Kumbukumbu ya kuuawa kwa Patrice Lumumba
Imefasiriwa na / Abdullah Nasser Farhat
Na / Kerebso Diallo
Mnamo 1957 mwandishi wa habari wa Ubelgiji aliuliza Patrice Lumumba: Vipi mnataka uhuru wakati hamna hata daktari au mwanasheria mmoja? Akamjibu: Na nyinyi wakoloni mlitawala nchi yetu kwa miongo mingi mkashindwa kufundisha daktari au mwanasheria hata mmoja, mnategemea tukubali zaidi udhalilishaji huu?
Leo ni kumbukumbu ya kuuawa kwa Patrice Lumumba ambaye hakutosheka akiuawa tu na nchi za Magharibi na washirika wake wa ndani, bali waliukata mwili wake na kuupasua kwa asidi ya sulfuriki, wakihofia kuzikwa kwake kuwa kaburi, na kila mtu ajue ni nani Patrice Lumumba ndiye, ambaye Malcolm X alimwita lakabu ya ( Mwafrika mkuu zaidi anayehai).
Na hadithi ya mapambano yake dhidi ya kutoa uhuru wa kidhania kwa wasomi wapya, weusi ambao wanalinda maslahi ya ubepari wa ndani na ukoloni mamboleo unaowakilishwa na tawala za Magharibi na mashirika ya kimataifa.
Hifadhi picha za maandamano makubwa yaliyofanyika katika mitaa ya Kairo kupinga mauaji ya "Patrice Lumumba" na kulaani uzembe la Umoja wa Mataifa na ushirikiano wake na Ubelgiji, Marekani na Moise Chompy.
Kwa maelezo zaidi kuhusu Kiongozi wa Congo ya Kidemokrasia " Patrice Lumumba" , bonyeza hapa...