Gamal Abdel Nasser ni mwanafunzi
Na: Amr Sabih
Wapinzani wa Gamal Abdel Nasser na mapinduzi yake hawapotei wakati wala nafasi ila kushikilia uwongo mbalimbali kwake, na moja ya uwongo wao wa kuchekesha ni madai kwamba Gamal Abdel Nasser ni mwanafunzi asiyefanikiwa kupitia kulinganisha makao zake za Cheti cha Sekondari mwaka 1936 na jumla ya Shule ya Sekondari sasa, nao wafanya hivyo kwa kuchapisha cheti cha uwongo ambacho wanadai kuwa cheti cha shule ya upili cha Gamal Abdel Nasser.
Kwa viwango vya wakati wake, Gamal Abdel Nasser alikuwa mwanafunzi bora aliingia Kitivo cha Sheria, kilichokuwa mojawapo ya vitivo vya juu mnamo wakati wake, ambapo Viongozi wa Misri walihitimu kutoka humo kabla ya mapinduzi, Mustafa Kamel, Muhammad Farid, Saad Zagloul, Mustafa Al-Nahhas na wengine.
Gamal Abdel Nasser alijiunga na Kitivo cha Sheria mnamo Oktoba 1936, na akakaa miezi 6 huko, kabla ya kujiunga na kundi la kipekee katika Kitivo cha Kijeshi mnamo Machi 1937.
Vigezo vya maksi na vipimo vya mafanikio sasa, ni tofauti na ilivyokuwa zaidi ya miongo 8 iliyopita, na wakati Gamal Abdel Nasser alipata Baccalaureate yake "shule ya upili" kwa sehemu ya fasihi mnamo 1936, na shahidi kubwa kwa jambo hilo ni kwamba Gamal Abdel Nasser aliweza kujiunga na Kitivo cha Sheria, "Chuo Kikuu cha Fouad I" wakati huo - Kairo sasa -, Kitivo cha Sheria wakati huo kilikuwa mojawapo ya vitivo vya juu ambavyo Viongozi, Mawaziri na Wakuu wa Jamii walihitimu.
Idadi ya wanafunzi walio na shahada wa Baccalaureate nchini Misri mnamo 1936 - mwaka huo Gamal Abdel Nasser alipopapata Baccalaureate - ilikuwa wanafunzi 4000.
Huko Misri hadi katikati ya miaka ya sitini ya karne ya ishirini, mwanafunzi apataye 65% katika sehemu ya kisayansi ya shule ya upili , anaweza kujiandikisha katika kitivo cha Tiba, Uhandisi, na Dispensari, na mwenye Kiwango hicho hicho katika sehemu ya fasihi ya shule ya upili aliweza kujiunga na Vitivo vya Al-Alsun, Uchumi na Sayansi za siasa, na Vyombo vya habari.
Jumla ya shule za upili ilibakia katika kiwango hiki hadi Rais Anwar El-Sadat alipoharibu elimu katika shule za kimataifa, lugha na za kibinafsi, na mbinu sawa ukifuatiliwa na Rais Hosni Mubarak, na hata kupanua katika kuanzisha vyuo vikuu vya kibinafsi na kubadilisha mifumo ya shule za upili, Jambo lililosababisha machafuko makubwa ya kielimu nchini Misri, nadra sana kuyaona katika nchi nyingine, ilisababisha uharibifu wa mfumo wa elimu wa Misri,na kuigeuza elimu kuwa bidhaa kwa mwenye uwezo wa kulipa gharama yake kubwa.
Tumesoma, tumesikia tena tumeona wanafunzi waliopata 99%, 100% na 101%, na hawawezi kusoma au kuandika bila makosa, pia walifeli katika taaluma zao baada ya shule ya upili kwa sababu alama zao kwa sababu ya mfumo wa mafunzo na ufundishaji, na kwa malipo ya wazazi wao kwa huduma ya elimu na si kwa sababu ya fikra na kipaji zao.
Gamal Abdel Nasser alikuwa na bidii katika masomo, baada ya miezi 6 ndani ya Kitivo cha Sheria aliacha kisha akajiunga na Chuo cha Kijeshi katika darasa la kipekee kutokana na mkataba wa 1936, na baada ya kuhitimu kama afisa katika jeshi la Misri, alitayarisha masomo ya uzamili, na akapata shahada ya uzamili kwa tasnifu yake juu ya mistari ya ulinzi kwa Misri, pia alichukua kozi ya Wafanyikazi wa Vita, na alifanya kazi kama mwalimu katika Chuo cha Kijeshi kwa masomo ya historia, upelelezi na mkakati.
Muhammad Ali Pasha, mwanzilishi wa familia ya juu na chimbuko la fahari kwa Al-Shamsharjieh, alikuwa hajui kusoma na kuandika na hakujifunza katika maisha yake yote, na pamoja na hayo, alikuwa mwanasiasa mahiri, Pia, Mfalme Farouk, ambaye anaombolezwa sana na Al-Shamsharjieh , hakumaliza elimu yake hata kidogo.
Ama Al-Khwan ni lazima wakumbushwe kuwa Mohamed Morsi, El-Beltagy, El-Arian, Badie', El-Shater na Ezzat ni miongoni mwa viongozi wakuu wa Al-Khwan,Walikuwa madaktari, wahandisi na maprofesa katika chuo kikuu, na licha ya hayo kiwango chao cha kisiasa hakikuwepo hata kidogo, hawakuweza kudumisha nguvu na walifukuzwa kwa urahisi!!.
Gamal Abdel Nasser alikuwa na uhakika aliposema:
Wamarekani na wafuasi wao hawatanisamehe kwa niliyowafanyia.. niko hai au maiti.
Picha hiyo ni ya cheti cha uzushi unaosambaa kwenye mitandao ya kijamii, na pamoja na picha ya Rais Gamal Abdel Nasser, anayetafuta kitabu cha kigeni?!! Wakati sayansi na hisabati huonekana ndani ya masomo ya cheti, ijapokuwa Gamal Abdel Nasser alikuwa anasoma katika idara ya fasihi!! Pia cheti hicho kina jina la cheti cha shule ya upili , ingawa wakati huo jina la cheti mnamo 1936 ni Baccalaureate.