Vijana na Michezo: Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa uko na Ufadhili wa Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi kwa mwaka wa tatu mfululizo

Vijana na Michezo: Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa uko na Ufadhili wa Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi kwa mwaka wa tatu mfululizo

Wizara ya Vijana na Michezo ilitangaza kuwa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa, katika toleo lake la nne uko na Ufadhili wa Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi, Rais wa Jamhuri, kwa mwaka wa tatu mfululizo, ambao unapangwa kufanyika mnamo Juni ijayo 2023 pamoja na kauli mbiu ya "Vijana wasiofungamana kwa upande wowote na Ushirikiano wa Kusini-Kusini", na hivyo kwa lengo la kuhamisha uzoefu wa Misri wa ujenzi wa taasisi. 

Ambapo, wakati wa matoleo yake ya zamani, Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa umepata sifa kubwa za kimataifa kwa kiwango kikubwa na katika ngazi kadhaa, kwa upande wa washiriki kutoka mabara ya ulimwengu, kama vile viongozi vijana katika mabaraza ya kitaifa, au katika ngazi ya watoa maamuzi na wanadiplomasia, tena umesababisha aina nyingi za ushirikiano katika ngazi ya kimataifa kati ya wahitimu wa Udhamini, na hicho ndicho kinachozingatiwa kiashirio halisi cha mafanikio ya Udhamini katika kufikia kipengele cha uendelevu kwa kuwekeza kwa vijana, ambayo ndio uongozi wa kisiasa unatamani kulingana na Ajenda yake ya Maendeleo 2030.

Udhamini huo hapo awali ulikuwa umepokea Ufadhili wa Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi, Rais wa Jamhuri, wakati wa toleo lake la pili, lililozinduliwa mnamo Juni 2021 pamoja na kauli mbiu ya "Ushirikiano wa Kusini na Kusini" kwa ushiriki wa viongozi vijana kutoka mabara ya Asia, Afrika, na Amerika Kusini. 

Pamoja na Upataji wake wa Ufadhili  wa Rais wa Jamhuri, katika toleo lake la tatu, lililofanyikwa mnamo Juni 2022, ambapo ulipanuka ili kujumuisha nchi rafiki, na  ulihangaika kukuza jukumu la vijana katika kufufua kanuni za kutofungamana na kuamsha ushirikiano kati ya Ulimwenguni Kusini(Global South), kama faili maarufu zaidi kwenye uwanja wa kimataifa zinazohitaji kuamshwa na kufaidika nazo kwa kuzingatia kupanuka kwa pengo la Ustaarabu na maendeleo kati ya nchi za Kaskazini na Kusini.