Manuel Scorza ... Mshairi , mwandishi wa riwaya na   mwanamapinduzi

Manuel Scorza ... Mshairi , mwandishi wa riwaya na   mwanamapinduzi
Manuel Scorza ... Mshairi , mwandishi wa riwaya na   mwanamapinduzi
Manuel Scorza ... Mshairi , mwandishi wa riwaya na   mwanamapinduzi

Manuel Scorza alizaliwa mnamo Septemba 7,1928 AD, katika mji wa Lima, mji mkuu wa Peru, na alikaa miaka kadhaa ya utoto wake katika mji wa Acurea katika jimbo la Huancapilica baada ya familia yake ilihamia huko.

 Manuel Scorza alisoma katika Shule ya Kijeshi ya Leoncio Prado, na mnamo 1945 aliingia Chuo Kikuu cha Kitaifa cha San Marcos.

Scorza alianza shughuli zake  za kisiasa wakati wa enzi ya Rais Manuel Udrea, ambapo alichapisha kitabu chake cha kwanza pamoja na kichwa "Faili za Mbali", ambacho kilisimamishwa na mamlaka ya Peru, na kumhamisha  kwa   Mexico mnamo 1949.  Scorza alikaa miaka  kumi Uhamishoni, hiyo miaka  ilikuwa migumu ambayo mvulana huyo alijifunza masomo ya utu wakati  hali ngumu ambayo iliacha alama  za nguvu  zake katika maisha yake kwa ujumla na   ya kifasihi, ambapo aliweza kuigeuza kwa   vipande vya mashairi  venye  Uhai na hamasa  , ambavyo alividhihirisha  kwenye  mkusanyiko wake wa mashairi "Laana", ambayo aliichapisha akiwa uhamishoni mwaka wa 1955 AD.

Mnamo 1959, Scorza alipata  Tuzo la Kitaifa la Ushairi kwa kitabu chake cha kwanza na hiyo  baada ya kurudi kwake kutoka uhamisho, baada ya  udikteta ulisitishwa . Tangu wakati huo huo, alianza awamu wa kiutamaduni  mashuhuri na mpya   huko Amerika Kusini ambapo alifikiria   mradi wa kiutamaduni, unaolenga kuufanya utamaduni  upatikane kwa kila mtu, kupitia  kufanya maonyesho ya vitabu na kuviuza kwa bei nafuu. mnamo muda wa chini ya wiki moja, mkusanyiko wa vitabu vya elfu kumi na tano vilivyotolewa kwa ajili ya kuuzwa kwenye maduka , vilivyopo katika maeneo mbalimbali ya mji mkuu, uliishauzwa . Uzoefu huo huo ulirudiwa kwa mafanikio sawa sawa huko Colombia, Venezuela na Cuba, ambapo vitabu vilikuwa vikichapishwa kwa bei nafuu na jukumu la wakala wa kuuza kukomeshwa,  kutokana  na hayo   Scorza akawa  mchapishaji maarufu .

Mnamo 1968, Manuel aliondoka Peru tena wakati wa migogoro iliongezeka ukali  ambayo    milima ya Peru ya Kati, ambapo aliingia ndani yake  kwa  lengo la kupata sera inayoheshimu wakazi wa asili wa India na kuwapa haki zao .

ingawa  Scorza ni mshairi,  ila   alipata ubora  wa kweli wa  kifasihi kwake  katika riwaya , ambayo ilimpa nafasi pana ya kuzungumzia upinzani wa wakulima wa Peru kwa hivi Riwaya yake ya kwanza   " Ngoma zinapigwa kwa ajili ya Ranks "  ilikuja kuwa   kipindi cha kwanza cha  makundi ya riwaya yanayopewa  kauli mbiu  mbili: "Palada" na "Vita Kimya." Riwaya hizo zilijumuisha: "Hadithi ya Garabombo Aliyefichwa", " bingwa anaye wasiwasi  ", "Wimbo wa Agapito Robles", na " kaburi ya matumaini",  kupitia  hizo,  Scorza aliweza kuchanganya ngano za kale na hadithi kwa mtazamo  wa kishairi wa juu  na kwa mtindo uliozifanya kuimarika hadi kiwango cha fasihi ya ulimwengu wakati wa  miaka saba kuanzia  (1972-1979 BK),  vilevile ,zimetafsiriwa  kwa lugha zaidi ya arobaini.

Mnamo 1982, Manuel Scorza alichapisha riwaya yake ya mwisho pamoja na kichwa " Ngoma isiyo na kifani." Riwaya hii ilikuwa peke yake  kabisa na  zilizopita. Na zinaonesha hatua mpya na mtindo  mpya wa uandishi, lakini kifo kilizuia hilo, ambapo Scorza aliaga Dunia katika ajali ya  ndege ya Avianca safari ya  011, ilipokaribia Uwanja wa Ndege wa Barajas katika mji mkuu wa Uhispania, Madrid, baada ya kugongana na  makundi ya vilima mnamo tarehe 27  Novemba  1983 BK  , ajali hiyo ilisababisha kifo cha Abiria 181, wakiwemo mhakiki wa fasihi Uruguayan Angel Rama na mwandishi wa Mexico Jorge Ibargüengoitia.