Sikukuu ya Wafanyikazi nchini Uganda

Sikukuu ya Wafanyikazi nchini Uganda

Sikukuu ya  wafanyikazi   inajulikana kama Siku ya Wafanyikazi Duniani na  sikukuu ya Mei. Nayo ni  likizo  rasmi katika nchi nyingi Duniani kwa wakazi ,  na shule na  makupuni  mengi hufungwa. Na kawaida yake inakuja mnamo Mei mosi, lakini nchi kadha husherehekea  mnamo tarehe zingine,tena Sikukuu  hiyo kawaida huhusishwa na kumbukumbu  ya mafanikio ya Harakati za Wafanyikazi.

Maadhimisho ya kwanza ya Sikukuu ya Wafanyikazi yalifanyikwa Mei mosi, 1890, na hayo  baada ya   Kongamano la Kwanza la Kimataifa kwa Vyama vya Kiujama  huko Ulaya mnamo  Julai 14, 1889 huko Paris, lilipotangaza kuainisha Mei mosi ya kila mwaka kuwa  "Siku ya Wafanyikazi kwa Umoja  na   Mshikamano wa kimataifa .”

Tarehe hiyo ilichaguliwa kwa sababu ya matukio ya upande wa  mwingine wa Atlantiki, ambapo  mnamo 1884,  Umoja wa Marekani wa  biashara iliyopangwa na Vyama vya Wafanyikazi  zilidai siku ya kazi iwe  masaa manane; kisha kuanza kuitekeleza kuanzia t Mei mosi, 1886.
Na hiyo ilisababisha mgomo wa umma na ghasia za Chicago Haymarket, lakini hatimaye  imeshaidhinishwa rasmi  kwa masaa manane kwa siku ya  kazi  .

  kwa miaka mingi, wanawake wengi nchini Uganda wamenyimwa haki ya kupiga kura katika sekta rasmi ya kibiashara kutokana  ukosefu wa fursa ya kupata  mikopo nafuu,  ukosefu wa ujuzi wa kiufundi unaohusiana na  kupanga miradi ya biashara na usimamizi wake , na ukosefu wa  kupatikana  masoko pamoja na taarifa zinazohusiana na  fursa za biashara, na kwa kutatua tatizo hilo,  Serikali ya Uganda mnamo mwaka wa fedha wa 2015/2016,  ilizindua Mpango wa Ujasiriamali wa Uganda kwa lengo kuu la wawezeshe wanawake wa Uganda kuboresha viwango vyao vya mapato na kuchangia maendeleo ya kiuchumi.

Na hiyo pia ni kutokana na michango ya  Umoja wa Wanawake Waafrika  wanaotetea haki ya  kupatikana  Ajira  kwa  wanawake wa vijijini.

Hatimaye,  Sikukuu ya Wafanyikazi nchini Uganda sio tu kumbukumbu ya kusherehekea, bali  ni maadhimisho ya kimataifa ya kupata haki zao.