Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela.. Kumbukumbu ya Wenye athari Duniani

Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela.. Kumbukumbu ya Wenye athari Duniani

" Kuwa na uhuru haimaanishi kuachana na minyororo, bali kuishi katika mazingira yanayoimarisha uhuru wa watu na kuuheshimu" Nelson Mandela.

Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela yaambatana na kumbukumbu ya kuzaliwa kwake, tena kama kutambua kutoka kwa Umoja wa Mataifa kwa mchango wake katika uimarishaji wa dhana ya haki na uhuru, na kuthamini maadili na kujitolea kwa Nelson Mandela katika kuhudumia Utu, katika maeneo yenye migogoro, upatanisho na kukuza usawa wa kijinsia na haki za watoto na makundi mengine yaliyo hatarini, pamoja na  mapambano yake ya demokrasia katika ngazi ya kimataifa na katika kukuza utamaduni wa amani sehemu mbalimbali za Dunia.

Miaka 67 ya mapambano ambayo Nelson Mandela aliyaishi, Rais wa zamani sana wa jamhuri ya Afrika Kusini, Mtetezi wa haki za binadamu, Mfungwa kwa ajili ya kusema ukweli, akihakikisha Amani, Kusimamia dhidi ya dhuluma, akihudumia Utu.

Kwa hivyo, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa liliamua kuteua  Julai 18 kila mwaka, iwe Siku ya Kimataifa kwa Nelson Mandla, kulingana na azimio lake (A/RES/64/13), ili kukuza  uwajibikaji wa kijamii wa watu binafsi kwa jamii zao, na uwezo wao wa kufanya mabadiliko Kuelekea bora zaidi, kwa kuzingatia Siku ya Mandela kuwa msukumo kwa kila mtu kufanya kazi, kubadilisha, na fursa ya kutafakari juu ya historia ya mpiganiaji wa kimataifa anayetetea heshima, na kuunga mkono maadili ya mshikamano wa binadamu na Umoja wa Utu. 

 Hatimaye, "Tunaweza kubadilisha ulimwengu na kuifanya kuwa mahali pazuri zaidi" Kiongozi wa kihistoria Nelson Mandela (1918-2013).