Mahusiano kati ya Misri na Tanzania: Mahusiano ya Kihistoria Imara na Ushirikiano wa Kijumla

Imetafsiriwa na: Noran Ahmed Mohammed saeed na Shahd Mohammed El.Sayed
Imehaririwa na: Mervat Sakr
Mratibu wa Lugha ya Kiswahili: Mervat Sakr
Sasa, tunapokabiliwa na hatua muhimu katika mageuzi ya diplomasia ya kimataifa na maendeleo ya uwakilishi wa kidiplomasia duniani kote huku migogoro ya kijeshi ikiendelea, serikali ya Misri inatilia mkazo mkubwa nguvu na uwezo ambao mahusiano ya kidiplomasia na nchi za Afrika yanaweza kuleta. Hii inajumuisha kufungua upeo mpya na kuimarisha njia za ushirikiano wa pamoja kati ya Misri na mataifa ya bara hili katika nyanja zote za kisiasa, kiuchumi, kitamaduni na kijeshi.
Kwa msingi huu, Misri imekuwa ikidumisha na kuimarisha ushirikiano wa karibu na mataifa ya Afrika Mashariki, huku mojawapo ya mifano mashuhuri ya ushirikiano huu ikiwa ni mahusiano ya karibu kati ya Misri na Tanzania. Hii ni ili kufanikisha uongozi wa asili na uongozi wa Misri barani Afrika, kutokana na misimamo na ushawishi mpana wa Misri kimataifa, kwa lengo la kufikia maslahi ya watu wa bara zima, hivyo Misri ina nia ya kuimarisha ushirikiano wenye matunda na ndugu wa Afrika... Aina maarufu za ushirikiano kati ya Misri na nchi za Afrika Mashariki zilikuwa mahusiano ya karibu wa Misri na nchi dada ya Tanzania.
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Tanzania ni mojawapo ya mataifa muhimu zaidi katika Afrika Mashariki na ni miongoni mwa nchi zinazounda Bonde la Mto Nile. Ipo katika eneo la kimkakati, ikipakana na Bahari ya Hindi upande wa mashariki, Kenya na Uganda upande wa kaskazini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Rwanda, na Burundi upande wa magharibi, na Msumbiji, Malawi, na Zambia upande wa kusini.
Jina "Tanzania" linatokana na muunganiko wa majina "Tanganyika" na "Zanzibar", ambazo ziliungana mnamo mwaka 1964 kuunda Jamhuri ya Shirikisho la Tanganyika na Zanzibar, jina ambalo baadaye mwaka huo huo lilibadilishwa kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rais wa sasa wa Tanzania ni Samia Suluhu Hassan. Kiswahili ni lugha ya taifa, huku Kiingereza kikiwa lugha rasmi ya elimu, biashara, na mawasiliano ya kimataifa. Aidha, Kiarabu kinazungumzwa zaidi katika visiwa vya Zanzibar, sambamba na lugha nyingine za kienyeji.
Tanzania ni mwanachama hai wa mashirika na jumuiya mbalimbali za kikanda na kimataifa, ikiwemo:
• Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)
• Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)
• Umoja wa Afrika (AU)
• Kundi la 77 (G77)
• Jumuiya ya Endojo
Hapa kuna muhtasari wa hatua muhimu za ushirikiano wa kihistoria kati ya Misri na Tanzania.
Mahusiano ya Misri na Tanzania katika Enzi ya Khedive Tawfiq – 1882
Mwandishi na mwanahistoria wa Misri, Muwafaq Bayoumi, alifichua nyaraka za kihistoria zinazoonesha mahusiano ya muda mrefu kati ya Misri na Tanzania. Alibainisha kuwa Misri imekuwa na uwepo thabiti barani Afrika tangu zamani, akionesha hati ya mwaka 1882, inaoeleza mojawapo ya sura muhimu za ushirikiano wa kitamaduni kati ya nchi hizi mbili, ikiwemo kusambazwa kwa muziki wa Kimisri hadi Tanzania.
Mahusiano ya Misri na Tanzania Wakati wa Uongozi wa Gamal Abdel Nasser na Julius Nyerere
Mahusiano ya Misri na Tanzania yalijengwa kwa misingi imara hata kabla ya kuundwa kwa Muungano wa Tanzania mnamo mwaka 1964, na hata kabla ya Tanganyika kupata uhuru wake mnamo mwaka 1961.
Mnamo mwaka 1954, viongozi wa Afrika walianzisha Tanganyika African National Union (TANU) chini ya uongozi wa Julius Nyerere na wenzake, wakipigania uhuru kamili wa Tanganyika. Juhudi hizi zilipata msaada mkubwa kutoka kwa Gamal Abdel Nasser, ambaye aliunga mkono harakati hizo hadi Tanganyika ilipopata uhuru wake kwa kura ya wengi mnamo mwaka 1961.
Katika mwaka huo huo (1954), Redio ya Misri ilianza kutangaza vipindi maalum kwa lugha ya Kiswahili, vikilenga wakazi wa Afrika Mashariki, kwa muda wa dakika 90 kila siku.
Mnamo mwaka 1961, Misri, chini ya uongozi wa Gamal Abdel Nasser, iliendelea kuunga mkono juhudi za uhuru wa Tanganyika na Zanzibar kutoka kwa utawala wa Uingereza. Kwa msaada wa Misri, Zanzibar na Tanganyika zilifanikiwa kupata uhuru, na baadaye Misri ilihamasisha umoja kati yao. Misri ilikuwa miongoni mwa mataifa ya kwanza kuunga mkono kuundwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kutoa msaada wa haraka baada ya kuanzishwa kwake.
Mahusiano ya Kidiplomasia
Mahusiano rasmi ya kidiplomasia kati ya Misri na Tanzania yalianza mnamo mwaka 1964, wakati Salim Ahmed Salim alipoteuliwa kuwa balozi wa kwanza wa Tanzania nchini Misri, mara baada ya kuundwa kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Mikutano na Ziara Rasmi za Viongozi
Mnamo mwaka 1966, Gamal Abdel Nasser alifanya ziara rasmi nchini Tanzania, ambako alikutana na Rais Julius Nyerere pamoja na viongozi wa Chama cha TANU. Mazungumzo yao yalihusu ushirikiano wa kusaidia mataifa ya Afrika ambayo bado yalikuwa yanapigania uhuru, pamoja na njia za kuimarisha Umoja wa Afrika.
Urafiki wa karibu uliendelea kati ya viongozi hawa wawili, kutokana na kufanana kwa sera zao. Nyerere nchini Tanzania na Nasser nchini Misri walifuata sera za ujamaa, na wote walikuwa na mtazamo wa pamoja kuhusu masuala ya bara la Afrika na diplomasia ya kimataifa.
Mojawapo ya matukio yanayoakisi mshikamano wao ni ziara ya kihistoria ya Rais Julius Nyerere nchini Misri, ambapo Gamal Abdel Nasser alimsindikiza hadi katika Bunge la Misri, ishara ya heshima kubwa na mshikamano kati ya mataifa yao mawili.
Mifano ya Ushirikiano Kati ya Misri na Tanzania
- Ushirikiano wa Kibiashara
Mnamo mwezi Februari mwaka 1967, serikali za Misri na Tanzania zilisaini protokali ya biashara, kama mwendelezo wa mkataba wa biashara uliotiwa saini mnamo mwaka 1964.
- Ushirikiano wa Kitamaduni:
Mojawapo ya hatua muhimu za ushirikiano wa kitamaduni kati ya Misri na Tanzania katika kipindi hicho ilikuwa kuanzishwa kwa Kituo cha Kiislamu cha Misri jijini Dar es Salaam, kilichofunguliwa rasmi mnamo mwaka 1968.
Misri iligharamia kikamilifu ujenzi na uendeshaji wa kituo hicho, ambacho kinahudumia zaidi ya wanafunzi 1,400 katika ngazi mbalimbali za elimu. Kila mwaka, kituo hicho hutuma zaidi ya wanafunzi 20 kuendelea na masomo katika Chuo Kikuu cha Al-Azhar nchini Misri.
Pia, Misri ilitoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wa Zanzibar na kutuma walimu wa Misri kusaidia kuinua kiwango cha elimu visiwani humo.
