Septemba 9, ni Kumbukumbu ya uzinduzi wa kuanzishwa kwa Umoja wa Afrika

Septemba 9, ni Kumbukumbu ya uzinduzi wa kuanzishwa kwa Umoja wa Afrika

Umoja wa Afrika ulianzishwa Septemba 9, 1999, ambapo Azimio la Sirte lilipohangaika kuanzishwa kwa Umoja mpya wa Afrika, na hivyo wakati wa kikao cha nne cha pekee cha Mkutano wa Umoja wa Nchi huru za Afrika kwa Wakuu wa Nchi na Serikali za Afrika zinazokutana katika mji wa Sirte nchini Libya.

Na hapo awali, katika muktadha huu, Mikutano minne ya kilele ilifanyika katika maandalizi ya uzinduzi rasmi wa Umoja wa Afrika mjini Durban, huko Afrika Kusini mwaka 2002, nao ni Mkutano wa Sirte wa 1999, uliopitisha Azimio la Sirte na wito wa kuanzishwa kwa Umoja wa Afrika,kisha, Mkutano wa 2000 wa Lomé ulizinduliwa, ambapo Sheria ya Katiba ya Umoja wa Afrika ilipitishwa, na Mkutano wa tatu ulikuwa wa kilele wa Lusaka kwa mwaka wa 2001, ambapo Mwenendo wa utekelezaji wa Umoja wa Afrika uliundwa.

Kwa hiyo, nembo ya Umoja wa Afrika ilizinduliwa, ambayo ina vipengele vinne, nayo ni matawi ya mitende kwenye pande zote za duara kama ishara ya amani, na duara wa dhahabu, ishara ya utajiri wa Afrika na mustakabali yake mzuri, ama Ramani ya Afrika bila mipaka katika mduara wa ndani, inamaanisha Umoja wa Kiafrika, na pete ndogo nyekundu zilizounganishwa kwenye msingi wa nembo ni ishara ya mshikamano wa Waafrika na damu iliyomwagika kwa ajili ya ukombozi.

Ama kwa upande wa bendera ya Umoja, ilipitishwa mnamo Juni 2010, wakati wa kikao cha kawaida cha kumi na mbili cha Baraza la Wakuu wa Nchi na Serikali, na Muundo huo unaelezewa kama ramani ya bara la Afrika katika kijani kibichi juu ya jua nyeupe, imezungukwa na mduara wa nyota 53 za dhahabu zenye alama tano kwenye usuli wa uwanja wa kijani kibichi, na asili ya kijani kibichi inaashiria matumaini, na nyota zinawakilisha nchi wanachama wa Umoja wa Afrika, na kisha Jamhuri ya Sudan Kusini ilijiunga na Umoja wa Afrika mnamo 2011 na kuwa nyota 54, na mnamo 2017, na Ufalme wa Morocco umerudisha uanachama wake katika Umoja huo, hivyo kuwa mwakilishi wa nyota 55 wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika.

Umoja wa Afrika umegawanyika katika kanda 5: 

Afrika Kaskazini, Afrika Mashariki, Afrika Magharibi, Afrika ya Kati na Afrika Kusini.

Lugha za kazi ndani ya Umoja wa Afrika ni Kiarabu, Kiingereza, Kifaransa na Kireno kwa mujibu wa Kifungu cha 11 cha Itifaki ya Sheria ya Katiba ya Umoja wa Afrika, na kwa kuongeza, inasema kuwa lugha rasmi za Umoja wa Afrika na Taasisi zake zote ni Kiarabu, Kiingereza, Kifaransa, Kireno, Kihispania, Kiswahili na lugha nyingine yoyote ya kiafrika.

Na kwa kutimiza jukumu la Umoja wa Nchi Huru za Afrika, Umoja huo umefanya kazi ili kufikia Mshikamano wa Afrika, na kusaidia na kuziwezesha nchi za Afrika katika uchumi wa dunia na kushughulikia matatizo mengi ya kijamii, kiuchumi na kisiasa yanayolikabili bara hili; tufikie Afrika iliyoungana, iliyounganishwa, yenye mafanikio na  yenye nguvu ya kimataifa katika nyanja ya kimataifa, kwa hiyo, Agenda ya Afrika 2063 ilizinduliwa wakati wa maadhimisho ya jubilee ya dhahabu ya Umoja wa Nchi huru za Afrika mwaka 2013, ambapo Ajenda hiyo ilianza kutumika mnamo 2015, Kauli mbiu ya Umoja wa Afrika kwa mwaka wa 2021 ni  "Sanaa, Utamaduni na Urithi: Chombo cha Kujenga Afrika Tunayoitaka"

Ikumbukwe kuwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika ulianzishwa tarehe 25 Mei, 1963, Addis Ababa, huko Ethiopia, Malengo yake muhimu zaidi  yalikuwa ni kuimarisha Umoja na mshikamano wa watu wa Afrika na kuzidisha juhudi za kutokomeza ubaguzi wa rangi na ukoloni katika sehemu zote za bara, na kuhifadhi udhibiti wa nchi wanachama na usalama zake wa kikanda, na kuimarisha ushirikiano wa kimataifa ndani ya mfumo wa Umoja wa Mataifa, Pamoja na kupitishwa kwa sera za wanachama kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni, kidiplomasia, kiufundi na kiulinzi.