Taasisi ya Upangaji ya kitaifa 

Taasisi ya Upangaji ya kitaifa 

Taasisi ya Upangaji ya kitaifa  ilianzishwa kutokana na Sheria Na. 231 ya 1960 kama taasisi ya umma yenye taswira muhimu ya binafsi ili kuboresha mbinu na mawazo ya mipango ya kisayansi nchini Misri kupitia  shughuli za utafiti, mafunzo,   za elimu, kukuza jukumu na kazi za Wizara ya Upangaji, kusambaza mawazo na kazi ya kupanga katika taasisi zote za kitaifa, na kueneza ufahamu wa kupanga katika jamii ya kimisri .

 Na kama dalili ya jukumu la Taasisi katika kuunga mkono maendeleo ya kina nchini Misri tangu kuanzishwa kwake, basi Taasisi hiyo imeongezwa kwa uwezo unaohitajika wa kibinadamu na kimaumbile na imepeleka dhamini za masomo kadha  kwa sehemu zote ulimwenguni  ili kupata shahada za elimu katika  nyanja  mbalimbali. vilevile , tasisi ililetea wataalam wakuu ulimwenguni  wenye utaalamu wa uwanja wa maendeleo na upangaji ili   kuwasilisha  uzoefu na maarifa kwa Taasisi, licha ya  nyanja za ushirikiano   na  mashirika ya kimataifa ya Umoja wa Mataifa ziliongezeka , pia  taasisi   kadha za kisayansi huko Ulaya, Afrika na Mashariki ya Kati.  vilevile , Taasisi hiyo  ilipewa uwezo wa kiteknolojia unaoendana na vigezo vya kisasa , ambapo  taasisi hiyo ndiyo iliyokuwa na heshima na ilitangulia  kumiliki kompyuta ya kwanza nchini Misri mwaka 1960.

na kupitia michango yake yote ya zaidi ya miongo mitano, Taasisi  hiyo ilitoa nyongezo na michango muhimu katika nyanja za kazi yake na  jukumu lake kuu .  ambapo  ilishirikiana na Wizara ya Upangaji katika kuandaa mipango na mikakati ya maendeleo mbalimbali , na katika kuainisha , kuchagua na kusoma  miradi mikubwa, pamoja na kuunga mkono juhudi za mpangaji katika kushughulikiana na  vipengele  muhimu vya maendeleo kama: maendeleo ya kikanda, utafiti wa makazi duni,  masuala ya  mazingira na uendelevu , mipango ya jinsia , ushirikiano wa kibiashara na urambazaji kati ya nchi za Mto  wa Nile, ushirikiano wa kiuchumi wa kikanda na kimataifa, kuendeleza nafasi  za kitaifa na mengineyo, vilevile , Taasisi inashirikiana na Wizara ya Upangaji katika kutekeleza miradi muhimu ya utafiti. 

Katika uwanja wa  Tafiti, machapisho ya utafiti ya Taasisi yalikuwa mengi na tofauti, ikiwa ni pamoja na mfululizo wa masuala ya mipango na maendeleo, maelezo ya nje,  vipeperushi vya  sera na hivi karibuni karatasi za  sera.Machapisho hayo yalishughulikia masuala yote muhimu ya maendeleo ya kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na maarifa wakati wa  tangu zaidi ya miongo mitano, na Taasisi ilishirikiana na timu za utafiti zinazoshirikiana na wale   waliofaidika  kutoka shughuli za tafiti  zake na  wenye maslahi  kutoka nchi ambapo wengi wao wanajulikana  kwa  ujuzi wa nyanja  na mwelekeo wa kiutendaji.

 Taasisi ilipata heshima  na ilitangulia kuchapisha ripoti ya kwanza ya kitaifa kuhusu maendeleo ya binadamu katika ulimwengu wa Kiarabu   mnamo mwaka 1993 na ripoti zifuatazo kila mwaka. Pia ilichapisha  baadaye ripoti za kimaendeleo ya binadamu katika  upande wa mikoa .Taasisi hiyo inazindua jarida maalumu la kisayansi nalo ni: Gazeti la Maendeleo na Upangaji la Misri.

Shughuli za machapisho ya utafiti na Gazeti la kisayansi zimeongezwa kwa harakati za kisayansi, kitafiti na kiutamaduni muhimu sawasawa kama : Semina ya Jumanne, Mkutano wa Wataalamu, Ufuatiliaji wa kitaaluma,Semina ya Watafiti Vijana,Semina za kisayansi, Mkutano wa mawazo wa kila mwaka, na nyinginezo zilizokutana pamoja ili kuwa na  Sifa maalum za kitafiti kwa Taasisi kuu hiyo.