Mahusiano ya Misri na Tanzania Kipindi cha Hayati Rais Anwar Sadat
Mikataba Kati ya Nchi Hizi Mbili
Mnamo tarehe Agosti 3, 1977: Misri na Tanzania zilisaini mkataba wa biashara, kwa madhumuni ya kuimarisha na kukuza mahusiano ya kibiashara kwa misingi ya usawa na manufaa ya pamoja.
Mnamo mwaka 1980: Misri na Tanzania zilisaini mkataba mkuu wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.
Mnamo tarehe Septemba 8, 1981: Kusainiwa kwa mkataba wa ushirikiano wa kiufundi kati ya Mfuko wa Misri wa Ushirikiano wa Kiufundi na Tanzania.
Ushirikiano wa Kiufundi
Mnamo tarehe Februari 1981: Baada ya kuanzishwa kwa Mfuko wa Misri wa Ushirikiano wa Kiufundi na Afrika, na kuanza kwa shughuli zake mwanzoni mwa miaka ya 1980, Misri na Tanzania zilisaini makubaliano ya ushirikiano wa kiufundi kwa kubadilishana hati na nyaraka rasmi.
Mahusiano ya Misri na Tanzania Kipindi cha Hayati Rais Mohamed Hosni Mubarak (1999-2003)
Mikutano ya Marais
Mnamo Julai 1999: Rais wa Tanzania Benjamin Mkapa alitembelea Misri na kufanya mazungumzo na Rais Hosni Mubarak kuhusu masuala ya kiuchumi na njia za kuimarisha mahusiano kati ya nchi hizo mbili ili yaendane na nguvu ya ushirikiano wao wa kisiasa.
Mnamo tarehe Januari 21, 2003: Rais Mkapa alifanya ziara ya pili nchini Misri kwa mazungumzo kuhusu masuala ya bara la Afrika, njia za kuimarisha ushirikiano wa pande mbili, na kushughulikia migogoro ya kikanda na kimataifa yenye maslahi ya pamoja.
Ushirikiano wa Kiuchumi
Mnamo Machi 2000: Mamlaka ya Uwekezaji ya Misri ilijadili uwezekano wa kuanzisha miradi ya pamoja kati ya Misri na Tanzania, hasa katika sekta za viwanda vya chakula, madini na kilimo. Pia, mazungumzo yalihusisha uwezekano wa kusambaza teknolojia ya Misri kwa Tanzania na kusaidia katika mafunzo ya wafanyakazi wa sekta ya viwanda nchini Tanzania.
Mnamo Julai 2003: Waziri wa Biashara na Viwanda wa Tanzania alikutana na Waziri wa Biashara ya Nje wa Misri, ambapo walikubaliana juu ya umuhimu wa kuanzisha eneo huru la biashara kati ya nchi hizo mbili ili kuongeza uwekezaji na kuimarisha biashara ya pande zote.
Mnamo Desemba 2003: Misri ilishiriki katika maonesho ya kibiashara ya Afrika yaliyofanyika katika mji mkuu wa Tanzania, Dar es Salaam.
Mikataba na Makubaliano
Misri na Tanzania ni wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) pamoja na mashirika mengine ya kikanda barani Afrika. Aidha, kuna makubaliano kadhaa ya ushirikiano kati ya nchi hizo, yakiwemo:
Mnamo Mei 1999: Misri, Tanzania, na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) zilisaini mkataba wa kutekeleza mpango wa usalama wa chakula nchini Tanzania.
Mnamo Oktoba 2002: Misri na Tanzania zilisaini mkataba wa kuanzisha Baraza la Biashara la Tanzania na Misri, kati ya Chama cha Wafanyabiashara wa Misri na Shirikisho la Vyama vya Biashara, Viwanda na Kilimo la Tanzania. Pia, pande zote zilijadili makubaliano ya kubadilishana misamaha ya ushuru wa forodha, kwa lengo la kupunguza ushuru wa bidhaa baina ya nchi hizo mbili.
Mahusiano ya Misri na Tanzania Rais Adly Mansour Rais Jakaya Kikwete 2012-2013-2014:
- Ushirikiano katika Sekta ya Afya:
Mnamo tarehe Februari 2012, Misri ilitoa msaada wa mashine ya X-ray kwa Hospitali ya Polisi jijini Dar es Salaam, na kuandaa chumba cha maiti kamili kwa hospitali hiyo hiyo. Pia, ilifanya ukarabati mkubwa wa jengo la upasuaji katika Hospitali ya Bagamoyo, na Shirika la Misri la Ushirikiano wa Maendeleo lilipeleka kitengo kamili cha upasuaji wa laparoscopic ya figo, pamoja na mashine 4 za dialysis.
Mnamo Aprili 2013, hati ya makubaliano ya pamoja kati ya Misri na Tanzania ilisainiwa katika sekta ya afya.
Mnamo miaka ya 2014 na 2015, ujumbe wa matibabu ulifanya ziara Tanzania kufanya upasuaji na kutibu baadhi ya watoto waliokuwa wanahitaji huduma ya haraka ya matibabu.
-Ushirikiano katika Sekta ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari:
Mnamo Septemba 2012, Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania alijadili na mwenzake wa Misri njia za ushirikiano kati ya Misri na Tanzania katika uwanja wa mawasiliano, na jinsi ya kufaidika na uzoefu wa Misri katika kukuza sekta hii muhimu, hasa uzoefu wa Misri wenye mafanikio katika uanzishwaji wa vijiji vyenye teknolojia.
Mikutano ya Kubadilishana Kati ya Wajumbe wa Nchi Hizo Mbili:
Mnamo Februari 2014, Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Nabil Fahmy, alifanya ziara Tanzania kuwasilisha hotuba kutoka kwa Rais Adly Mansour kwa Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete. Hotuba hiyo ilijumuisha maono ya Misri ya kuimarisha mahusiano ya pande mbili na Tanzania katika nyanja mbalimbali za kisiasa, kiuchumi, kibiashara na kijeshi.
Mnamo Aprili 2014, Waziri Mkuu wa zamani, Ibrahim Mahlab, alielekea Tanzania kujadili mahusiano ya Misri na Tanzania, na alisisitiza kuhusu umuhimu wa kuimarisha mahusiano yake na ndugu wa Tanzania na bara la Afrika kwa ujumla.
Mnamo Juni 2014, Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, alifanya ziara Misri kuongoza ujumbe wa kushiriki katika sherehe za kuapishwa kwa Rais Abdel Fattah al-Sisi kama Rais wa Misri. Nabil Fahmy, Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, alikutana naye, na mkutano huo ulijadili kuanza tena kwa shughuli za Misri ndani ya Umoja wa Afrika. Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania alikaribisha kurudi kwa Misri katika shughuli za Umoja wa Afrika, na pande hizo mbili zilijadili njia za kuunga mkono ushirikiano wa kikanda kuhusu masuala ya Afrika, hasa kuhusiana na njia za kufikia maendeleo katika bara la Afrika.
Majadiliano yalidhihirisha/yalionesha mwafaka/makubaliano wa maoni kuhusu umuhimu wa kuipa kipaumbele ajenda ya maendeleo barani Afrika, na kutatua migogoro kwa njia za amani ili kuwezesha juhudi za maendeleo kufanyika kwa ufanisi.
Mnamo Desemba 2014, Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania wakati huo, alifanya ziara ya pili Misri. Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Sameh Shoukry, alimkaribisha, na pande hizo mbili zilijadili mahusiano ya pande mbili na masuala muhimu ya kikanda na kimataifa ya maslahi ya pamoja.
MAENDELEO YA MAHUSIANO KATI YA MISRI NA TANZANIA WAKATI WA UTAWALA WA RAIS ABDEL FATTAH EL-SISI NA MAREHEMU JOHN MAGUFULI (2015 – 2021)
Mikutano na Mawasiliano kati ya Marais wa Nchi Hizi Mbili:
Mnamo tarehe Januari 31, 2017 – Rais wa Misri, Abdel Fattah El-Sisi, alikutana na Rais wa Tanzania, John Magufuli, pembezoni mwa Mkutano wa Umoja wa Afrika uliofanyika Addis Ababa. Viongozi hao wawili walisisitiza uhusiano wa kihistoria na wa kipekee uliopo kati ya nchi zao. Rais El-Sisi alimwalika Rais Magufuli kutembelea Misri ili kuimarisha zaidi ushirikiano wa pande mbili. Kwa upande wake, Rais Magufuli alisifu nafasi ya uongozi ya Misri barani Afrika.
