Vikosi vya kiraia na vya kijeshi .. Mifano bora ya Wachipukizi na Walinzi wa Ardhi

Vikosi vya kiraia na vya kijeshi .. Mifano bora ya Wachipukizi  na Walinzi wa Ardhi

Baada ya mapinduzi ya Julai 1952, azimio la kwanza kabisa la Jamhuri lilitolewa  mnamo Oktoba 25, mwaka wa 1953 na Kanali Jenerali Mohamed Nagib kwa kuanzisha Ulinzi wa Kitaifa,  unaohusika na vituo vya kikanda ambao watu wake ni wanaojitolea kwa lengo la kulinda majengo na malengo muhimu.

na Rais Gamal Abdel Nasser aliposhika madaraka alitoa azimio namba 55 kwa mwaka wa 1968 kuhusu kuanzishwa kwa makundi ya ulinzi wa kiraia yatakayofanya baadhi ya mambo ya kulinda ukanda wa ndani na aliongeza kwamba makundi ya ulinzi wa kiraia ni kundi la kiraia na kitaifa ndani ya mikoa, 
wajibu wake ni kutoa misaada inayolinda safu za nyuma za vikosi vya silaha na mnamo Aprili 21, mwaka wa 1969,  azimio la Jamhuri namba 593 lilitolewa kwa kuanzisha uongozi wa vikosi vya ulinzi wa kiraia na wa kijeshi katika eneo la El-Qobba Bridge.

  Na mnamo msimu wa Joto mwaka wa 1971 Rais marehemu Mohamed Anwar Al-Sadat alitoa amri zake za kufundisha somo la 
huduma za kijeshi kwa wanafunzi wa shule na vyuo vikuu halafu azimio namba 46 mwaka wa 1973 lilitolewa kwa kuzifundisha kwa elimu ya sekondari na ya juu kwa ajili ya kuboresaha uelewaji wa kijeshi na kuwapa wanafunzi hawa wa shule na vyuo vikuu roho na upendo ili kuwa na kizazi cha vijana kina uwezo wa kuimarisha nchi ya Misri na pia kuandaa wanafunzi wote ili kulinda Jamhuri ya kimisri na safu za nyuma za vikosi vya silaha.

Mnamo Aprili 23, 2019 Bunge kupitia kikao chake lilikubali kurekebisha kifungu (200) kutoka katiba kilichojumuisha kazi za vikosi vya Kijeshi kulinda katiba,mambo ya kimsingi ya nchi na uraia wake kwa mujibu wa nafasi yake kama nguzo muhimu ya nchi ya Misri.

Mnamo Julai 27, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ,Abdel Fattah El-Sisi,kamanda mkuu wa vikosi vya Kijeshi alikubali marekebisho ya Kifungu cha (200) cha Katiba; kilichosema katika aya yake ya kwanza kabla ya mwaka  wa 2019 :Vikosi vya kijeshi viko kwa ajili ya raia na lengo lake ni ni kulinda nchi na usalama wa ardhi zake ,na taifa peke yake linalounda vikosi hivyo .na hakuna mtu anayeruhusiwa au mamlaka au kikundi kuunda miundo, timu,mashirika ya kijeshi au yasiyo kijeshi, na vikosi vya kijeshi vina bunge kuu lililoandaliwa na sheria.

Baada ya marekebisho kilitaja kwamba" Vikosi vya Kijeshi ni vya watu na lengo lake ni kulinda nchi na kuhifadhi usalama waka na ardhi zake ,katiba ,demokrasia, mahitaji ya msingi ya taifa,uraia wake ,mapato ya watu,haki na uhuru wa watu . Na taifa peke yake linaweza kuunda vikosi hivyo na hakuna mtu anayeruhusiwa au mamlaka au kikundi kuunda miundo makundi, mashariki ya Kijeshi au yasio Kijeshi .

Na pia baadhi ya vifungu vya sheria  namba (55) ya mwaka 1968 vimerekebishwa kuhusu mashirika ya Ulinzi ya Wananchi na sheria namba (46) ya mwaka 1973 kuhusu Ulinzi wa Kijeshi katika kipindi cha elimu ya sekondari na chuo kikuu, na Kifungu (5 mkariri) : kila mkoa una mshauri wa kijeshi na wasaidizi watosha wameteuliwa na waziri wa ulinzi,na kuainisha masharti ya kazi zao ambapo mshauri wa kijeshi anahusika na yafuatayo:

Kuwakilisha Wizara ya Ulinzi katika mkoa huo.

