Siku ya Uhuru wa Sinai.. miaka 41 imepita tangu kurudi kwa ardhi ya Feruzi  

Siku ya Uhuru wa Sinai.. miaka 41 imepita tangu kurudi kwa ardhi ya Feruzi  

Peninsula ya Sinai kito cha taji la Misri, chanzo cha fahari kwa taifa, nyayo za Manabii (msingi wa Manabii), mahali pa siri kubwa, mlima wa kugeuka sura, mti uliobarikiwa na bonde takatifu.

Siku ya Aprili 25, Taifa la Misri laadhimisha miaka 40 ya Uhuru wa Sinai, likizo hii inachukuliwa kuwa moja ya siku muhimu zaidi katika historia ya hali ya Misri wakati wa kisasa, inayoshuhudiwa kilele cha vita vya ugomvi na Amani, mwanzo wa vita kuu ya Oktoba mnamo  1973, ambapo, Jeshi la Misri liliweza kupata ushindi na kurejesha kiburi cha Jeshi la Misri, na kisha kuanza majadiliano ya Amani, hadi kila inchi ya nchi ya Sinai iliporejeshwa.

Misri iliikomboa ardhi yake iliyokalowa mnamo 1967 kwa njia zote za mapambano... Kuanzia kwenye mapambano ya silaha katika vita vya uasi na kisha hadi vita vitukufu vya Oktoba mnamo 1973, pamoja na kazi ya kisiasa na kidipolmasia, kuanzia na mazungumzo magumu ya kutenganisha vikosi mnamo 1974 na 1975, pia mazungumzo ya Camp David ambayo yalisababisha mfumo wa Amani katika mashiriki ya kati "Mkataba wa Camp David" mnamo 1978, iliyofuatiwa na kutiwa saini kwa mkataba wa Amani wa Misri na Israel mnamo 1979.

Kwa muda wa miaka 41 tangu kukombolewa kwa Sinai, eneo hilo la thamani limekuwa kitovu cha uangalifu wa taifa hilo hadi limekuwa kiashirio cha Amani na Maendeleo.

Siku ya uhuru wa Sinai, haikuwa likizo ya kitaifa ya Misri tu, lakini sikukuu ya kitaifa kwa nchi zote za kiburi.