Mnamo tarehe Agosti 14, 2017 – Rais Abdel Fattah El-Sisi alifanya ziara rasmi nchini Tanzania, ikiwa ni ziara ya kwanza ya kiongozi wa Misri tangu mwaka 1968. Rais Magufuli, pamoja na maafisa waandamizi wa serikali, walimpokea rasmi Rais El-Sisi.
Wakati wa ziara hiyo, marais hao walifanya mazungumzo ya ana kwa ana, kisha wakafanya kikao cha mashauriano kilichohusisha ujumbe wa nchi zote mbili. Walikubaliana kuimarisha ushirikiano katika mapambano dhidi ya ufisadi na kufufua Kamati ya Pamoja kati ya nchi hizo kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi.
Aidha, Rais Magufuli alimwalika Rais El-Sisi kuweka jiwe la msingi la mradi wa Bwawa la Umeme la Stiegler’s Gorge, akionesha matumaini kuwa Rais El-Sisi ataliweka chini ya usimamizi wake, kama ilivyo kwa miradi mikubwa ya kitaifa nchini Misri.
Mnamo tarehe Oktoba 2018 – Rais Abdel Fattah El-Sisi alipokea simu kutoka kwa Rais John Magufuli, ambapo walijadili maendeleo ya mahusiano kati ya nchi zao, hasa katika nyanja za uchumi na biashara. Rais Magufuli alisifu uwekezaji wa Misri nchini Tanzania, hasa baada ya Kampuni ya Misri ya Arab Contractors kushinda zabuni ya ujenzi wa Bwawa la Umeme la Stiegler’s Gorge katika Bonde la Mto Rufiji, mradi ambao serikali ya Tanzania inauona kuwa wa kimkakati kwa uzalishaji wa umeme.
Mnamo Desemba 2018 – Rais El-Sisi alipokea simu nyingine kutoka kwa Rais Magufuli, ambapo walijadili maendeleo ya mradi wa Stiegler’s Gorge. Rais El-Sisi alisisitiza mshikamano wa Misri na Tanzania na kuelezea matarajio ya Misri ya kuimarisha zaidi mahusiano ya pande mbili. Aidha, walikubaliana kuongeza mshikamano wa kidiplomasia na kushirikiana katika masuala ya maendeleo ya bara la Afrika.
Ziara za Pande Mbili:
Mnamo Februari 2016 – Rais Magufuli alimkaribisha Balozi wa Misri nchini Tanzania na kueleza dhamira yake ya kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya nchi hizo mbili.
Mnamo Januari 2018 – Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Augustine Mahiga, alifanya ziara rasmi nchini Misri na kukutana na mwenzake wa Misri, Sameh Shoukry.
Mnamo Desemba 2018 – Waziri Mkuu wa Misri, Dkt. Mostafa Madbouly, alitembelea Tanzania kushiriki hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa Bwawa la Umeme la Stiegler’s Gorge, akimwakilisha Rais El-Sisi.
Mnamo Mei 2019 – Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Palamagamba Kabudi, alifanya ziara nchini Misri kwa mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili.
Mnamo Julai 2019 – Rais El-Sisi alimpokea Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, mjini Kairo, ambapo walijadili njia za kuimarisha mahusiano ya kibiashara na maendeleo ya miradi ya pamoja.
Mnamo Machi 2020 – Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Sameh Shoukry, alifanya ziara nchini Tanzania na kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania kwa mashauriano juu ya masuala ya ushirikiano wa pande mbili.
Mahusiano ya Kiuchumi:
Misri na Tanzania zimekuwa zikizingatia kuimarisha mahusiano yao wa kiuchumi kwa kuwekeza katika biashara, maendeleo na miradi ya uwekezaji.
Mnamo Januari 2018 – Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Misri na Tanzania waliongoza kikao cha tatu cha Kamati ya Pamoja ya Mawaziri kati ya nchi hizo mbili. Walijadili ushirikiano wa kiuchumi na masuala ya kikanda, na hatimaye kutia saini hati tatu za makubaliano katika sekta za mafunzo ya kidiplomasia, utalii, na kilimo.
Mnamo Julai 2018 – Ujumbe wa Mamlaka ya Maendeleo ya Viwanda ya Misri ulifanya mashauriano na ujumbe kutoka Tanzania kuhusu fursa za biashara na uwekezaji kati ya nchi hizo mbili.
Mnamo Novemba 2018 – Ujumbe wa Shirikisho la Viwanda la Misri, ukiongozwa na Dkt. Sherif El-Gabaly, ulifanya ziara nchini Tanzania kwa lengo la kutangaza bidhaa za Misri na kushirikiana na soko la Tanzania.
Mnamo Julai 2019 – Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, alitembelea Misri kwa mazungumzo kuhusu ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.
Mnamo Julai 2019 – Waziri wa Uwekezaji wa Misri, Dkt. Sahar Nasr, na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, walizindua Kongamano la Biashara kati ya Misri na Tanzania, likihudhuriwa na Waziri wa Kilimo wa Tanzania na wafanyabiashara kutoka mataifa yote mawili.
Mahusiano kati ya Misri na Tanzania umeendelea kuimarika katika nyanja za kisiasa, kiuchumi, na kijamii, na unaendelea kuwa chachu ya maendeleo kwa mataifa yote mawili.
MAENDELEO YA USHIRIKIANO KATI YA MISRI NA TANZANIA KATIKA SEKTA MBALIMBALI
Ushirikiano wa Kijeshi
Mnamo Novemba 2017: Waziri wa Nchi wa Uzalishaji wa Kijeshi wa Misri, Mohamed Said Al-Assar, alikutana na Mkurugenzi wa Shirika la Ujasusi na Huduma za Usalama la Tanzania, Modestus Kipilimba, ambapo walijadili njia za kuimarisha ushirikiano wa kijeshi. Waziri Al-Assar alihakikisha utayari wa Misri wa kutoa mahitaji yote ya Tanzania, ya kijeshi na ya kiraia, ili kuimarisha uhusiano wa pande mbili.
Mnamo Machi 2019: Rais wa Misri, Abdel Fattah El-Sisi, alimpokea Waziri wa Ulinzi na Huduma za Kitaifa wa Tanzania, Hussein Mwinyi. Rais alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa kijeshi kati ya nchi hizo mbili, hasa kutokana na mkutano wa Kamati ya Ushirikiano wa Kijeshi uliofanyika Kairo chini ya uongozi wa Mawaziri wa Ulinzi wa pande zote mbili.
Ushirikiano wa Kielimu na Kitamaduni
Misri inatoa ufadhili wa masomo katika fani mbalimbali zinazohitajika na Tanzania, zikiwemo udaktari, famasia, na uhandisi.
Pia, imeanzishwa idara maalum ya Kiswahili katika Kitivo cha Lugha cha Chuo Kikuu cha Ain Shams na Kitivo cha Lugha na Tafsiri cha Chuo Kikuu cha Al-Azhar.
Ushirikiano katika Sekta ya Afya
Mnamo Julai 2017: Shirika la Nile of Hope la Misri lilizindua msafara wa upasuaji wa watoto wenye matatizo ya kuzaliwa nao katika mji wa Zanzibar, ambapo ulifanyika upasuaji wa watoto zaidi ya 50 na uchunguzi wa kitabibu kwa watoto zaidi ya 200.
Ushirikiano wa Kihabari
Mnamo Januari 2018: Mkuu wa Shirika la Habari la Mashariki ya Kati la Misri, Ali Hassan, alipokea ujumbe wa wanahabari wa Tanzania ulioongozwa na Dkt. Jim J. Yotazi, Mhariri Mkuu wa Tanzania Standard Newspapers, kampuni kubwa ya habari nchini Tanzania. Walijadili ushirikiano wa kubadilishana habari kwa lengo la kuimarisha mahusiano kati ya mataifa hayo mawili.
