Uzinduzi wa shughuli za siku ya pili ya "Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa " katika toleo lake la pili, kwa kutembelea Makumbusho ya Kiongozi Gamal Abdel Nasser

Uzinduzi wa shughuli za siku ya pili ya "Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa " katika toleo lake la pili, kwa kutembelea Makumbusho ya Kiongozi Gamal Abdel Nasser
Uzinduzi wa shughuli za siku ya pili ya "Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa " katika toleo lake la pili, kwa kutembelea Makumbusho ya Kiongozi Gamal Abdel Nasser
Uzinduzi wa shughuli za siku ya pili ya "Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa " katika toleo lake la pili, kwa kutembelea Makumbusho ya Kiongozi Gamal Abdel Nasser

  

 Asubuhi ya leo ,Alhamisi , Wizara ya Vijana na Michezo iliandaa ziara ya kutembelea Makumbusho ya Kiongozi  Marehemu Gamal Abdel Nasser, ikiwa ni sehemu ya shughuli za siku ya pili ya Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa - Kundi la tatu, lililoandaliwa na Wizara hiyo pamoja na Ufadhili wa Mheshimiwa Rais Abd El Fatah El-Sisi, Rais wa Jamhuri, kwa ushiriki wa Viongozi Vijana 150 kutoka Nchi Zisizofungamana kwa upande wowote na Nchi Rafiki, unaotarajiwa kufanyika kuanzia Mei 31 hadi Juni 17, 2022 huko Kairo kwa kauli mbiu "Vijana Wasiofungamana kwa upande wowote na  Ushirikiano wa Kusini-Kusini".


Kwa kuzingatia ziara yao ya Makumbusho ya Kiongozi Marehemu Gamal Abdel Nasser, Kikao kilifanyika kwa washiriki wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa, kwa mahudhurio ya Mheshimiwa Waziri Mohamed Al-Orabi, aliyekuwa Waziri wa zamani sana wa Mambo ya Nje, Waziri Mwakilishi Munther Selim, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Makundi ya Kisiasa na Kikanda, Dkt. Adel El-Adawy, Profesa Msaidizi wa Mahusiano ya Kimataifa katika Chuo Kikuu cha Marekani, na Mshauri wa Uchumi Gamal Khaled Gamal Abdel Nasser, mjukuu wa Kiongozi Marehemu Gamal Abdel Nasser,aliyezungumzia utu na uongozi usio na kifani kwa kiongozi Gamal Abdel Nasser, mwanadamu, ambaye ndani yake ni mfano unaojumuisha ujuzi wa uongozi, mfano wa kuigwa na mfano kwa wengine na mafanikio yake ya kiutamaduni ya kitaifa ya Misri. kuandika matembezi na mapambano yake na kile alichotolewa na  Kiongozi Marehemu.


 Katika ziara yao ya kutembelea Jumba la Makumbusho la kiongozi Marehemu Gamal Abdel Nasser katika eneo la Manshiyat Al-Bakry mashariki mwa Kairo, Viongozi Vijana wanaoshiriki katika Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa  katika toleo lake la tatu walifahamiana na jumba hilo la makumbusho, linalosimulia kupitia yaliyomo  matukio ya kipindi kigumu katika historia ya Misri na taifa la Kiarabu, ambapo makumbusho hayo yalikuwa makazi ya kiongozi Gamal Abdel Nasser Kisha, baada ya kifo cha Rais Gamal Abdel Nasser, nyumba hiyo ilitengwa kwa ajili ya makazi ya familia yake. kwa amri ya serikali, na kisha baada ya kifo cha mkewe, umiliki wake kuhamishiwa Misri tena , hadi uamuzi wa Rais ulipotolewa wa kuigeuza kuwa jumba la makumbusho, kisha ikawa Sekta ya Sanaa, kisha ikiboresha tena hadi Mheshimiwa Rais Abd El Fatah El-Sisi mnamo Septemba 28, 2016 wakati wa kumbukumbu ya miaka 46 ya kifo cha Kiongozi Marehemu Gamal Abdel Nasser, ambapo ilikuwa mnamo Septemba 28, 1970.
Washiriki wa kundi la tatu la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa, wakati wa ziara yao kwenye jumba la makumbusho la Kiongozi Marehemu Gamal Abdel Nasser, walikagua sehemu zote na yaliyomo ndani ya jumba hilo la makumbusho, ambayo ni pamoja na mlango, mapokezi na ukumbi wa makumbusho. Chumba cha ofisi, chumba cha kulala, saluni ya Rais, kona ya Manshiyat al-Bakri, na kona ya mali za kiongozi huyo na Nishani zake,  inayojumuisha nyaraka nyingi na mali za kibinafsi za Rais Gamal Abdel Nasser, zikiwemo nguo zake, barua, binafsi. na picha za familia, na kamera zake za picha, kalamu, mapambo, beji na zawadi alizozipata.


 Mwishoni mwa ziara yao huko, washiriki wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa walipiga seti ya picha za ukumbusho, wakionyesha heshima na Shukrani ya Misri na Wamisri kwa historia yao na jukumu la viongozi wao waaminifu, akiwemo Kiongozi Marehemu Gamal Abdel Nasser, ambaye hakuwa tu  kiongozi wa Misri na Waarabu, lakini pia mmoja wa Viongozi bora zaidi katika historia ya wanadamu wote mnamo  karne ya ishirini.


 Bw.Hassan Ghazali, Mratibu Mkuu wa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa,katika toleo lake la tatu, alieleza kuwa Udhamini huo unatoa fursa sawa kwa jinsia zote mbili, kama inavyoonyeshwa na lengo la tano la Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030, pamoja na kuwawezesha vijana na kutoa fursa kwa waigizaji kutoka nchi mbalimbali Duniani kusaidiana pamoja na kuunda ushirikiano katika Nyanja mbalimbali, si tu katika ngazi ya bara, bali hata katika ngazi ya kimataifa, kama inavyoonyeshwa na lengo la kumi na saba la malengo ya maendeleo endelevu. .

Bw. Ghazali aliongeza kuwa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa , katika toleo lake la tatu, unakuja na ushiriki wa viongozi vijana wanaowakilisha takriban nchi 73 Duniani kote, pamoja na ujumbe wa Misri, wote wanawakilisha makundi mengi ya kijamii yaliyolengwa na Udhamini mwaka huu, ikiwa ni pamoja  matawi ya kitaifa kwa Vijana wasiofungamana kwa upande wowote, na wakuu wa mabaraza ya kitaifa kwa vijana,wanachama wa mabaraza ya mitaa watafiti katika vituo vya tafiti wa kimkakati na mawazo, pamoja na wanachama wa mashirika ya kitaaluma, pamoja na wataalamu wa vyombo vya habari, waandishi wa habari na wajasiriamali wa kijamii.