Kampuni ya Nile kwa usafiri wa nchi kavu

Kampuni ya Nile kwa usafiri wa nchi kavu

Hakika usafiri  una umuhimu mkubwa sana katika biashara ya ndani na ya nje na usafiri wa nchi kavu una nafasi kubwa kulingana na umuhimu wake kama Sehemu ya Uchumi wa kitaifa na nguzo muhimu katika mkakati wa Maendeleo; ambapo usafiri huo wa nchi kavu ni miongoni mwa njia za usafiri nzuri zaidi kwa upande wa bei yake nafuu na uzalishaji kwa mahali popote ndani na nje ya nchi. Pia kwa  kukuza na kuiboresha usafiri wa nchi kavu unaopatikana kwenye uchumi wa kitaifa na kimataifa, basi kuishughulisha zaidi ni miongoni mwa malengo ya kitaifa ya nchi na suala la kupatia Uhuru wa kiuchumi. Kwa hivyo azimio la Rais Gamal Abdel Nasser, mnamo 1963 limetolewa kwa kuanzisha Kampuni ya Nile kwa usafiri wa nchi kavu.

Kampuni hiyo ya Nile inachukuliwa kama moja ya makampuni makubwa ya uanzilishi katika uwanja wa kusafirisha bidhaa  ndani na ya nje ya Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, pia inayochangia kikubwa  katika kuzisafirisha bidhaa muhimu sana, nazo ni kama ngano na majiko na vitu vingine vinavyohudumia Uchumi wa  kitaifa, Mauzo ya ndani na ya nje kutoka kwa bandari zote ndani ya Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, licha ya Ushirikiano wa nje  kama Muungano wa Kiarabu kwa usafiri wa nchi kavu.

Makao makuu ya Kampuni hiyo yako mjini  Alexandria,ikiwa na  matawi kadhaa mengine katika miji mbalimbali kama vile : Kairo, Suez, Kafr El Zayat na El-Mahala.