Ushirikiano katika Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
Mnamo Novemba 2019: Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Misri alikutana na Naibu Waziri wa Mawasiliano wa Tanzania, Atashasta Nditiye, ambapo walijadili njia za kuimarisha ushirikiano katika sekta hiyo.
Ushirikiano wa Kibunge
Mnamo tarehe Aprili 3, 2019: Spika wa Bunge la Misri, Dkt. Ali Abdel Aal, alitembelea Tanzania na kukutana na Rais wa Tanzania, John Magufuli. Ali Abdel Aal alisisitiza kuwa Tanzania ni miongoni mwa mataifa ya kwanza aliyotembelea barani Afrika, akionesha dhamira ya kuimarisha mahusiano ya kibunge kati ya nchi hizi mbili.
Mnamo Juni 2019: Spika wa Bunge la Misri, Dkt. Ali Abdel Aal, alikutana na Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai, ambapo walikubaliana kuimarisha ushirikiano wa kibunge na kusisitiza umuhimu wa Kamati ya Urafiki wa Kibunge kati ya Misri na Tanzania kama daraja la kuimarisha mahusiano ya mabunge yao.
Mikataba na Makubaliano kati ya Nchi Mbili
Mnamo Aprili 2018: Wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la Biashara kati ya Misri na Tanzania, ilitiwa saini hati mbili za makubaliano kati ya Shirikisho la Viwanda la Misri na mashirika mawili ya kibiashara ya Tanzania: Chama cha Wafanyabiashara wa Tanzania na Chama cha Viwanda, Biashara na Kilimo cha Tanzania. Aidha, ilitiwa saini mkataba wa ujenzi wa kiwanda cha mbolea nchini Tanzania.
Ushirikiano katika Sekta ya Maji na Uzalishaji wa Umeme
Mnamo Desemba 2016: Waziri wa Rasilimali za Maji na Umwagiliaji wa Misri, Dkt. Mohamed Abdel Aty, alitembelea Tanzania na kukutana na mwenzake wa Tanzania, Gerson Lwenge, ambapo walijadili njia za kuimarisha ushirikiano katika usimamizi wa rasilimali za maji.
Wizara hiyo ilitekeleza mradi wa kuchimba visima 100 vya maji safi nchini Tanzania. Kati ya visima hivyo, 30 vilizinduliwa Januari 2013, na vingine vimeendelea kujengwa katika awamu mbalimbali.
Mradi wa Bwawa la Julius Nyerere (Stiegler’s Gorge) kwa Uzalishaji wa Umeme wa Maji
Mnamo Desemba 2018: Waziri Mkuu wa Misri, Dkt. Mostafa Madbouly, alihudhuria hafla ya kutia saini mkataba wa ujenzi wa Bwawa la Julius Nyerere katika Bonde la Mto Rufiji. Mradi huu, unaotekelezwa na kampuni za Arab Contractors na Elsewedy Electric kutoka Misri, utazalisha megawati 2,115 za umeme, huku ukiwezesha hifadhi ya maji na usambazaji wake nchini Tanzania.
Mnamo Julai 2019: Waziri wa Nishati wa Misri, Dkt. Mohamed Shaker, alikutana na viongozi wa Shirika la Umeme la Tanzania kujadili njia za kuimarisha ushirikiano wa pande mbili katika sekta ya nishati mbadala.
Mnamo Oktoba 2019: Waziri wa Nishati wa Tanzania, Medard Kalemani, alifanya ziara nchini Misri na kukutana na Waziri wa Nishati wa Misri, ambapo walijadili ushirikiano katika miradi ya nishati ya jua na upepo.
Mnamo Machi 2020, ujumbe wa wawakilishi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Umeme kutoka Zanzibar ulifanya ziara katika Mamlaka ya Nishati Mpya na Mbadala. Ziara hiyo ilihusisha uwasilishaji wa shughuli za mamlaka hiyo, pamoja na kujadili miradi ya nishati mbadala nchini Misri na maono yake kwa mwaka 2035.
Mnamo Novemba 2020, Waziri wa Nyumba Dkt. "Assem El-Gazzar" alikagua mradi wa ujenzi wa Bwawa na Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere kwenye Mto Rufiji, nchini Tanzania. Alisisitiza azma ya Rais "Abdel Fattah El-Sisi" ya kufuatilia maendeleo ya mradi huo mara kwa mara, katika muktadha wa uhusiano mzuri kati ya nchi hizo mbili na kujali kwa Misri masuala ya Afrika, sambamba na utekelezaji wa mradi huu muhimu kwa wananchi wa Tanzania.
Mnamo Novemba 2020, Tanzania ilisherehekea mchakato wa kugeuza mkondo wa Mto Rufiji kwa kuhudhuriwa na Waziri Mkuu wa Tanzania pamoja na Mawaziri wa Nyumba na Umeme wa Misri. Muungano wa makampuni ya Misri uliweza kukamilisha kazi za uchimbaji wa Bwawa la Julius nchini Tanzania, limelotekelezwa kwa ajili ya uzalishaji wa nishati ili kusaidia maendeleo ya Taifa la Tanzania.
Mnamo tarehe Novemba 18, 2020, Waziri Mkuu wa Tanzania "Kassim Majaliwa" alithibitisha kuwa mradi wa ujenzi wa Bwawa na Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere, kinachotekelezwa na muungano wa makampuni ya "Arab Contractors" na "Elsewedy Electric" kwenye Mto Rufiji, ni ushahidi wa mahusiano imara kati ya Misri na Tanzania chini ya uongozi wa Rais "Abdel Fattah El-Sisi" na Rais wa Tanzania "John Magufuli".
Majaliwa alisema kuwa kuna maagizo ya mara kwa mara kutoka kwa Rais El-Sisi na Rais Magufuli ya kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizo mbili, akisisitiza kuwa utendaji mzuri wa makampuni ya Misri yanayotekeleza mradi wa bwawa hilo ni ushahidi kwamba Wamisri na Watanzania ni ndugu. Alielekeza ujumbe wake kwa maafisa wa serikali ya Misri na makampuni ya ujenzi ya Misri, akisema: "Mna beba matumaini ya Watanzania."
Msaada uliotolewa kwa ndugu wa Kitanzania:
Mnamo Agosti 2016, ujumbe kutoka Chuo Kikuu cha Alexandria wenye madaktari saba ulitembelea Tanzania na kisiwa cha Zanzibar. Ziara hiyo ilikuwa katika muktadha wa makubaliano kati ya Chuo Kikuu cha Alexandria na Chuo Kikuu cha Muhimbili, ikilenga kuimarisha ushirikiano wa kiafya na kielimu kati ya vyuo hivyo viwili kwa ajili ya kufanya upasuaji kwa watoto.
Mnamo Desemba 2016, Misri ilituma misaada kwa waathirika wa tetemeko la ardhi lililopiga eneo la Kagera, kaskazini mwa Tanzania. Misaada hiyo ilihusisha vifaa tiba, vifaa vya matibabu vya dharura, pamoja na mahema ya kuwahifadhi wale waliopoteza makazi yao.
Upeo wa mahusiano ya Misri na Tanzania katika kipindi cha utawala wa Rais "Abdel Fattah El-Sisi" na Rais "Samia Suluhu Hassan" (2021-2024):
Mikutano na mawasiliano kati ya marais:
Mnamo tarehe Juni 9, 2021, Rais wa Misri "Abdel Fattah El-Sisi" alifanya mazungumzo kwa simu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. "Samia Suluhu Hassan", ambapo alimpongeza kwa kuchukua madaraka ya uongozi. Rais wa Misri alisisitiza mahusiano ya kipekee na ya kihistoria kati ya Misri na Tanzania, akieleza matarajio yake ya kushirikiana na Rais wa Tanzania ili kuimarisha uhusiano huo katika nyanja mbalimbali.
Kwa upande wake, Rais wa Tanzania alitoa shukrani zake kubwa kwa Misri, watu wake na uongozi wake, akieleza kuwa kuna fursa kubwa za kukuza ushirikiano na kuendeleza mahusiano kati ya mataifa hayo mawili. Alisisitiza pia mchango mkubwa wa Misri katika kusaidia juhudi za maendeleo nchini Tanzania.
