"Chuo Kikuu cha Gamal Abdel Nasser huko Conakry "
Chuo Kikuu cha Gamal Abdel Nasser kiko katika eneo la "Dixen" katika mji mkuu wa Guinea Conakry, pia kilianzishwa mnamo 1962, kwa jina la " Institute Polytechnique de Conakry" kama taasisi ya kwanza ya kisayansi ya kutoa elimu ya juu huko Guinea, na shughuli huko ilikuwa ikienda mara kwa mara, na kwa uratibu, kwa ushirikiano pamoja na Umoja wa Kisovieti wa zamani.
Chuo kikuu hicho kimepata umaarufu mkubwa tangu kilipoanzishwa kutokana na uhusiano wake tangu siku zake za mwanzo na kipindi cha maendeleo ya kiuchumi kilichofuatia kupata uhuru wa nchi. mnamo Mwaka 1965, Kitivo cha Uongozi wa Juu kiliunganishwa na Chuo Kikuu katika taasisi moja. na mnamo 1974, Chuo Kikuu kikawa na vitivo na vyuo13 ikiwa ni pamoja na ; Kitivo cha Tiba, lakini sasa kinajumuisha idadi kubwa ya vitivo pamoja na kitivo cha Tiba, vitivo vya Famasia, Meno na Sayansi, kituo cha masomo ya mazingira, kituo cha kompyuta, na Sehemu za uhandisi wa umeme, uhandisi wa kompyuta, uhandisi wa kemikali, uhandisi wa viwanda, na mawasiliano yasiyo na waya.
Mnamo 1989, Chuo Kikuu kilipewa jina jipya la "Chuo Kikuu cha Gamal Abdel Nasser huko Conakry." na kinajipambanua kwa kufanya kazi kupitia mtandao wa kompyuta wa fiber-optic, ambao ulitekelezwa kwa misaada ya Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani, jambo ambalo lilisaidia kila kitivo kutoa maabara ya kompyuta kati ya tano hadi tisa kwa wanafunzi wake. Na kuanzia 2007, elimu ya chuo kikuu mtandaoni ikawa ikipatikana katika Chuo Kikuu.