Baraza Kuu la Utamaduni

Baraza Kuu la Utamaduni
Baraza Kuu la Utamaduni

Uamuzi wa kuanzisha Baraza Kuu kwa Sanaa na Ustawi wa Fasihi uliidhinishwa kwa mujibu wa Sheria Namba 4 kwa mwaka 1956 , liwe taasisi  huru linaloambatanishwa kwa Baraza la Mawaziri , lenye  jukumu la kuratibu na kuunganisha juhudi za mashirika ya serikali yanayofanya kazi katika nyanja za sanaa na fasihi.

 Miaka miwili baadaye, Baraza lilikuwa na uwezo wa kudhamini sayansi za kijamii.Kwa karibu robo ya karne, Baraza Kuu la Sanaa, fasihi na Sayansi za Kijamaa liliendelea kuchukua jukumu lake katika maisha ya kitamaduni na kitafakari nchini Misri

Mnamo 1980 ilibadilishwa kwa "Baraza Kuu la Utamaduni "kwa kutolewa na sheria  namba 150 kwa mwaka 1980.Baraza Kuu la Utamaduni liliongozwa na Waziri wa Utamaduni. Na katibu mkuu kwa Baraza kuu la Utamaduni ana jukumu  kuendesha sera yake na anasimamia utekelezaji wake, na jambo lile halikuwa kubadilisha jina tu bali ilibadilika katika jukumu na malengo.  Basi kwamba Baraza Kuu la Utamaduni limekuwa akili inayopanga kwa ajili ya sera ya kitamaduni nchini Misri kupitia kamati zake  zifikazo kamati ishirini na nane, ambazo ni pamoja na kikundi cha wasomi  na wabunifu kutoka vizazi na mienendo tofauti.

Mnamo miaka ya hivi karibuni, Baraza Kuu la Utamaduni limeshuhudia kuongezeka kwa shughuli zake. Ambapo limekuwa kituo cha kitamaduni na mawazo kwa kiwango cha kimisri na kiarabu na ngome ya kuijua  kupitia mikutano na semina zilizopangwa na kuhudhuriwa na kikundi cha wasomi na watafakari waarabu, ambayo ikawa inafaa kwa mwingiliano wa kitamaduni kwa kiwango cha Kiarabu pamoja na Ushiriki wa watafiti wengine mashuhuri katika taasisi za kimasomo ulimwenguni  mashariki na magharibi katika shughuli za Baraza.

Jengo la kisasa la Baraza Kuu la Utamaduni liko katika ukumbi  wa Opera., Jengo hilo linaangalia mto wa Nile kutoka upande wa magharibi wa barabara ya Um Kulthoum. Na kutoka upande wa mashariki huangalia  Ukumbi wa nyumba ya kimisri ya Opera .

 Jengo hilo lina maktaba kuu  inayoweza kuchukua watu 50 na kazi kuu ya maktaba katika jengo jipya la Baraza kuwa maktaba kwa vitabu vya zamani ambapo inajumuisha kikundi cha masomo, kamusi na vitabu vya zamani muhimu katika nyanja zote za elimu ,pamoja na kikundi cha vitabu vya zamani, na ambazo hakuna maktaba moja nchini Misri inayozijumuisha.

Maktaba pia ina machapisho ya Baraza , Kituo cha kitaifa kwa Ufasiri  , mfululizo wa kitabu cha kwanza, semina na mikutano inayofanyikwa kwa Baraza.

 Jukumu la Baraza Kuu kwa Utamaduni:

Baraza Kuu la Utamaduni linachangia mafanikio mengi katika ngazi ya kitamaduni na kimawazo, kitaifa , kikanda na kimataifa.  Na miongoni mwa Mafanikio haya ni:

 Baraza limepanga mikutano na semina nyingi za kitaifa, kikanda na kimataifa, ambapo limejadili masuala mengi ya mawazo, utamaduni, sanaa na fasihi . , kama vile ilivyokuwa eneo la mawasiliano ya kiakili kati ya wafikiri na wabuni wamisri, waarabu na wazungu katika miaka iliyopita.na miongoni mwa mikutano hii ya kimataifa ni mkutano wa Amaz Donkol , mkutano wa riwaya ya kimisri- kimorocco . Mkutano wa mwanamke mwarabu  na Ubunifu, Mkutano wa Masuala ya Ufasiri na Mingiliano ya kitamaduni , pia Baraza lilisherehekea kumbukumbu ya alama za kitamaduni, mawazo, waumbaji na wafikiri kupitia semina tofauti, Na maadhimisho ya Baraza yaliongezeka hadi alama kadhaa za mawazo ya kimataifa na sanaa na maandiko, ya zamani na ya kisasa, kama vile:Federico Garcia Lorca - Sophoances - Bertold Brecht - Alexander Pushkin - Ibn Rushd - Refaah Al Tahtawi - Abdul Rahman Al Rafie - Jamal Al Deen Al Afghani - Mohammed Abdo - Zaki Naguib Mahmoud - Salah Abdel Sabour -  Berm Eltunsi - Umm lilting -Naguib Rihani - Abi Hayyan Tawhidi - Taha Hussein - Tawfiq al-Hakim - Mahmoud Said, pia Baraza limetoa kundi la nakala kadhaa, ambazo zimetayarishwa na kamati tofauti za Baraza kama jarida la  njia za muziki, jarida la falsafa,  jarida la kitabu na kuchapisha, jarida la Ufasiri.

Katika kiwango cha Tuzo za nchi : Serikali iliunga mkono jukumu la Baraza katika kukuza ubunifu na kuthaminiwa kwa wasomi na watalam kwa kurudisha idadi ya  tuzo za nchi kwa  kutathmini uhamasishaji, ambazo hupewa kwa Baraza Kuu la Utamaduni katika matawi ya sanaa, fasihi na sayansi za kijamii kulingana na  kuteuliwa kwa taasisi kadhaa za kisayansi na kiutamaduni. Na gharama za tuzo zile ziliongezeka kufikia paundi laki mbili  kwa tuzo za kutathmini .

Tangu mwaka  wa 2003, Baraza limeanza kutoa barua mpya inayoitwa "Machapisho ya hivi karibuni" ambayo ina orodha ya machapisho ya hivi karibuni ya Baraza iliyotolewa wakati wa robo mwaka , nayo ni habari mfululizo ya kila miezi mitatu.

Shughuli za Baraza zimepokea msaada na uungaji mkono wa nchi . na Baraza lilishuhudia maendeleo wazi katika shughuli zake  mnamo miaka ya hivi karibuni. , na limekuwa kituo cha utoaji wa kiutamaduni na kielimu katika ngazi za kitaifa, kikanda na kimataifa, ambapo maisha ya Baraza yalikaa zaidi ya miaka arobaini na tano, na lilikusanya  wataalam wa sanaa, fasihi na sayansi za kijamii, na likaanza shughuli zake ambazo ziliamriwa katika sheria ya kuanzishwa kwa mipaka mipana zaidi iwezekanavyo, na kupitishwa kutoka miradi isipokuwa ikiwezekana kuingia kwenye shughuli za taasisi ya kiserikali au shirika la umma.

 Malengo ya Baraza Kuu la Utamaduni:

Ni kurahisisha njia za kiutamaduni kwa watu na kuziunganisha na maadili ya kiroho, kwa kukuza demokrasia ya utamaduni na kuifikia katika sekta pana zaidi ya watu , pamoja na  likikuza vipaji katika nyanja tofauti za utamaduni, sanaa na fasihi, kufufua urithi wa zamani na kuwajulisha raia kwa tija za maarifa ya kibinadamu, na kuthibitisha maadili ya  jamii ya kidini, kiroho na maadili.

Inatafutia kuratibu juhudi za kiserikali na za kijamii katika nyanja za sanaa na fasihi. Kwa hivyo Baraza hilo lilikuwa la kwanza kwa aina yake kwa uwanja wa Kiarabu, lililosababisha kuhamasisha nchi nyingi za Kiarabu kuifuata Misri na kuunda Mabaraza kama yale.

Vyanzo

Tovuti ya Baraza Kuu la Utamaduni.