Mnamo Novemba 2021, Rais "Abdel Fattah El-Sisi" alimkaribisha Rais wa Tanzania, Dkt. "Samia Suluhu Hassan", katika ziara yake rasmi ya kwanza nchini Misri. Mazungumzo ya pande mbili yalifanyika, yakifuatiwa na mazungumzo mapana kati ya ujumbe wa nchi hizo mbili.
Rais wa Misri alikaribisha Rais wa Tanzania na kusisitiza nia ya Misri kusaidia mahitaji ya maendeleo ya Tanzania, hasa katika sekta za miundombinu, umeme, afya, na kilimo, kupitia uwekezaji wa kampuni za Misri zenye uzoefu mkubwa katika nyanja hizo. Pia alieleza dhamira ya Misri kusaidia Tanzania kwa kutoa mafunzo na nafasi za masomo ili kujenga uwezo wa wataalamu wa Kitanzania.
Kwa upande wake, Rais Samia Suluhu Hassan alitoa shukrani zake kwa uhusiano wa muda mrefu na wa kipekee kati ya Tanzania na Misri, akisisitiza kuwa Tanzania inajali sana kukuza ushirikiano huo katika nyanja mbalimbali, hasa katika biashara na uchumi.
Aidha, alieleza dhamira ya nchi yake kuongeza ushirikiano wa kiufundi unaotolewa na Misri kwa wataalamu wa Kitanzania, pamoja na kushirikiana na kampuni za Misri katika sekta ya miundombinu. Alitaja pia mradi mkubwa wa ujenzi wa Bwawa la "Julius Nyerere", ambalo ni mfano wa kina wa uhusiano mzuri kati ya Tanzania na Misri.
Katika hitimisho la mazungumzo hayo, marais wote wawili walishuhudia hafla ya kutiwa saini kwa hati kadhaa za makubaliano kati ya nchi hizo mbili katika sekta za elimu ya juu, elimu ya msingi na sekondari, pamoja na sekta ya vijana na michezo.
Mnamo Novemba 2022, Rais Abdel Fattah El-Sisi alimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, pembezoni mwa Mkutano wa Kilele wa Dunia wa Mabadiliko ya Tabianchi (COP27). Mazungumzo yao yalihusu njia za kuimarisha mahusiano ya pande mbili, pamoja na kujadili maendeleo ya hivi karibuni kuhusu hali ya mambo barani Afrika. Viongozi hao wawili walisisitiza maoni yao yanayolingana kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa.
Mnamo Desemba 2023, Rais Abdel Fattah El-Sisi alikutana na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan pembezoni mwa Mkutano wa 28 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi huko Dubai. Mazungumzo yao yalijikita katika kuimarisha mahusiano ya pamoja, hasa kuhusu uwekezaji wa Misri nchini Tanzania, ushirikiano wa kiufundi, na kujenga uwezo kwa ajili ya kuwapa mafunzo wataalamu wa Kitanzania katika nyanja mbalimbali.
Mikutano na ziara za pande mbili kati ya ujumbe wa nchi hizo:
Mnamo Juni 2022, Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Sameh Shoukry, alimkaribisha mwenzake wa Tanzania, Liberata Mulamula. Walifanya kikao cha mashauriano ambapo walijadili ushirikiano wa kiuchumi,uratibu wa kisiasa, na mahusiano ya kihistoria unaoziunganisha nchi hizo mbili.
Maendeleo ya mahusiano ya kiuchumi kati ya nchi hizo mbili:
Mnamo tarehe Juni 12, 2021, kama sehemu ya mwendelezo wa msukumo mkubwa wa mahusiano ya kiuchumi kati ya Misri na Tanzania, Waziri wa Uwekezaji wa Tanzania, Geoffrey Mwambe, alizialika kampuni za Misri kuwekeza nchini Tanzania, hasa katika maendeleo ya viwanda, uendelezaji wa sekta ya kilimo, na uzalishaji wa bidhaa za kilimo. Waziri Mwambe alieleza kuwa kampuni za Misri zinaweza kufaidika na wingi wa malighafi zilizopo nchini Tanzania kama vile pamba, mafuta, chai, kahawa, na ngozi, badala ya kuzisafirisha nje kama bidhaa ghafi.
Kati ya tarehe 15 hadi 18 Juni 2021:
Katika jitihada za kuimarisha na kukuza mahusiano ya kibiashara kati ya nchi hizo mbili, Baraza la Kuuza Nje la Sekta ya Chakula lilitangaza kupeleka msafara wa kibiashara kwenda Tanzania kwa lengo la kuongeza mauzo ya nje ya sekta hiyo katika soko la Tanzania, likizingatiwa kuwa ni mojawapo ya masoko muhimu zaidi kwa bidhaa za chakula.
Balozi wa Misri nchini Tanzania, Bw. Mohamed Aboul Wafa, alizindua shughuli za msafara wa kibiashara na mikutano ya ana kwa ana (B2B) kati ya kampuni za Misri na zile za Tanzania, iliyoandaliwa na Baraza la Kuuza Nje la Sekta ya Chakula kwa kushirikiana na Mamlaka ya Biashara ya Kimataifa ya Misri.
Mnamo Novemba 2021, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alitembelea makao makuu ya Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Huru ya Misri kwa ajili ya kuzindua mkutano wa Jukwaa la Biashara la Misri na Tanzania. Jukwaa hilo lilihudhuriwa na idadi kubwa ya wafanyabiashara wa Misri, wakiwemo wale wenye uwekezaji nchini Tanzania pamoja na wale wanaopanga kuwekeza huko katika siku zijazo.
Mnamo Aprili 2022, Waziri wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Misri, Dk. Rania Al-Mashat, alikutana na Emmanuel Tutuba, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango ya Tanzania, kwa ajili ya kujadili jinsi ya kuimarisha uhusiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili pamoja na maendeleo ya hivi karibuni katika sekta ya uchumi wa kimataifa na juhudi za ushirikiano wa maendeleo.
Mnamo Juni 2022, Misri ilishiriki katika Maonesho ya 46 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam. Banda la Misri lilikuwa kubwa zaidi kati ya mabanda ya nchi zilizoshiriki, likihusisha mashirika na kampuni 25 kutoka Misri, yakiwemo Mamlaka ya Uzalishaji wa Kijeshi, Mamlaka ya Kiarabu ya Viwanda, na Mamlaka ya Maendeleo ya Miradi Midogo na ya Kati. Kampuni nyingine zilizoshiriki zilihusika katika sekta mbalimbali kama vile viwanda vya uhandisi, vifaa vya umeme, mavazi yaliyoshonwa tayari, ngozi, samani, vifaa vya nyumbani, bidhaa za ufundi na mengineyo.
Mfumo wa Mikataba kati ya Nchi Mbili:
Mnamo Novemba 2021, Misri na Tanzania zilitia saini hati kadhaa za makubaliano katika sekta za elimu ya juu, elimu ya msingi na sekondari, vijana na michezo.
Mnamo Februari 2022, hati ya makubaliano ilisainiwa kati ya Kampuni ya Kitaifa ya Rasilimali za Uvuvi na Kilimo cha Majini, mojawapo ya kampuni za Mamlaka ya Miradi ya Huduma za Kitaifa, na Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya Tanzania.
Makubaliano hayo yalitiwa saini na Meja Jenerali Walid Hussein Aboul Majd, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Miradi ya Huduma za Kitaifa, pamoja na Waziri wa Mifugo na Uvuvi wa Tanzania. Lengo lake lilikuwa ni kuimarisha ushirikiano wa pamoja katika sekta ya ufugaji wa samaki wa baharini na maji baridi.
Ushirikiano katika Sekta ya Maji na Uzalishaji wa Umeme wa Maji:
Mnamo Machi 2021, Waziri wa Rasilimali za Maji na Umwagiliaji wa Misri, Dkt. Mohamed Abdel Aty, alitangaza kuwa Misri inaendelea kusaidia Tanzania katika sekta ya maji. Alieleza kuwa uchimbaji na uwekaji wa visima 30 vya maji chini ya ardhi vinavyotumia nishati ya jua umekamilika, ili kuhakikisha upatikanaji wa maji safi ya kunywa katika maeneo ya vijijini yaliyo mbali na vyanzo vya maji. Visima hivi vimejengwa katika mikoa mitano: Same, Mwanga, Kiteto, Bariadi, na Busega, katika maeneo ya Kilimanjaro, Manyara, na Simiyu.