Kuchangia katika ufuatiliaji wa mara kwa mara wa huduma zinazotolewa kwa wananchi na miradi inayotekelezwa.

Mawasiliano ya kijamii na wananchi ili kujua matatizo yao na kuchukua hatua zinazohitajika.

Kuratibu na mamlaka husika katika mkoa kuchukua hatua zinazohitajika ili kufikia malengo ya maendeleo ya serikali katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni, na kuzuia kutokea kwa hatari kubwa inayodhuru Usalama na Amani ya nchi.

Kuratibu na mamlaka za elimu katika ngazi ya mkoa kutekeleza mtaala wa elimu ya kijeshi kwa mujibu wa sheria zilizowekwa na Wizara ya Ulinzi.

 Mashindano ya  ya vikosi wa  ulinzi wa watu ya  kijeshi

Matokeo ya vitendo vya (Vikosi vya Walinzi wa Kitaifa - Upinzani Maarufu) yalionekana katika miji ya Mfereji wakati wa majibu ya uchokozi wa pande tatu dhidi ya Misri mnamo 1956, katika Mapigano ya Port Said, yaliyofanyikwa mnamo Novemba 6, 1956, wakati vikosi (Walinzi wa Kitaifa, Upinzani Maarufu) waliweza kukabiliana na vikosi vya uhasama na kuwasababishia hasara kubwa.

Vikosi vya Ulinzi Maarufu na vya Kijeshi pia vilikuwa na jukumu la kishujaa katika Vita vya Oktoba 1973; Ilijumuishwa katika EPIC   ya kutokufa ya Suez, inayojulikana kama (Mapigano ya Kituo cha Polisi cha Arbaeen), ambayo yalifanyikwa mnamo Oktoba 24, 1973, wakati kikosi cha kijeshi cha Israeli kilipotoka kwenye barabara ya Zaitiya na kuingia eneo la Mkoa wa Suez, ambapo vikosi vya ulinzi maarufu na vya kijeshi chini ya amri ya Kanali Jenerali Adel Islam, mshauri wa kijeshi wa Jimbo la Suez, na kwa maagizo kutoka kwa Gavana Badawi Al-Khouli kutoa maagizo na maagizo ya kukabiliana na vikosi vya adui vinavyosonga mbele kwa kutumia RPG na silaha za kibinafsi, ambayo ilisababisha uharibifu wa vifaru (23) vya adui na kuuawa kwa adui (796).

Na kama muendelezo wa jukumu la kishujaa la Vikosi vya Ulinzi Maarufu na Kijeshi katika vita vya Oktoba 1973, walipewa kazi za kulinda mitambo na malengo muhimu na kulinda barabara za pili zinazoelekea Kairo kupitia Ismailia.

Kazi za Vikosi vya ulinzi wa wananchi na kijeshi ni yafuatayo:

Uratibu kati ya vifaa vya Kamanda Mkuu wa jeshi na Wakuu wa mikoa katika kukabiliana na majanga  na maafa na kuondoa athari zinazotokana.

 Ni kawaida Vikosi vya ulinzi wa wananchi na kijeshi vinaendelea kusaidia Vikosi vya utendaji katika mikoa katika kukabiliana na misiba na maafa, inayohitaji uratibu kamili na na Vikosi mbalimbali vinavyohusika na serikali .na hivyo kupitia/kuweka hali ya mgogoro (mafuriko_mzunguko wa gari moshi_kuunguliwa moto_kuanguka kwa jengo_...n.k) ndani ya mkoa. Kisha kila kurugenzi la serikali,kulingana na uwezo wake,vifaa,nguvu za binadamu na utaalamu wenye uwezo wa kupanga na kutekeleza kwa kushiriki katika kutatua hali hiyo. Pamoja na Mpangilio wa vifaa vya kiufundi na uhandisi na kufanya mtihani wa barabara ili kupima uwezo wa vifaa kutekeleza kazi zinazohitajika. Kisha hali ya dharura (mshangao) inawekwa na wote wawili vikosi vya ulinzi wa wananchi na kijeshi ili kupima uwezo vikosi vya utendaji (Vikosi vya usalama,trafiki,ambulensi /unafuu,polisi/ukoaji,mshikamano wa kijamii,Vijana na michezo,afya,elimu,umwagiliaji,makazi/Wakfu ,kanisa , Barabara/njia, Kilimo , Ulinzi wa Raia,na msemaji wa vyombo vya habari)kushughulikia na hali hiyo, pamoja na kuanzisha kambi ya dharura ya makazi kulingana na uwezo wa mkoa, ili watu walioathirika wahakikishwe kuwa mahali pazuri pa kukidhi mahitaji yao muhimu, inayochangia kuinua roho na nafsi yao.

