Sherehe ya Wamisri kwa Eid Al-Fitri

Sherehe ya Wamisri kwa Eid Al-Fitri

Imefasiriwa na / Fatma Mahmoud


wakati wa kuingia  Uislamu  nchini Misri mnamo karne ya saba AD, Eid Al-Fitri ikawa mojawapo ya Sikukuu muhimu zaidi za kidini zinazosherehekewa   na Wamisri, ambayo  shughuli zake kati yao zilitofautiana na ulimwengu  wa Kiislamu kote , haswa katika enzi mbili  za Fatimid na Mamluk. 

Maandalizi ya Eid Al-Fitri yalianza mwishoni mwa mwezi wa Rajab, ambapo serikali iliainisha  kiasi cha dinari 20,000  zinazopa "Dar Al-Fitri", iliyoundwa na Wafatimi kwa ajili ya kupika keki na peremende,ambapo wanapika keki zinazojazwa  kwa karanga  pamoja dinari za dhahabu , na dinari moja ilikuwa imetosha gharama za familia kwa miezi mitatu kwa uchache, vilevile Dar Al-Fitri ilikuwa ikisambaza keki na peremende kwa wakuu na  umma kwa ujumla kabla ya Sikukuu, na baadhi ya vipande  vilipelekwa nchi jirani pia. pamoja na hayo , kiasi  kikubwa cha pesa kilikuwa kiimeainishwa  ili kutengeneza "   mapambo " nazo  ni   nguo  za  pamba na hariri zilizoshonwa kwa dhahabu na Fidha  na hizo zilisambaza  kwa watu   kiasi kwamba  wamisri waliita Eid Al-Fitri "sikukuu ya   mapambo."

Mnamo wiki ya mwisho ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, misikiti hupambwa na kuwashwa kwa taa, na muadhini huimba kasida - kabla ya kila adhana -  kasida za "Tawshih za Ramadhani" kwa kuaga mwezi mtukufu, wakisema:

 “Mwenyezi Mungu hajaweka mwezi mtukufu hukumbukwa  zaidi yako ewe Ramadhani .. hajaweka mwezi mtukufu hukumbukwa  zaidi yako  ewe mwezi wa Qur’an.”

Wakati jua linapozama mnamo usiku wa mwisho wa Ramadhani, msafara mkubwa unaoongozwa na hakimu mkuu na anasindikizwa na  Mashekh na wakuu wa amri za Kisufi hupanda Mlima wa  Mokattam ili kuangalia  wa mwezi wa   Shawwal,  hadi ikiwa  mwezi wa mpevu  ikithibitishwa, misikiti inatangaza kuwa kesho ni siku ya kwanza ya Eid Al-Fitri.

Kuanzia Asubuhi ya Eid ,  umati mkubwa wa watu ukisubiri mbele ya kasri ya Khalifa kwa ajili ya msafara wake ili kwenda kuhudhuria swala ya Eid, ambapo msafara wa idadi mkubwa   ya wana wa mfalme na askari huelekea uwanja wa swala ya Eid . ambayo  kawaida hufanyika Bab Al-Nasr,  pia  ,msafara mwingine unatoka mbele ya nyumba ya imamu wa swala pamoja na masheik, wataalamu na umma kwa uwanja wa swala ya Eid , pindi  swala imeisha ,  msafara wa khalifa unasonga pamoja na kundi la wapiganaji na wakuu, na vikundi vya Sufi, tembo na twiga pia hushiriki  kwenye  masindikizo haya, hadi uwanja wa sherehe kwa  sikukuu ambapo  " Sumat" inafanyika, ambayo ni  Karama ya chakula    kubwa inayoendelea kutoka asubuhi hadi sala ya adhuhuri na hudumu kwa muda wa siku tatu, na huandaliwa kwa  Kiasi kikubwa cha chakula, kinywaji, keki na pipi, na wakuu na mafaqihi wanampongeza khalifa kabla ya kukaa mezani, na khalifa anawapa zawadi na dinari za dhahabu ,  pia hurusha dinari za dhahabu  dirishani mwa jumba lake kama mkono wa  eid  kwa watu, ambayo ilijulikana kama "Jamaika" . vilevile , anaamrisha kutoa msamaha kwa wafungwa katika tukio hili la heshima, na  Watu  hutoka ili kusherehekea sikukuu kwenye bustani na matembezi  kwenye ufuo wa Mto Nile, ambapo muziki, wanasarakasi, wacheza muziki, na vikao vya burudani vilieneza  kufurahia  Eid iliyobarikiwa.

Vyanzo

Tovuti ya Makumbusho ya Ustaarabu ya Misri.