Aidha, aliongeza kuwa mafunzo kadhaa yametolewa kwa wataalamu wa Wizara ya Maji ya Tanzania ili kuongeza ujuzi katika usimamizi wa rasilimali za maji na umwagiliaji. Pia, makampuni ya Misri yanaendelea na ujenzi wa bwawa la Stiegler’s Gorge kwenye Mto Rufiji nchini Tanzania, mradi unaolenga kufanikisha matarajio ya wananchi wa Tanzania. Waziri pia alitoa salamu za pongezi kwa Rais mpya wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akimtakia mafanikio katika majukumu yake mapya.
Mnamo Mei 2021, Waziri wa Makazi, Huduma za Umma, na Maendeleo ya Miji wa Misri, Dkt. Assem El-Gazzar, aliongoza ujumbe wa Misri kwenda Tanzania ili kukagua maendeleo ya ujenzi wa bwawa la Julius Nyerere na kituo cha uzalishaji wa umeme wa maji. Alisisitiza kuwa kuna maagizo ya moja kwa moja kutoka kwa Rais wa Misri, Abdel Fattah El-Sisi, kuhakikisha ufuatiliaji wa mara kwa mara wa mradi huu kwa sababu ya umuhimu wake mkubwa kwa ndugu zao wa Tanzania. Kwa hivyo, ziara za ukaguzi zinafanyika mara kwa mara.
Mnamo tarehe Agosti 13, 2021, Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alikutana na Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Swedish Electric Egypt, Bw. Ahmed El-Sewedy. Kampuni yake ni sehemu ya muungano unaojenga kituo cha umeme wa maji cha Julius Nyerere.
Katika mkutano huo, El-Sewedy alimfahamisha Rais wa Tanzania kwamba kampuni yake imewekeza pia katika miradi mingine nchini humo na inatarajia kuongeza uwekezaji zaidi. Alieleza kuwa katika eneo la Kigamboni, Dar es Salaam, kampuni hiyo imejenga kiwanda cha kuzalisha nyaya za umeme, transfoma, vifaa vya kuzuia hitilafu za umeme, na mita za umeme. Kwa sababu ya mazingira mazuri ya uwekezaji nchini Tanzania, kampuni hiyo imeamua kuongeza juhudi zaidi kwa kujenga eneo la viwanda lenye ukubwa wa mita milioni mbili za mraba, ambalo litajumuisha pia kiwanda cha mbolea.
Zaidi ya hayo, El-Sewedy alieleza kuwa anataka kuwekeza katika ujenzi wa reli za kisasa na atahamasisha makampuni takriban 50 kutoka Misri kuwekeza Tanzania. Kwa upande wake, Rais Samia Suluhu Hassan alimshukuru Ahmed El-Sewedy na akaahidi kuwa serikali yake itashirikiana kuhakikisha utekelezaji wa miradi hiyo ya maendeleo kwa wakati unaofaa.
Mnamo Agosti 2021, Dkt. "Assem El-Gazzar," Waziri wa Makazi, Huduma za Umma, na Jamii za Mijini wa Misri, alitangaza kuanza kwa usakinishaji wa sehemu za kwanza za mitambo ya kuzalisha umeme katika Bwawa la Julius Nyerere. Muungano wa Kimasri unaojumuisha makampuni mawili, "El-Mokawloon El-Arab" na "Elsewedy Electric," ulianza kusakinisha sehemu za kwanza za mitambo ya kuzalisha umeme wa maji katika mradi wa Bwawa na Kituo cha Julius Nyerere nchini Tanzania.
Mnamo Julai 2022, Jeshi la Misri liliandaa ziara kwa ujumbe kutoka Tanzania kwenda Kituo cha Kusafisha Maji ya Bahari cha Galala, Kituo cha Kusafisha Maji cha Mahsameh, na Kituo cha Kusafisha Maji cha Hammam katika mradi wa Delta Mpya. Wanachama wa ujumbe huo walipokea maelezo ya kina kuhusu utaratibu wa uendeshaji wa vituo hivyo, hatua mbalimbali za kusafisha na kutibu maji kwa kutumia teknolojia za kisasa. Wanachama wa ujumbe huo walitoa shukrani zao za dhati kwa jeshi la Misri kwa kuandaa ziara hiyo, ambayo iliwapa fursa ya kufahamu mifumo ya kisasa ya uendeshaji na udhibiti wa vituo hivyo, vinavyochangia kuongeza manufaa ya rasilimali za maji zinazopatikana.
Mnamo Oktoba 2022, Balozi "Sherif Issa," Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri anayehusika na masuala ya Afrika, alitembelea Tanzania ili kuwasilisha barua kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, "Sameh Shoukry," kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, "Stergomena Tax," kuhusu kuimarisha na kuendeleza uhusiano wa pande mbili katika nyanja mbalimbali, pamoja na kufuatilia maendeleo ya mradi wa Bwawa la Julius Nyerere kwa ajili ya uzalishaji wa umeme wa maji.
Mnamo Novemba 2022, Dkt. "Assem El-Gazzar," Waziri wa Makazi, Huduma za Umma, na Jamii za Mijini wa Misri, alifanya mkutano wa mara kwa mara wa kufuatilia maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa Bwawa na Kituo cha Julius Nyerere, unaotekelezwa na muungano wa Kimasri wa makampuni ya "El-Mokawloon El-Arab" na "Elsewedy Electric," kwa kushirikiana na maafisa wa wizara na wawakilishi wa muungano huo.
Mnamo Desemba 2022, ujumbe wa Misri ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje, "Sameh Shoukry," na Dkt. "Assem El-Gazzar," Waziri wa Makazi, Huduma za Umma, na Jamii za Mijini, ulifanya ziara nchini Tanzania kuhudhuria sherehe za kuzindua ujazaji wa Ziwa la Bwawa la Julius Nyerere, mradi unaotekelezwa na muungano wa Kimasri wa makampuni ya "El-Mokawloon El-Arab" na "Elsewedy Electric" katika Mto Rufiji, Tanzania. Rais wa Tanzania, "Samia Suluhu Hassan," alihudhuria sherehe hizo kutokana na umuhimu mkubwa wa mradi huo kwa wananchi wa Tanzania.
Nyanja za Ushirikiano Kati ya Nchi Mbili:
Ushirikiano wa Elimu na Utamaduni:
Mnamo Oktoba 2022, Dkt. "Mohamed Mokhtar Gomaa," Waziri wa Waqfu wa Misri, alikutana na Dkt. "Abu Bakr Zubeir," Mufti wa Tanzania. Wakati wa mkutano huo, walisisitiza umuhimu wa kuendeleza ushirikiano wenye matunda kati ya Wizara ya Waqfu ya Misri na Ofisi ya Mufti wa Tanzania, hasa katika kusambaza fikra za wastani na kupambana na itikadi kali. Walijadili pia maeneo kadhaa ya ushirikiano wa pamoja, yakiwemo shughuli za Kituo cha Utamaduni cha Misri kinachohusiana na Wizara ya Waqfu nchini Tanzania, pamoja na mafunzo kwa maimamu na wahubiri wa Kitanzania katika Chuo cha Kimataifa cha Waqfu jijini Kairo.
Usafiri wa Anga:
Agosti 2022, Waziri wa Usafiri wa Anga wa Misri, Rubani "Mohamed Manar," alipokea ujumbe kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Tanzania. Pande hizo mbili zilijadili njia za kuimarisha ushirikiano katika sekta ya usafiri wa anga. Katika mazungumzo hayo, walifikia makubaliano ya awali ya kuteua kampuni ya ndege ya "Air Cairo" kufanya safari kati ya Misri na Tanzania, pamoja na "EgyptAir" iliyokuwa tayari imeteuliwa kama ndege ya kitaifa ya Misri.