Kuandaa vikao vya kielimu kwa wanafunzi wa shule na vyuo vikuu (za kiserikali / za kibinafsi ) na taasisi za juu za kibinafsi, Uratibu unafanywa na Wizara za (Malezi na Elimu ya Ufundi - Elimu ya Juu na Utafiti wa Kisayansi) ; kuandaa vikao vya kielimu kwa kushirikisha makundi yote ya jamii (vituo vya watoto yatima - mipango ya vijana - watu wenye ulemavu) , ambapo kikao kinajumuisha mada zinazoathiri Usalama wa kitaifa wa Misri, vitisho vinavyozunguka na kanda na vitendo vya kishujaa vya kupambana na jeshi katika vita dhidi ya ugaidi, pamoja na ushiriki wa wanafunzi wa chuo kikuu ndani ya shughuli za kikao ili kuonesha jukumu lao, pamoja na ushiriki wa watu mashuhuri wa umma, ambao wana hisia chanya na ushiriki wa timu ya kwaya, chuo kikuu na shule, katika aya ya kisanii wakati wa kikao, pamoja na kuwaheshimu wanafunzi bora, Familia za wafia imani na wahasiriwa wa operesheni za kigaidi.  Watu wenye ulemavu pia wanaheshimiwa kwa ushiriki wao na kuinua ari yao.

 

 Kuandaa maonesho ya bidhaa za watu wenye ulemavu katika makazi na vilabu vya vikosi vya kijeshi
          
 Jamii  inayothamini watoto wake wenye ulemavu,  kutumia msaada na utunzaji wote unaowezekana kwao,  ndiyo jamii ambayo iko karibu na kufikia viwango vikubwa zaidi vya maendeleo, kupiga hatua na ufufuo kamili katika nyanja zote ni lengo adhimu na tukufu kuwa Jamii inayoinua hadhi ya watoto wake, kuthamini mafanikio yao, na kuona uwezeshaji wao na ushirikiano katika nyanja zote za maisha .  Ni jambo la fahari na heshima kuona watoto wetu wa kiume na wa kike wenye ulemavu wakifikia matokeo mengi, ambayo hayajawahi kushuhudiwa katika nyanja mbalimbali, linalothibitisha ukubwa wa uwezo wao wa kukabiliana na matatizo na kuyashinda magumu; kama vile serikali inakupa kipaumbele maalum wanawe wenye ulemavu, kwa kuamini uwezo wao, kupitia kuonesha bidhaa za watu wenye ulemavu katika jukumu na vilabu vya Vikosi vya Wanajeshi chini ya usimamizi wa Vikosi vya Ulinzi Maarufu na Kijeshi, kwa lengo la kuinua ari ya watu binafsi na kufikia ushiriki wa jamii.

 Kuandaa sherehe za kisanii mnamo mwaka mzima wa masomo na wakati wa likizo na likizo rasmi

 Ambapo aya ya kisanii (Operetta - Nyimbo za kizalendo) inachezwa na Wachipukizi wa Wizara ya Vijana na Michezo mbele ya waheshimiwa (Waziri wa Vijana na Michezo - Waheshimiwa Magavana - Waheshimiwa Wakuu wa Vyuo Vikuu - Wawakilishi wa Bunge - Wanazuoni) na maonesho ikiwa ni pamoja na uchoraji, michoro ya kazi za wanafunzi zinazoangazia ujuzi wao na utamaduni wao.

Ushiriki katika Utekelezaji wa mradi wa Ujuzi wa Kusoma na Kuandika na kufundisha watu wazima

 Kwa mujibu wa Imani ya Vikosi vya kijeshi  katika umuhimu wa kujua kusoma na kuandika katika jamii ya Misri,na vikosi vya ulinzi maarufu na kijeshi vinachagania kwa utaratibu  na mamkaka kuu ya kusoma na kuandika na kufundisha watu wazima katika mradi huo kwa lengo la Usalama wa Kitaifa wa Misri, ambapo kamanda mkuu wa majishi Waziri wa Ulinzi na Uzalishaji  wa majishi  aliidhinisha kwa ukarabati wa walimu(2000) kwa lengo la kutokomeza ujinga kila mwaka kutoka bajeti ya jeshi.

