Vijana wa Udhamini wa Nasser wako kwenye matembezi ya kiutalii huko eneo la  Piramidi za Giza na Saqara

Vijana wa Udhamini wa Nasser wako kwenye matembezi ya kiutalii huko eneo la  Piramidi za Giza na Saqara
Vijana wa Udhamini wa Nasser wako kwenye matembezi ya kiutalii huko eneo la  Piramidi za Giza na Saqara
Vijana wa Udhamini wa Nasser wako kwenye matembezi ya kiutalii huko eneo la  Piramidi za Giza na Saqara

Shughuli za siku ya 4 ya Udhamini wa "Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa " zilianza  kwa kupanga matembezi ya kiutalii  katika eneo la  piramidi za Giza na Saqara, kwa wajumbe Vijana walioshiriki katika Udhamini huo , ambapo walitazama  Piramidi ili wajue zaidi kuhusu Ustaarabu wa kifarao wa kale.

 Vilevile ,  Mkurugenzi Mkuu wa eneo la  mabaki ya kale ya   ya Saqara , Dkt. Sabri Farag  alikuwa wa kwanza wa kuwapokea washiriki wa Udhamini huo, akiambatana nao matembezi yao ya ziara ya kutazama maeneo ya kale katika eneo hilo na Piramidi tatu.

Washiriki wa Udhamini  walisikiliza maelezo ya kina kuhusu historia ya mahali palipovutia Dunia nzima, Piramidi na jinsi zilivyojengwa, na kuhusu kipindi kile cha  historia ya kifarao ya Misri , pia washiriki  walifikia eneo la Panorama ambapo walipiga picha kadhaa za kumbukumbu na walinunua  vipande vya kale  pamoja na zawadi za kumbukumbu.