Chuo cha Kitaifa cha Mafunzo na Ubalozi wa Ufaransa zamheshimu mhitimu wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa

Chuo cha Kitaifa cha Mafunzo na Ubalozi wa Ufaransa zamheshimu mhitimu wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa

Bw. Ahmed Mukhtar,  Mhitimu wa kundi la pili la Udhamini wa Uongozi wa Kimataifa wa Nasser na Mhitimu wa Mpango wa Urais wa kuandalia  Watendaji Wanaohitimu  kwa Uongozi kundi la Timu ya Al-Assar amezawadiwa, na hayo yametokea  miongoni mwa shughuli  za maadhimisho ya Chuo cha Kitaifa cha Mafunzo na Kituo cha Utamaduni cha Ufaransa kwenye  makao makuu ya Ubalozi wa Ufaransa kwa ajili ya ushindi wa wahitimu wa kundi la  Jenerali Mohamed Al-Assar kutoka Mpango wa  uongozi  wa kuandalia Watendaji wa kuongoza  (EPLP), katika mtihani wa  Diploma ya Lugha ya Kifaransa (DELF) na hiyo inakuja ndani ya mfumo wa ushirikiano wa pamoja kati ya Misri na Ufaransa Kupitia ushirikiano wa Chuo cha Kitaifa cha Mafunzo "NTA" na Shule ya Usimamizi ya Ufaransa "L'ena ”, vilevile,  Maadhimisho hayo  yanakuja  ili kuthibitisha  juhudi za Chuo cha Taifa cha Mafunzo za kuwaandalia  viongozi wenye uzoefu mbalimbali ,  wenye uwezo wa zana mbalimbali za mawasiliano na wanaoweza kushirikisha kwa ufanisi  wa  kuleta mabadiliko kwa nchi yao.

Ahmed Mokhtar anafanya kazi kama mkaguzi wa usalama wa anga katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kairo.vilevile , ni kocha  na mwamuzi wa midahalo katika  baraza la  kiutamaduni la Uingereza , katika kipindi cha Sauti ya Vijana waarabu  na kisha programu ya Sauti ya Vijana ya eneo ya katikati .

Yeye pia ni mwanachama hodari  na mwenye uzoefu  kwenye jamii  ya kiraia tangu kipindi cha Chuo Kikuu na hivyo  kupitia Kamati ya  makundi katika Umoja wa Wanafunzi, naye  sasa ni mtafiti wa Shahada ya Uzamili ya Ujasiriamali  ambapo alikuwa ameshahitimu kutoka Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu cha Ain Shams mnamo 2005. licha ya  kujifunza katika Taasisi ya  kuwaandalia viongozi huko Helwan

Licha ya kupata kwake  kozi ya Mkakati wa Usalama wa kitaifa, Kozi ya Usimamizi wa Migogoro, Majadiliano na  kozi ya  kutunga Maamuzi inayohusiana na kuelimisha masuala  ya siasa kutoka Chuo cha Kijeshi cha Nasser, na baada ya kuhitimu  kwake kutoka Chuo Kikuu, alifanya kazi katika taasisi  za kimaendeleo kadhaa  mpaka akawa mwanachama katika kamati  ya Kiraia na Kazi ya kujitolewa  kwenye  Baraza la Kitaifa la Vijana mnamo 2010,  naye Sasa ni mwanachama  wa  wakurugenzi wa chama cha  Moameroon  cha maendeleo  ya jamii tangu 2016,  pamoja na kufanya kazi katika uwanja wa kutoa  mafunzo katika taasisi kadhaa.

Mokhtar alihitimu kutoka kwa  kundi la pili la Mpango wa uongozi wa  kuwaandalia Watendaji  kwa Uongozi katika Chuo cha Kitaifa cha Mafunzo, na  kupitia kwake alipata kozi ya usimamizi wa migogoro kutoka Kituo cha GCSP cha Mafunzo ya Usalama na Siasa nchini Uswizi, na kozi za usimamizi na uongozi kutoka shule ya   "L.ena  " huko Ufaransa.

 Ikumbukwe kuwa Udhamini wa  Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa , katika toleo lake la pili, ulikuwa na Ufadhili wa Mheshimiwa Rais Abd El Fatah El-Sisi na ulilenga viongozi vijana   wa utendaji wenye taaluma mbalimbali na watendaji ndani ya jamii zao, wakiwakilisha mabara matatu, Afrika, Asia na Amerika ya Kusini, pamoja na kauli mbiu "Ushirikiano wa Kusini-Kusini".