Katika uwanja wa mafunzo na ushauri, mafanikio ya Taasisi yasiyo na kifani , ambapo  michango ya mafunzo ya Taasisi ilikuwa tofauti, na pande zake  za kimkakati na zisizo za kijadi   zilikuwa anuwai kwa lengo la   kukuza  maendeleo, vilevile, kujumuisha kategoria na sekta mbalimbali, kwa ushirikiano wa  ndani , Kiarabu na  wa kimataifa.

Miongoni mwa shughuli maarufu zaidi za Taasisi katika uwanja huo ni kutekeleza makumi ya programu za mafunzo  mnamo kila mwaka katika mikoa ya Misri, Wizara na Taasisi za  serikali, pamoja na mafunzo mbalimbali katika uwanja wa kompyuta. Diploma ya Taasisi pia ilichangia tangu  miongo mingi katika kuunda uwezo wa maelfu ya vijana na viongozi wa Misri na nchi za Kiarabu na Afrika katika uwanja wa mipango na maendeleo. kuhusu upande wa masomo ya juu , tasisi ilishuhudia mabadiliko  ya ubora hivi karibuni , kuanzia awamu ya Uzamili wa tasisi ya Upangaji na Maendeleo ambayo ikiidhinishwa na Baraza kuu la Vyuo Vikuu   2008  /2009, na kujiandaa ili kuanzisha utekelezaji wa  programu ya Uzamili  kwa ushirikiano na Taasisi ya Afrika ya Maendeleo ya Kiuchumi na Upangaji.

Tumegundua kuwa Taasisi tangu kipindi kizima cha kazi yake yenye shughuli nyingi, imekusanyika uzoefu na maarifa ambayo inaonesha  faida za ushindani kwa muda wa kazi yake ndefu, kama vile: utaalamu wa  utafiti wa utendaji, uundaji wa mfano, takwimu na akaunti za kitaifa, uzoefu wa kuunda data , taarifa na maarifa katika nyanja mbalimbali za upangaji na maendeleo, na uzoefu wa kuendeleza uwezo wa kusajili hati, akaunti ya  kisayansi na maktaba za kina. Utandawazi , uwasiliano na ushirikiano  wa tasisi pamoja na mashirika mengi muhimu ya ndani, kikanda na kimataifa ulichangia katika  kuthibitisha  uzoefu huo, na kuanzisha  Taasisi ya Maendeleo ya Korea KDI, Taasisi ya Afrika ya Maendeleo ya Uchumi na Mipango IDEP, Benki ya Maendeleo ya Afrika, Taasisi ya Kiarabu ya Upangaji , Taasisi ya Tunisia ya Mafunzo ya Ushindani na masomo   ya Kiasi na nyinginezo, pamoja na mapokezi ya Taasisi hiyo kwa wataalam wengi wa kimataifa katika nyanja mbalimbali za maendeleo, na kuandaa makongamano mengi, semina, na majukwaa ya  kisayansi na kifiria .

Kwa lengo la kuendeleza majukumu ya Taasisi, Sheria Na.31 , mwaka  2015 ilitolewa hivi karibuni kuhusu Taasisi ya Upangaji ya Kitaifa  ili kuimarisha na kuthibitisha jukumu lake kama mamlaka ya umma yenye uhusika huru wa unaofanya shughuli ya kisayansi, na kama kituo kikuu cha  kwa kufikiri juu ya masuala ya upangaji na maendeleo, na kuthibitisha jukumu lake katika kuendeleza tafiti na  masomo yanayohusiana na  uandaaji  wa mipango ya maendeleo ya serikali na njia za kuitekeleza, na kusoma misingi ya  na mbinu za  kisayansi za kupanga na kuendeleza kwa lengo la ya kuwapatia wale wanaosimamia mchakato wa upangaji katika ngazi zote, watoa maamuzi na watunga sera  kwa maoni  na njia mbadala za kimkakati , na kueneza uelewano na ufahamu kwa masuala ya mipango   na maendeleo ya kina na   endelevu katika jamii. vilevile , sheria mpya  ya Taasisi inakiri haki ya taasisi ama pekee yake  au pamoja na wengine kwa kupatia   shahada za kitaaluma: Diploma , Uzamili na Uzamivu katika nyanja za Upangaji na Maendeleo.