Ubalozi wa Pakistani mjini Kairo wakaribisha wahitimu wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa
Balozi wa Jamhuri ya Pakistani kwenye Jamhuri ya kiarabu ya Misri,Balozi Sajid Bilal alipokea: Asim Babbar, Zurmina Nayyar, Vibha Framin, Washiriki wa Shughuli za toleo la tatu la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa, ulioshikilia Ufadhili wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri, Rais Abdel Fattah El-Sisi, Kwa ushiriki wa viongozi vijana 150 kutoka nchi za kutofungamana kwa upande wowote na nchi rafiki, mnamo kipindi cha kuanzia Mei 31 hadi Juni 17, 2022 katika Jumba la Mamlaka ya Uhandisi mjini Kairo.
Mkutano huo ulishughulikia kutambulisha Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa katika toleo lake la tatu, na kujadili jinsi ya kuwezesha na kuanzisha ushirikiano wa nchi mbili kati ya Jamhuri ya Kiarabu ya Misri na Jamhuri ya Pakistani katika uwanja wa vijana, na kujadili shughuli na programu zinazoweza kutekelezwa mnamo kipindi kijacho.
Na akiwahutubia viongozi vijana wa Pakistani, Balozi Majid Bilal alidokeza kuwa mabadilishano hayo muhimu yanaongeza fursa za mawasiliano na kuimarisha mahusiano kati ya watu wa nchi hizo mbili, na pia alipongeza nafasi ya viongozi vijana katika kuanzisha mahusiano ya karibu kati ya Pakistan na Misri kupitia programu hizo.
Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa unalenga kuhamisha uzoefu mkale wa Misri katika uimarishaji na ujenzi wa taasisi za kitaifa, pamoja na kuunda kizazi cha viongozi vijana kutoka nchi za kutofungamana kwa upande wowote wenye maoni yanayoendana na Ushirikiano wa Kusini-Kusini, na ufahamu wa jukumu la Harakati ya kutofungamana kwa upande wowote kihistoria na jukumu lake la baadaye, mbali na kuamsha jukumu la Mtandao wa Vijana wa Nchi Wanachama wa Harakati ya kutofungamana kwa upande wowote (NYM), Na kuunganisha viongozi vijana wenye ushawishi mkubwa katika ngazi ya nchi za kutofungamana kwa upande wowote na nchi rafiki.
Pamoja na kutoa fursa sawa kwa jinsia zote mbili kama lengo la tano la Malengo ya Maendeleo Endelevu ya 2030 linavyoonyesha, pia unawawezesha vijana na kutoa fursa kwa waigizaji kutoka nchi mbalimbali za Dunia kuchanganyika pamoja, na kuanzisha ushirikiano katika nyanja mbalimbali, si tu Barani bali katika ngazi ya kimataifa, kama ilivyotajwa katika lengo la kumi na saba la Maendeleo Endelevu.