Kumbukumbu la Kuanzishwa kwa UNICEF

Kumbukumbu la Kuanzishwa kwa UNICEF

Imetafsiriwa na/ Meret Magdy
Imehaririwa na/ Fatma El-Sayed

UNICEF daima imekuwa nguvu isiyowezekani kuikomesha .Tangu kuanzishwa kwake, imekuwa ikipigania mabadiliko katika maisha ya watoto ulimwenguni kote, bila kujali utambulisho wao na mahali popote wanapoishi.Wakati huu, shirika hilo limesalia kwenye mstari wa kwanza wa ulinzi mstari wa mbele wa migogoro ya kibinadamu, migogoro ya silaha na majanga ya asili.Kujibu mamilioni ya watoto na kutetea haki yao ya kuishi, kwa msaada wa wafanyakazi wake wa kujitolea, washirika, na ujuzi wa nyanja, ilifikia zaidi ya nchi na mikoa 191.
Mnamo Septemba 11, 1946, UNICEF ilianzishwa kwa Azimio 57 (1) la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ili kutoa vifaa na msaada kwa watoto baada ya Vita Kuu ya II. Jina lake la awali lilikuwa Mfuko wa Dharura wa Kimataifa wa Watoto wa Umoja wa Mataifa, Hazina ya muda ya misaada ya Umoja wa Mataifa.Kisha shirika likaanzisha na kuanza kuunda dhamana ya mshikamano kati ya nchi tajiri na maskini na kuwapa vijana katika nchi zote njia mbadala ya kuishi na kufanya kazi kwa ulimwengu wenye: uhuru kwa wote, usawa kati ya jamii zote. 

Mnamo 1956, shirika lilishinda Tuzo ya Amani ya Nobel
Kamati ya tuzo hiyo ilitangaza kwamba shirika hilo lilitimiza masharti ya wosia wa Nobel na liliweza kuimarisha udugu kati ya mataifa, na kuongeza kwamba UNICEF ilitambua kwamba watoto ndio ufunguo wa maisha ya baadaye. UNICEF si vigumu kwa mtu yeyote, na hata watu wenye mamlaka zaidi hawawezi kuielewa.” Tuna haki ya kukiri kwamba kazi inayofanywa na UNICEF imethibitisha kwamba rehema haiwezi kuzuiwa na mipaka yoyote ya kitaifa.”

Kuhusu kauli mbiu ya UNICEF, ya kwanza mnamo 1953 ilikuwa na "Mtoto akinywa kikombe cha maziwa," ambayo ilionyesha shughuli kuu ya shirika wakati huo: kupeleka maziwa kwa watoto. Huku ikihifadhi vipengee vya nembo ya Umoja wa Mataifa ambayo iliegemezwa, kama vile matawi mawili ya mizeituni na umbo la dunia nyuma, nembo hiyo ilibadilika na kuwa umbo la "Mama akiwa amemshika mtoto wake" UNICEF ilipopanua kuzingatia zaidi mahitaji ya watoto, na hii pia ilihusishwa na kupitishwa kwa Umoja wa Mataifa kwa Mkataba wa Haki za Mtoto wa Mwaka 1959, ambao ulifafanua haki za mtoto kama ulinzi, elimu, huduma ya afya na makazi. , pamoja na lishe bora.Ishara ya ulimwengu wote inayomwakilisha mama anayemlea mtoto wake inaashiria matumaini, usalama na furaha, jambo ambalo UNICEF inataka kuwapa wazazi na watoto wao; ili kuamsha nguvu na shauku yao, ambayo inaonyesha matumaini ya UNICEF na matokeo ambayo inatafuta kufikia kwa kila mtoto.

Kwa hivyo, lengo la UNICEF katika miaka iliyopita limekuwa kueneza meza, iliyopambwa kwa vitu vyote vyema ambavyo asili hutoa, kwa watoto wote wa ulimwengu, na kwa sababu hii shirika hilo linachukuliwa kuwa wakala wa amani wa umuhimu mkubwa, na mwaka 2016, Umoja wa Mataifa ulipitisha msemo “kwa kila mtoto” kama kielelezo cha mkakati wake wa UNICEF, kwani maneno hayo yanarejelea jukumu la kimataifa la UNICEF la kulinda haki za watoto kila mahali, ambalo linajumuisha dhamira ya shirika hilo kutoa umuhimu mkubwa kwa watoto walio katika mazingira magumu zaidi.


Mratibu wa lugha ya kiswahili/ Tasneem Hamdy