Siku ya kimataifa ya Kupambana na majaribio ya Nyuklia "

Siku ya kimataifa ya Kupambana na majaribio ya Nyuklia "

Hapo mwanzo , wazo la kumiliki silaha za nyuklia lilikuwa mojawapo ya vigezo muhimu zaidi vya maendeleo ya kisayansi na nguvu ya kijeshi ulimwenguni, bila ya kuzingatia athari  hasi za majaribio  zinazoharibu maisha ya binadamu, pamoja na hatari na a matokeo ya nyuklia  na majanga ya kibinadamu na ya mazingira yanayotokana na majaribio ya angahewa, kwa hivyo umuhimu wa kuadhimisha siku  ya kimataifa hiyo unakuja  ili  Kupambana na majaribio ya Nyuklia, ambapo mnamo kipindi kilichopita , mwakani  1996, Umoja wa Kimataifa ulizindua mkataba wa kimataifa unaokiri kwa  kupiga marufuku kwa  majaribio ya nyuklia, na kusisitiza kuweka mipaka na  kukomesha  aina zote za majaribio ya nyuklia japo  nchi 185 zilitia saini mkataba huo na nchi zingine 170 ziliidhinisha ila  hazijaanza bado kuutekelezwa hadi sasa.

Na mnamo 2009, Umoja wa Mataifa ulitangaza  tarehe Agosti 29 kuwa Siku ya Kimataifa ya Kupambana na Majaribio ya Nyuklia, kwa  mujibu wa  azimio la  64/35  linalokiri kuwa "inapaswa kufanya juu chini ili  kukomesha majaribio ya nyuklia ili kuepusha athari hasi na zinazoharibu maisha na afya ya watu.vilvile ,  Azimio hilo linaomba Kuzinduliwa kwa shughuli na matukio ya kuelimisha ili kuongeza ufahamu wa athari za majaribio ya milipuko ya silaha za nyuklia au milipuko  ya nyuklia yoyote mingine, na kusisitiza dharura ya  kuyakomeshwa kama ni njia mojawapo ya mbinu na mifumo inayolenga kufikia lengo la kuunda ulimwengu usio na silaha za nyuklia.

Mnamo Agosti 29, 2012, Kazakhstan ilizindua mpango wa kimataifa wa "ATOM" katika uwanja wa ukomeshaji wa silaha za nyuklia na diplomasia ya umma. Hayo yalitajwa katika Kongamano la kimataifa "Kutoka  kupiga marufuku kwa  majaribio ya nyuklia Kuelekea ulimwengu usio na silaha za nyuklia" katika Siku ya Kimataifa  ya kupambana na Majaribio ya Nyuklia, na zaidi ya watu 316000  ulimwenguni kote walitia saini mkataba wa mtandao unaohusisha mradi wa " ATOM" ambao unaiomba serikali kuthibitisha mwanzo wa   kutumika kwa Mkataba wa Marufuku ya Majaribio ya Nyuklia kwa ajili ya  kukiri jukumu na umuhimu wa viongozi na mashirika ya kisiasa na ya umma na kuwahimiza,  kisha  mnamo 2016, ilizindua tuzo  " kwa ajili ya ulimwengu usio  na  Silaha za Nyuklia na Usalama wa Dunia", lengo lake kuu lilikuwa kufahamisha ulimwengu kwa viongozi, mashirika, wasimamizi na watu wasio wa serikali, ambao walitoa juhudi na michango mikubwa katika uwanja wa kutekeleza utulivu wa kikanda,  kuimarisha usalama wa kimataifa na kusimama kwa nguvu dhidi ya vita, ugaidi na upanuzi wa silaha za maangamizi makubwa.