Aidha, pande hizo mbili ziliteua kampuni mbili za ndege kutoka Tanzania. Ujumbe wa Tanzania pia uliomba kuimarisha safari za ndege kuelekea kisiwa cha Zanzibar na kuhamasisha ushirikiano wa kibiashara na kiufundi kati ya mashirika ya ndege ya Misri na Tanzania.
Usafiri wa Baharini:
Mnamo tarehe Januari 12, 2024, Luteni Jenerali "Richard Motaiba" alikutana na Luteni Jenerali "Reda Ahmed Ismail," Mkuu wa Sekta ya Usafiri wa Baharini wa Misri, ili kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati ya taasisi za usafiri wa baharini za Misri na Tanzania.
Ushirikiano huo ulijumuisha mashirika kama vile Chuo cha Bahari cha Dar es Salaam, SUMATRA, TASAC, Mamlaka ya Bandari Tanzania, na Mamlaka ya Bahari Zanzibar. Bw. Reda Ismail alieleza furaha yake kwa ziara hiyo na akasema kuwa ushirikiano mzuri kati ya taasisi za Tanzania na Misri utachangia kuimarisha uhusiano wa kibiashara, kuongeza biashara, na kufungua masoko mapya kwa kuwepo kwa huduma bora za usafiri wa anga na bahari kati ya nchi hizo mbili.
Ushirikiano katika Masuala ya Vijana na Michezo:
Mnamo Septemba 2022, Wizara ya Vijana na Michezo ya Misri, kwa mwongozo wa Waziri Dkt. "Ashraf Sobhy," ilishiriki katika Kongamano la Eneo Huru la Biashara la Afrika lililohusu wanawake na vijana, lililofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Kongamano hilo lilijadili jinsi ya kuwekeza kwa vijana na wanawake kama nguzo muhimu za ujenzi wa jamii za Afrika na maendeleo yao, pamoja na umuhimu wa Mkataba wa Biashara Huria wa Bara la Afrika. Kongamano hilo pia lilijikita katika kuondoa vikwazo vinavyowakabili wanawake na vijana katika biashara, kukuza usawa wa kijinsia, na kuboresha elimu ya kifedha ili kuongeza ukuaji wa uchumi kote barani Afrika.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Tanzania, Dkt. "Damas Ndumbaro," alifanya mazungumzo na Waziri wa Vijana na Michezo wa Misri, Dkt. "Ashraf Sobhy," jijini Kairo. Viongozi hao walikubaliana juu ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili, hasa katika kubadilishana uzoefu na kutoa mafunzo katika sekta ya michezo. Aidha, ujumbe wa Tanzania ulipata fursa ya kutembelea kituo cha michezo cha Klabu ya Al-Jazira, ambacho kina nyanja mbalimbali za kulea vipaji vya michezo kutoka kwa watoto wadogo hadi vijana, ambao ni hazina kubwa kwa wanamichezo wa taifa.
Sekta ya Afya:
Dkt. "Ali El-Ghamrawy," Mkuu wa Mamlaka ya Dawa ya Misri, alipokea ujumbe wa ngazi ya juu kutoka Tanzania, ukiongozwa na Luteni Jenerali "Richard Motaiba," Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Misri, pamoja na Bw. Adam Fimbo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba ya Tanzania (TMDA). Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Dkt. "Ayman El-Khatib," Naibu Mkuu wa Mamlaka ya Dawa ya Misri.
Mazungumzo yalilenga kuimarisha ushirikiano wa sekta ya dawa kati ya nchi hizo mbili, ikiwemo kujadili fursa za ushirikiano wa pamoja, kuanzisha programu za mafunzo na warsha za kitaalamu kwa ajili ya kubadilishana maarifa na uzoefu katika nyanja za mamlaka hizo mbili.
Aidha, mazungumzo yalihusu kurahisisha taratibu za kuingiza dawa za Misri katika soko la Tanzania. Kwa upande wake, Mkuu wa Mamlaka ya Dawa ya Misri alisifu mahusiano ya kina kati ya nchi hizo mbili na kusisitiza dhamira ya Misri ya kuongeza upatikanaji wa dawa za Kimasri nchini Tanzania ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa Tanzania.
Sekta ya Mifugo na Uvuvi:
Mnamo Februari 2024, Misri iliahidi kushirikiana na Tanzania katika kuimarisha sekta ya mifugo na uvuvi. Luteni Jenerali "Richard Makanzu," Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Misri, alifanya mazungumzo na Profesa "Saad Mousa," Mkuu wa Idara ya Mahusiano katika Wizara ya Kilimo ya Misri, pamoja na Mamlaka ya Udhibiti wa Mimea, kwa lengo la kuimarisha mahusiano na kuchunguza maeneo mapya ya ushirikiano kati ya Wizara ya Kilimo ya Tanzania na Wizara ya Kilimo ya Misri.
Profesa Saad alisisitiza umuhimu wa kufufua na kutekeleza kikamilifu makubaliano ya ushirikiano yaliyosainiwa mnamo mwaka 2018 katika sekta ya kilimo kupitia Kamati ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC). Pia alieleza hitaji la kufufua hati mbili za makubaliano katika sekta ya kilimo ili kupanua wigo wa ushirikiano katika sekta ya mifugo, vifaa vya kilimo, umwagiliaji, uvuvi, na mafunzo mbalimbali kwa ajili ya kutoa nafasi kwa maafisa wa kilimo kutoka Tanzania na Zanzibar. Luteni Jenerali Richard Makanzu alitoa shukrani zake kwa ushirikiano mzuri kati ya Tanzania na Misri katika sekta mbalimbali, ikiwemo kilimo, na akasisitiza haja ya kuendelea kuimarisha uhusiano huo kwa kuendeleza sekta ya uvuvi.
Sekta ya Barabara na Usafiri:
Timu ya Waziri wa Uchukuzi wa Misri, Meja Jenerali Mhandisi "Kamel El-Wazir," ilifanya ziara nchini Tanzania na kukutana na maafisa wa Mamlaka ya Biashara ya Tanzania (TAN TRADE). Waziri huyo alikutana na maafisa wa serikali, sekta binafsi, na viongozi wa Shirikisho la Viwanda la Tanzania ili kujadili njia za kuimarisha biashara kati ya nchi hizo mbili na kuongeza ushirikiano kati ya bandari za Misri na Tanzania.
Katika mkutano huo, Waziri wa Uchukuzi alisisitiza kuwa ziara hiyo inafanyika kwa mujibu wa maagizo ya uongozi wa kisiasa wa Misri ili kuongeza ushirikiano wa kiuchumi na kuimarisha biashara ya ndani ya bara la Afrika. Waziri alieleza kuwa Bandari ya Dar es Salaam ni moja ya bandari muhimu zaidi katika Ukanda wa Afrika Mashariki. Alipendekeza kuunganisha bandari hiyo na mojawapo ya bandari za Misri (Bandari ya Safaga) kwa kuanzisha njia ya meli ya moja kwa moja kutoka Misri hadi Bandari ya Dar es Salaam.
Pia, alijadili mpango wa kuanzisha eneo la vifaa (logistics hub) jijini Dar es Salaam, Tanzania, na Kigali, Rwanda, ili kukusanya bidhaa za Misri na kuzisafirisha kwa njia ya bahari hadi Tanzania, kisha kwa njia ya barabara kwenda Rwanda na nchi zingine zisizo na bandari katika Afrika ya Kati.
Aidha, Waziri wa Uchukuzi alisisitiza umuhimu wa ushirikiano katika maeneo ya viwanda vilivyopo Tanzania, ujenzi wa bandari kavu, na maendeleo ya Bandari ya Dar es Salaam na mtandao wa reli. Pande hizo mbili pia zilijadili njia bora za kuunganisha miradi hiyo kupitia mtandao wa barabara za ndani ya Tanzania, pamoja na barabara kuu inayounganisha Misri na Tanzania katika mfumo wa Barabara ya Cairo–Cape Town, ambayo inapitia nchi 10 za Afrika, ikiwemo Tanzania.
