baada ya kuachiliwa walirudi kwenye shughuli zao za kimapinduzi kwa majina bandia, Qualter na Tito.

Halmashauri Kuu ya tawi la Zagreb ilimtuma Tito huko Vienna ili kushirikiana katika mkutano mkuu wa Chama cha Kikomunisti cha Yugoslavia katika mwaka 1934, , Na Alichaguliwa kuwa mwanachama wa ofisi ya siasa ya chama pamoja na Eduard Milovan na Aleksandar Ranković. Mnamo 1935, alisafiri kwenda Umoja wa Kisovyeti na kufanya kazi kwa mwaka mmoja katika Comintern, na kuwa afisa mashuhuri katika Jumuiya ya Mambo ya Ndani ya Watu, Na Alitumwa na kikosi maalum kushiriki katika Vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Uhispania kuwaunga mkono Jamhuri na wa kushoto, Mnamo 1937, Stalin alimpa kazi ya kukaa Yugoslavia ili kupanga Chama cha Kikomunisti cha Yugoslavia.

Mnamo Aprili 6, 1941, baada ya kuzuka kwa Vita vya Dunia vya pili, Ujerumani iliivamia Yugoslavia kwa msaada wa vikosi vya Italia na Hungarian, Josip Tito aliunda kamati ya kijeshi ndani ya Chama cha Kikomunisti cha Yugoslavia,haswa baada ya Mfalme Peter kukimbia na jeshi la serikali kuanguka, Alitoa tamko la kuwataka wananchi kupinga na kutoa wito wa Umoja katika kipindi na uvamizi hiyo. Mnamo tarehe ishirini na saba Juni mwaka huo huo; Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha Yugoslavia ilitangaza kumteua Tito kuwa Kamanda Mkuu wa Majeshi kwa juhudi zake dhidi ya Unazi na washirika wake.

Operesheni za kijeshi za Yugoslavia ziliongezeka na upinzani wao ulikuwa  matokeo mazuri sana,na Wajerumani walielekeza nguvu zao katika kuzima upinzani, Walijaribu kumuua Tito mara tatu, mojawapo lilifanyika Mei 25,1944, Na Ndege zao ziliposhambulia makao makuu ya Tito huko Bosnia, lakini aliokolewa. Na mnamo Tarehe ishirini na nane Septemba 1944, Tito aliruhusu Jeshi Nyekundu kuingia Yugoslavia na kutekeleza operesheni za kijeshi ili kuondoa ngome za mwisho za uvamizi wa Wajerumani, Kisha Jeshi la Ukombozi la Yugoslavia lilianzisha shambulio kubwa na kufanikiwa kuvunja ulinzi wa Wajerumani, waliolazimika kujiondoa kutoka Yugoslavia, Kwa hivyo, Tito alishinda na Yugoslavia ikakombolewa kutoka kwa uvamizi.

 Josip Tito akawa Waziri Mkuu mnamo mwaka 1934, na akateuliwa kuwa rais wa kwanza wa Jamhuri ya Yugoslavia mnamo 1953, Na alipata daraja la Marshal Kama Kamanda Mkuu wa Jeshi la Yugoslavia, Aliidhinisha katiba mpya na kujenga upya jeshi la Yugoslavia, lililokuwa mojawapo ya majeshi yenye nguvu zaidi ya Ulaya wakati huo.

Tito alikuwa mtetezi kutofungamana kwa upande wowote na mpinzani wa sera ya Joseph Stalin, kiongozi wa Umoja wa Kisovieti, Daima ametetea umuhimu wa njia nyingi za kufikia ujamaa. Hebu kila nchi iwe na mbinu inafaa kutembea kwake, jambo ambalo Stalin hakupenda, na akaona uasi ndani yake, na kuondoka kutoka kwa ujamaa wa kweli,Alimfukuza Tito kutoka kwa Comintern. Aliita sera yake "Ukomunisti wa Tito" kama aina ya kejeli na kudharau sera yake, Na baada ya muda, jina hili lilitumika kwa mikondo yote ya kikomunisti ambayo ilitetea uhuru wa kitaifa na haikukubali ujamaa wa Umoja wa Soviet.

Baada ya kujitenga kwa Tito kutoka Umoja wa Kisovieti, alibadilishana misaada ya kiuchumi na nchi za Jumuiya ya Asia na Afrika, Lakini hakukubali msaada kutoka Magharibi, na baada ya kifo cha Stalin mnamo 1953 na Tito alianza kurudisha uhusiano wake na Muungano wa Sovieti, Tito hakutaka kuwa na mtu yeyote wakati wa Vita Baridi.

Mwishoni mwa 1954, mkutano wa kwanza wa Gamal Abdel Nasser na Tito ulifanyikwa, ukifuatiwa na kukaa tena katika jiji la Indonesia la Bandung mnamo mwaka 1955 Rais Josip Tito alipokutana na kiongozi wa Misri Gamal Abdel Nasser wakati wa Mkutano wa Bandung, ulioitishwa na mpiganaji marehemu Ahmed Sukarno, Rais wa Indonesia wa wakati huo, Ilihudhuriwa na nchi 29 kutoka mabara ya Asia na Afrika, na Ilihudhuriwa na Waziri Mkuu wa India Jawaharlal Nehru na Chuan Lai ya Kichina. Matokeo yake makuu yalikuwa ni kuanzishwa kwa Kundi la Afro-Asian katika Umoja wa Mataifa, na kisha Harakati ya kutofungamana kwa upande wowote.

Alikuwa na uhusiano mkubwa na kiongozi wa Misri Gamal Abdel Nasser, ambaye alimchukulia kuwa rafiki yake bora. Rais Josip Tito alitembelea Kairo mara kadhaa, na nguvu ya uhusiano huu ilionekana wakati wa vita, kwani alikata mahusiano yote ya kidiplomasia na Israeli baada ya vita vya 1967, na Tito alilisaidia jeshi la Misri kwa vifaru 100 ili kufidia hasara ya jeshi la Misri, na katikati ya mji mkuu wa Misri,Kairo, ni moja ya mitaa na vitovu vyake muhimu zaidi iliitwa na Josip Tito.

 Hali ya afya ya Rais Josip Tito ilizidi kuwa mbaya, kwani alikuwa akisumbuliwa na kuziba kwa mshipa katika mguu wake wa kushoto mnamo mwaka 1979, na baada ya safari ndefu ya matibabu, madaktari waliamua kuukata mguu, na hali ikawa mbaya zaidi na kuaga Dunia Mei 4, 1980, Na kutangaza maombolezo katika Jamhuri ya Yugoslavia kwa siku saba, mazishi mazito yaliandaliwa, yakihudhuriwa na viongozi na wakuu wengi kutoka nchi mbalimbali za Dunia.