"Gamal Hemdan na mapinduzi ya Juni 1967 "
Na/ Shahdy Attya
Yaliyotokea mnamo Juni 5, 1967 na kwa yale yaliyofuata, kutoka kwa kurudi nyuma hadi kushindwa,janga, mkasa, n.k yote yaliitwa kwa namna tofauti tofauti .
Miongoni mwa majina ambayo yanaelezea ukweli wa kile kilichotokea kwa taifa la Kiarabu mnamo wakati huo, Dkt. Gamal Hemdan, katika utafiti muhimu ulioitwa ," malengo thabiti na mbinu zinazobadilishwa " aliuchapisha kwenye jarida la Al-Kateb mnamo Agosti 1967 na akautambulisha kwa “Mapinduzi ya Juni ya 1967” , Utafiti huo muhimu na wa hatari, uliozidi kurasa 25, ulikuwa la kwanza ulioandikwa na Gamal Hemdan baada ya kipindi cha kurudi nyuma ambapo ulifichua kiwango cha ufahamu wa Gamal Hemdan juu ya ukweli wa uchokozi wa kimarekani na kizayuni dhidi ya taifa la kiarabu. taifa, ambalo ni uharibifu wa uongozi wa kimapinduzi unaoendelea katika nchi, na kwamba kutoka kwa raia mnamo Juni 10 kwa haraka na kwa hiari kumeshindwa uchokozi kufikia kiini cha malengo yake, na siku zimethibitisha ukweli wa nadharia ya Gamal Hemdan ambapo Israel haikuweza kuhisi kwamba imeshinda na kufikia malengo yake kamili kutokana na uchokozi wa 1967 isipokuwa baada ya kutokuwepo kwa Gamal Abdel Nasser . vilevile ,Gamal Hemdan kupitia utafiti wake, akielezea upinduzi wa raia dhidi ya mapinduzi ya kimataifa, mapinduzi ya 1952 yanagalikuwa mapinduzi dhidi ya mapinduzi ya ndani, mapinduzi ya Juni 1967 yangalikuwa mapinduzi dhidi ya mapinduzi ya kimataifa, Gamal Hemdan anasema katika utafiti wake:
Hakuna kitu kabisa ambacho kinatufidia kwa kurudi nyuma kwa jeshi isipokuwa ushindi wa kijeshi wenye uzito mkubwa, na labda hakuna mtu aliyegundua lengo la kurudi nyuma kwa jeshi kama vile bingwa shujaa anayesimama imara Abdel Nasser alivyoligundua hilo jioni ya tarehe 9 Juni , wakati ambapo hakuna pia isiyotambua lengo la mzozo huo mzima kama vile umati wa taifa la Kiarabu walivyotambua mnamo tarehe 10 Juni , na kati ya hili na lile, mapambano ya kiarabu dhidi ya njama ya kikoloni yalikosa kwa upesi na kwa moja kwa moja inastaajabisha lengo lake kuu na la msingi, ambalo ni kuwaangamiza viongozi wakuu wa mapinduzi katika nchi kubwa.kwa mtazamo huu, hakuna shaka kwamba uchokozi umeshindwa kufikia malengo yake ya msingi. Kwa hakika bado hatujatambua lengo la tarehe tisa na kumi ya Juni, na tunaamini kwamba yataandikwa katika historia ya Waarabu kama ni hatua ya mabadiliko makubwa na ishara kubwa njiani ambapo mvutano wa njama ulikuwa mapinduzi ya kijeshi tu na lengo lake lilikuwa kuua mapinduzi na kuyazika milele kama nchini Misri au nchni Syria lakini kilichotokea kilikuwa kinyume kabisa, ambapo ilikuwa ni kuweka Upya kwa vijana wa mapinduzi ya kitaifa ya maendeleo na kuwafufua milele .
bali hatutii chumvi sana tukisema kwamba ni mapinduzi mapya yanayokamilisha mapinduzi ya kitaifa na mapinduzi dhidi ya mapinduzi ya kupinga Ikiwa mapinduzi ya Julai 1952 yalikuwa ni mapinduzi dhidi ya mapinduzi ya ndani, basi ya Mapinduzi ya Juni 1967 yalikuwa ni mapinduzi dhidi ya mapinduzi ya kimataifa, ya kwanza yalikuwa mapinduzi ya silaha kwa maslahi ya watu na ya pili ni mapinduzi maarufu kwa maslahi ya uongozi wenye silaha, ya kwanza yalitoka kambini ili kulinda watu kutoka hatari ya ndani na ya pili yalitoka barabarani ili kulinda kambi kutoka kwa hatari ya nje .. Kwa hili - kwa mantiki na mfano sahihi - mzunguko wa mapinduzi ulifanyika kama mzunguko wa umeme uliofungwa, na watu na jeshi walikutana kimapinduzi mara mbili: katika mara ya kwanza jeshi lilikuwa kiongozi na mara ya pili raia walikuwa viongozi ...
kwangu , sijui kama utafiti huo ulichapishwa tena ndani ya kile kilichokusanya kutoka kwa makala za Gamal Hemdan kwa maadhimisho ya maonesho na kuchaguliwa kwake kama Mtu wa Mwaka au la. ikiwa mimi miongoni mwa wasimamizi wa maonesho haya nitachapisha utafiti huo katika kijitabu kutokana na umuhimu wake sio tu katika maoni yake wazi kwa lengo la mvutano wa kiarabu kiisraiel bali kwani wenye sababu zinazoshawishi Gamal Hemdan kujitenga baada ya katikati ya miaka sabini wakati ambapo aliona na kutambua vipi mapinduzi yameharibiwa na uchokozi umepata malengo yake yote zaidi ya Gamal Hemdan mwenyewe alivyodhania baada ya kutokuwepo uongozi wa mapinduzi kutoka eneo hilo .