Chini ya Kauli Mbiu «Kukomesha Ubaguzi wa Rangi na Kujenga Amani» Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Amani Yatafanyika Mwaka Huu

Chini ya Kauli Mbiu «Kukomesha Ubaguzi wa Rangi na Kujenga Amani» Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Amani Yatafanyika Mwaka Huu

Imetafasiriwa na/ Hasnaa Hosny
Imeharirwa na/ Mervat Sakr

Ushindi wa kweli na wa kudumu ni Ushindi wa amani, sio Ushindi wa vita.

Utamaduni wa amani ni Utamaduni wa mazungumzo na kuzuia, na Ajenda ya 2030 ya Maendeleo Endelevu ilithibitisha kuwa "hakuna njia ya kufikia maendeleo endelevu bila amani, wala kuanzisha amani bila maendeleo endelevu", kama ilivyoitwa na dini za mbinguni, zilizotajwa katika Biblia (Utukufu kwa Mungu juu, duniani ni amani, na katika watu wenye furaha). Luka 2:14, na inasema katika Qur'an Tukufu, "Wasamehe na useme amani" 89 Al-Zukhruf.

Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilitangaza Siku ya Kimataifa ya Amani mwaka 1981 kwa lengo la kusherehekea na kukuza maadili ya amani miongoni mwa mataifa na watu wote, na miaka ishirini baadaye, kwa azimio namba 55/8282, Baraza Kuu liliiteua Septemba 21 kama siku ya kila mwaka ya kusherehekea tukio hilo, likisisitiza Usitishaji mapigano duniani na kutotumia nguvu kupitia elimu, Uelewa wa Umma na Ushirikiano ili kufikia Usitishaji mapigano duniani kote.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema: "Ubaguzi wa rangi unaendelea kueneza sumu yake katika taasisi, miundo ya kijamii na maisha ya kila siku katika kila jamii. Wanaendelea kuwa sababu muhimu katika kuendelea kwa Ukosefu wa Usawa... Wanaendelea kuwanyima haki zao za msingi za binadamu... Wanadhoofisha jamii, kudhoofisha demokrasia, kudhoofisha uhalali wa serikali, nk. Uhusiano kati ya Ubaguzi wa rangi na Usawa wa kijinsia hauna Utata."

Wakati migogoro ikiendelea kuchipuka duniani kote ambayo husababisha watu kukimbia hatari, tumeona Ubaguzi unaozingatia rangi katika mipaka. Wakati virusi vya Korona vikiendelea kushambulia jamii zetu, tumeona jinsi makundi fulani ya kikabila yalivyoathirika zaidi kuliko wengine. Kama uchumi unavyoteseka, tumeona hotuba za chuki na vurugu zinazoelekezwa dhidi ya wachache wa kikabila.

Hakuna shaka kwamba sisi sote tuna jukumu la kufanya katika kukuza amani. Kukabiliana na Ubaguzi wa rangi ni njia muhimu ya kuchangia.

Tunaweza kufanya kazi ili kuvunja miundo inayoendeleza Ubaguzi wa rangi kati yetu. Tunaweza kusaidia Usawa na harakati za haki za binadamu kila mahali. Tunaweza kuzungumza dhidi ya hotuba za chuki - katika maisha yetu halisi na mkondoni.Tunaweza kukuza kupinga Ubaguzi wa rangi kupitia elimu na haki ya kurekebisha.


Mratibu wa lugha ya kiswahili/ Tasneem Hamdy