Kuandaa ziara za nje Kwa wanafunzi wa(Shule/Vyuo Vikuu)

Ziara zinapangwa kwa (Vitivo/vitengo/madhahabu)na ziara za kijeshi hupangwa na wanafunzi wa(Shule/Vyuo Vikuu),na mashirika mbalimbali ya serekali kwa idadi ya(50:100)wanafunzi wa kiume na wa kike wameambatana na (Mkuu wa Chuo Kikuu/Naibu/Mkuu wa Shule/Afisa mwenye cheo kinachofaa).

Utekelezaji wa mikutano ya michezo katika Vitivo/Taasisi za kijeshi

Mikutano ya michezo inatekelezwa katika michezo ya pamoja,binafsi baada ya utaratibu uliopita pamoja na Shirikisho la michezo la Vyuo Vikuu-Mamlaka ya michezo -Byuo/Taasisi za kijeshi Kwa ajili ya kuchanganya baina ya kufanya mazoezi ya michezo kama lengo lenyewe,na kujua juu ya maisha ya kijeshi kwa upande mwingine na kukaribia kutoka nyumbani kupitia michezo.

Utaratibu wa kambi za kuishi pamoja kwa vipengele vya maskauti katika vitengo vya kijeshi

Utaratibu unafanywa na Shirikisho Kuu la Skauti na viongozi na utawala mkuu wa mapainia/Wizara ya Vijana na Michezo ili kutekeleza kambi ya kuishi kwa siku 5 ndani ya moja ya vitengo vya kijeshi ambayo ni pamoja na shughuli za mwingiliano(mgongo-Utetezi- urambazaji mwitu-sherehe ya burudani) inayolenga kuhamisha uzoefu na kukuza roho ya timu.

Ushiriki wa wanafunzi wa vyuo vikuu vya umma katika hafla ya kuhitimu vyuo vikuu vya kijeshi na vyuo vya ufundi.

Wanafunzi bora wa vyuo vikuu vya Misri wanashiriki katika hafla ya kuhitimu kwa wenzao kutoka chuo cha kijeshi, pamoja na usimamizi wa vikosi vya ulinzi wa kiraia na kijeshi.

Kuandaa kwa hafla za wanafunzi bora wa vyuo vikuu vya Misri

Vikosi vya ulinzi wa kiraia na kijeshi vinaandaa sherehe ya kila mwaka kwa wahitimu, sambamba na kuhitimu kwa vikundi vya vyuo vikuu na vyuo vya kijeshi ili kuongeza uhusiano kati ya wanafunzi bora wa vyuo vikuu vya Misri na wanafunzi bora waliohitimu vyuo vikuu vya kijeshi, aidha ngao zinabadilishana na Mheshimiwa Kamanda mkuu wa Majeshi, Rais wa nchi.

Uandazi wa ziara ya wanafunzi wa shule na vyuo vikuu kwa wajeruhiwa wa operesheni za kivita 

Ndani ya utunzaji uliotolewa na vikosi vya kijeshi kwa watoto wake waliojeruhiwa katika operesheni za kijeshi waliojitolea kila kitu kwa ajili ya kulinda ardhi na kuhifadhi utakatifu wake. Kwa hivyo, vikosi vya ulinzi vya kiraia na kijeshi vinajali kuandaa ziara za mara kwa mara kwa wanafunzi wa shule na vyuo vikuu vya Misri ili kuwafahamisha ushindi na kujitolea mhanga zilizofanyiwa na mashujaa hao kwa ajili ya nchi hii.

Usimamizi wa malengo muhimu na salama ( ulinzi mkali/ mashirika maarufu) vikosi vya ulinzi wa kiraia na kijeshi wanashiriki katika usimamizi juu ya vipengele vya kulinda malengo muhimu kwa kuratibu na Polisi wa kiraia kupitia kuandaa kozi za mafunzo pamoja na trafiki na uangalizi unaoendelea kwa viwango vya mafunzo na uwezo wao wa kulinda malengo muhimu kupitia washauri wa kijeshi.

Kuhudhuria kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kwa ufunguzi za miradi mikubwa ya maendeleo 

Ndani ya ujali wa Kamanda Mkuu wa Jeshi ili kuunga mkono jamii ya kiraia na kuendelea nafasi ya uzalendo kwa watu wote, uongozi wa vikosi vya ulinzi wa kiraia na kijeshi kwa kushirikiana na vyuo vikuu vya Misri kwa kuhudhuria wanafunzi wa vyuo vikuu vya umma na binafsi katika ufunguzi za miradi mikubwa ya maendeleo.
 
Vyanzo :

Tovuti ya Uongozi wa Vikosi vya Kiraia na Kijeshi.