Sekta ya Kilimo:
Kamati ya Umwagiliaji imesaini hati ya makubaliano na Kampuni ya Arab Contractors ya Misri kwa ajili ya mradi wa umwagiliaji wa Bonde la Bugwema katika Ziwa Viktoria. Baada ya kusaini, Waziri wa Kilimo, Bw. Hussein Bashe, alieleza kuwa jumla ya mradi huo ni hekta 30,000, ambapo awamu ya kwanza itaanza na hekta 10,000. Waziri alibainisha kuwa mradi wa Bugwema ni moja ya miradi iliyotangazwa bungeni na imepangwa kutekelezwa katika mwaka wa fedha wa 2023/2024. Mradi huo utatekelezwa kwa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi.
Kwa upande wa mahusiano ya kibiashara na viwanda:
Katika juhudi za kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Arab Contractors, Mhandisi Hossam El-Din El-Reefi, Makamu wa Kwanza wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Arab Contractors, alikutana na Waziri wa Ujenzi wa Tanzania, Dkt. Innocent Bashungwa, kujadili njia za ushirikiano katika miradi ya maendeleo ya miji mbalimbali ya Tanzania. Wakati wa mkutano huo, Mhandisi Hossam El-Reefi alitoa salamu za Mhandisi Ahmed El-Assar, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, na kusisitiza dhamira ya kampuni kushiriki katika kuendeleza maendeleo ya Tanzania.
Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi wa Wizara ya Ujenzi ya Tanzania, akiwemo Bw. Mohamed Pista, Mwenyekiti wa Mamlaka ya Barabara na Madaraja ya Tanzania. Kwa upande wake, Waziri wa Tanzania aliisifu nguvu ya uhusiano kati ya Misri na Tanzania na akapongeza mchango wa Arab Contractors nchini Tanzania, hasa mafanikio katika mradi wa Bwawa la Julius Nyerere.
Balozi wa Tanzania nchini Misri alimpongeza kampuni ya El Sewedy Electric kwa utekelezaji mzuri wa ujenzi wa Bwawa la Julius Nyerere huko Rufiji. Mradi huo ni ishara muhimu ya ushirikiano kati ya Tanzania na Misri na unathibitisha kwamba changamoto za Afrika zinaweza kutatuliwa kwa juhudi za Waafrika wenyewe kutokana na uwezo, utaalamu, na dhamira yao ya kuendeleza bara la Afrika. Mhandisi Ahmed El Sewedy alimpongeza Balozi Richard Mutayoba kwa kuteuliwa kuwa mwakilishi wa Tanzania na nchi nyingine sita. Alimhakikishia balozi kuwa kampuni yake iko tayari kuzindua bwawa hilo wakati wowote kulingana na ratiba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Zaidi ya hayo, kampuni hiyo iko tayari kuwekeza katika miradi mikubwa nchini Tanzania na itashirikiana na ubalozi kusaidia utekelezaji wa majukumu yake nchini Misri.
Mnamo Februari 2024, Meja Jenerali Richard Mutayoba, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Misri, alitembelea Mamlaka ya Kiarabu ya Viwanda (AOI). Lengo la ziara hiyo lilikuwa kuimarisha uhusiano na AOI na kutathmini utendaji wake pamoja na vifaa vinavyotengenezwa na kampuni tanzu zake. Viongozi wa AOI wanatarajia kutembelea Tanzania kwa ajili ya kukutana na viongozi wa wizara mbalimbali, taasisi, na kampuni za Tanzania ili kujadili njia bora za ushirikiano wa kibiashara, kubadilishana bidhaa, na mambo mengineyo.
Kwa upande wa diplomasia:
Mnamo Januari 2024, Meja Jenerali Richard Mutayoba, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Misri, pamoja na maafisa wa ubalozi, walitembelea kampuni ya SERENDIB GROUP, inayomilikiwa na Bw. Hisham Halaldeen, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, ambayo makao yake makuu yako katika Jiji la 6 Oktoba. Kampuni hiyo ina viwanda vya kusindika bidhaa za kilimo kama chai na asali.
Zaidi ya hayo, kampuni inapanga kuanzisha mashamba makubwa kwa ajili ya kilimo cha chai na viungo mbalimbali, pamoja na kujenga viwanda vya kusindika bidhaa hizo ili kuongeza thamani yake na kuunda fursa za ajira kwa vijana wa Tanzania. Pia, kampuni inatarajia kununua korosho, karafuu, tangawizi, na mwani kutoka Tanzania kwa ajili ya kusafirisha kupitia viwanda vitakavyoanzishwa.
Meja Jenerali Richard Mutayoba pia alitembelea kampuni ya Rich Home ya Misri, inayozalisha bidhaa mbalimbali kama magodoro, mito, mashuka, na mazulia yenye ubora wa kimataifa katika Jiji la Obour. Kiwanda hicho kinatumia bidhaa za plastiki kuzigeuza kuwa nyuzi zinazotumika kutengeneza bidhaa hizo huku kikihifadhi mazingira kupitia "urejelezaji" wa taka za plastiki. Balozi aliwahimiza wafanyabiashara kuwekeza nchini Tanzania kwani ni sehemu bora kwa uwekezaji kutokana na mazingira mazuri ya biashara, maeneo bora ya uwekezaji, rasilimali nyingi kama bahari, mito, maziwa, ardhi yenye rutuba, hifadhi za asili, madini, fukwe nzuri, na vivutio vya utalii.
Pia, aliwaalika wafanyabiashara kushiriki katika maonesho ya "Saba Saba" kwa ajili ya kuonesha bidhaa zao kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya ubora. Aidha, alihakikishia wafanyabiashara kuwa watapewa msaada wote wanaohitaji ili kufanikisha lengo lao la kuingia kwenye soko la Tanzania.
Mnamo Desemba 2023, Balozi Richard Mutayoba, akiwa ameandamana na maafisa wa ubalozi, alitembelea kampuni ya Delta Tube, inayojihusisha na utengenezaji wa vifaa na zana za umeme kwa kutumia alumini. Kampuni hiyo, ambayo makao yake makuu yako Kairo, ilianzishwa mwaka 2015. Mmiliki wa kampuni alieleza nia ya kuwekeza nchini Tanzania na kufungua tawi la kampuni yake iwapo itahitajika.
Balozi alimpa mwongozo sahihi na jinsi ya kuwasiliana na mamlaka husika ili kufanikisha lengo hilo. Pia, alimhakikishia mmiliki wa kampuni kuwa Tanzania ni nchi yenye mvuto mkubwa wa uwekezaji kutokana na ukuaji wake wa kiuchumi na mazingira rafiki ya uwekezaji.
Mfuko wa Misri wa Ushirikiano wa Kiufundi na Afrika:
Kuna ushirikiano mkubwa kati ya Misri na Tanzania katika sekta mbalimbali za maendeleo kama mafunzo, afya, na misaada ya kibinadamu. Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizo na makubaliano ya ushirikiano na Mfuko wa Misri wa Ushirikiano wa Kiufundi na Afrika, pamoja na Wakala wa Misri wa Ushirikiano kwa Maendeleo.
Tanzania inanufaika na wataalamu wa Kimasri na msaada wa kiufundi kutoka Misri, hasa katika sekta za madini, metallojia, kilimo, teknolojia, vyombo vya habari, diplomasia, umeme, na maendeleo ya rasilimali watu kwa ajili ya viwanda na sekta nyinginezo.
Msaada kwa ndugu wa Tanzania:
Mnamo Januari 2022, ndege mbili za kijeshi zilisafirisha tani kadhaa za msaada wa matibabu kutoka Wizara ya Afya na Idadi ya Watu ya Misri kwenda kwa ndugu wa Tanzania, ili kusaidia kupunguza mzigo kwa wananchi wa Tanzania. Msaada huo ni sehemu ya juhudi za Misri katika kuchangia maendeleo ya bara la Afrika.
Mnamo Septemba 2022, Balozi Mohamed Jaber Abu El-Wafa, Balozi wa Misri nchini Tanzania, alikabidhi msaada wa vifaa vya matibabu kutoka Misri katika hafla rasmi iliyohudhuriwa na Dawood Masasi, Mkuu wa Kitengo cha Dawa katika Wizara ya Afya ya Tanzania, Mafier Tokai, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Hifadhi ya Dawa, pamoja na maafisa wengine wa Wizara ya Afya ya Tanzania.