Siku ya Vitabu Duniani na Haki za mwandishi

Siku ya Vitabu Duniani na Haki za mwandishi

Kupitia kusoma haswa katika Siku hii ya Vitabu Duniani na haki za mwandishi, sambamba na Aprili 23, tunaweza Kunyoosha madaraja kati yetu na wengine licha ya umbali, na kuwaza kwa undani, tusafiri nayo popote tunapotaka.

 Basi kwa hivyo, UNESCO imepitisha Siku ya Vitabu na Hakimiliki Ulimwenguni, ikifanyika kila mwaka mnamo Aprili 23 tangu 1995, ili kusherehekea kitabu na waandishi Duniani kote.

 Tarehe Aprili 23 imechaguliwa ikizingatiwa kama historia bora katika uwanja wa fasihi ya ulimwengu, Inaadhimisha kumbukumbu ya kifo cha waandishi kadhaa mashuhuri kama William Shakespeare, Miguel de Cervantes na Inca Garcilaso de La Vega.

Madhumuni ya Siku ya Vitabu Duniani ni kuonyesha hali ya waandishi, na umuhimu wa vitabu Duniani kote, kwa kuwahimiza watu kwa ujumla, na haswa vijana, Ili kugundua furaha ya kusoma na kuheshimu michango ya kipekee iliyotolewa na waandishi waliosukuma mbele maendeleo ya kijamii na kiutamaduni ya wanadamu.

Leo tuna haja kubwa zaidi ya kusoma.