Jukwaa la Nasser la Kimataifa latangaza Ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa nchini Misri katika utekelezaji wa Kundi la Tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa

Jukwaa la Nasser la Kimataifa latangaza Ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa nchini Misri katika utekelezaji wa Kundi la Tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa

Jukwaa la Nasser la Kimataifa limetangaza rasmi kupokea ufadhili kwa Umoja wa Mataifa kwa kundi lake la tano la Udhamini wa Hayati Gamal Abdel Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa, ambalo litafanyika mwezi Mei ujao chini ya kauli mbiu "Misri na Umoja wa Mataifa: Miaka 80 ya Uwakilishi wa Masuala ya Ulimwenguni Kusini", chini ya ufadhili wa Mheshimiwa Rais Abdel Fattah El-Sisi, Rais wa Jamhuri, na kwa ushiriki wa vijana 150 kutoka kwa viongozi wa vijana wenye utaalamu mbalimbali wa utendaji, pamoja na vijana wenye ushawishi na wanaofanya kazi kwa bidii kutoka kote ulimwenguni.

Kwa upande wake, Mtafiti wa Anthropolojia Hassan Ghazaly, Mwanzilishi wa Jukwaa la Nasser la Kimataifa, alieleza kuwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa unatokana na imani ya serikali ya Misri kuhusu umuhimu wa kuimarisha nafasi ya Umoja wa Mataifa katika kukabiliana na changamoto hizi kupitia mageuzi ya muundo wa kimataifa ili kuhakikisha uwakilishi wa haki zaidi kwa nchi za Kusini katika kufanya maamuzi ya kimataifa.

Aliongeza kuwa ushirikiano huo unalenga pia kuimarisha mifumo endelevu ya ufadhili kwa ajili ya kusaidia miradi ya maendeleo katika nchi zinazoendelea, na kuwawezesha vijana kama viongozi wa baadaye wenye maono endelevu ya ukuaji na maendeleo, Akielezea kuwa kauli mbiu ya kundi la tano la Udhamini wa Nasser kwa Uongozi wa Kimataifa imekuja kwa jina "Misri na Umoja wa Mataifa: Miaka 80 ya Uwakilishi wa Masuala ya Ulimwenguni Kusini" ambapo Misri ilishiriki katika kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa mnamo mwaka 1945.

Vile vile, Misri imeendelea kuwa na jukumu muhimu sana katika kuunga mkono masuala ya Ulimwenguni Kusini, ikiwa na mtazamo unaojumuisha kujitolea kwake kwa misingi ya haki ya kimataifa na juhudi za kufikia maendeleo endelevu katika nchi zinazoendelea. Akiongeza kuwa kwa kipindi cha miaka 80, Misri imekuwa mfano wa nchi inayounganisha kujitolea kwa maslahi ya kitaifa na uwazi wa kimataifa, ikijitahidi kuinua sauti ya Kusini na kuimarisha ushirikiano miongoni mwa wanachama wake. Pia Misri ilishiriki kikamilifu tangu mwanzo katika kuandaa mkataba wa Umoja wa Mataifa, kwani Misri ilitambua tangu wakati huo umuhimu wa Umoja wa Mataifa kama jukwaa la kimataifa la kutetea masuala ya nchi zinazoendelea.

Mwanzilishi wa Jukwaa la Nasser la Kimataifa aliongeza kuwa Misri ilikuwa na jukumu muhimu sana katika uhuru wa nchi nyingi za Ulimwenguni Kusini katika miaka ya hamsini na sitini ya karne ya ishirini hata Misri iliongoza juhudi kubwa za kusaidia nchi hizi ndani ya Umoja wa Mataifa hata kabla ya kupata uhuru wao, kwa kuwasafirisha viongozi wa kitaifa kutoka Kairo hadi New York kuwasilisha masuala yao ya haki kwa Umoja wa Mataifa wakati wa Mkutano Mkuu. Misri iliamini katika misingi ya mshikamano miongoni mwa nchi za Ulimwenguni Kusini. 

Akieleza kuwa kadri nafasi ya Umoja wa Mataifa ilivyoendelea katika kusaidia maendeleo endelevu, Misri ilibaki mstari wa mbele katika nchi zinazojitahidi kuimarisha mkondo huu katika Ulimwenguni Kusini, na kwa kulingana na Ajenda ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu ya 2030. Aidha, Misri ilianzisha mipango mingi na katika miaka ya hivi karibuni imejikita katika kuimarisha misingi ya ushirikiano wa Kusini-Kusini.

Mtafiti wa Anthropolojia Hassan Ghazaly alieleza kina cha maana ya ishara iliyobebwa na kauli mbiu rasmi iliyotolewa na Umoja wa Mataifa katika kuadhimisha kumbukumbu ya miaka themanini tangu kuanzishwa kwake. Alisema kauli mbiu hiyo, "Pamoja kwa Mustakabali Bora," inabeba maana muhimu sana, ikiwakilisha wito wenye nguvu na wa dharura kwa nchi zote duniani, mashirika yake, na watu wake kufanya kazi kwa pamoja na kuunganisha juhudi ili kujenga mustakabali ulio bora zaidi, wenye ustawi, haki, na endelevu kwa vizazi vya sasa na vijavyo sawa.

Alisisitiza kuwa kauli mbiu hii si maadhimisho tu ya miongo minane tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa, bali inakwenda zaidi ya hilo ili kuendana kwa karibu katika maudhui na malengo yake na "Mkataba wa Mustakabali" unaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa. Mkataba huo unawakilisha maono kabambe yanayolenga kufanya upya na kuimarisha nafasi ya taasisi za kimataifa katika ulimwengu wetu wa kisasa, pamoja na kusukuma mbele kufikia malengo makuu kadhaa ifikapo mwaka 2025.

Ghazaly pia alibainisha kuwa mchakato wa kupata msukumo wa muundo wa kauli mbiu hii kutoka kwa muundo mkuu wa nembo ya Umoja wa Mataifa haukuwa bahati mbaya, bali ulikuja kwa lengo kuu la kudumisha kiwango cha juu cha uwiano na msimamo na utambulisho thabiti wa taasisi ambao Umoja wa Mataifa unajivunia nao ulimwenguni.

Ni vyema kutajwa kuwa Udhamini wa Nasser kwa Uongozi ulianzishwa kwa mara ya kwanza mnamo mwaka 2019 kama udhamini wa kwanza wa vijana wa Kiafrika kwa Waafrika, sambamba na uenyekiti wa Misri wa Umoja wa Afrika chini ya ufadhili wa Baraza la Mawaziri ili kuhamisha uzoefu wa maendeleo wa Misri kwa vitendo, katika mfumo wa kuimarisha dhana ya ushirikiano wa Kusini-Kusini ambapo Misri ina jukumu la uongozi. Baada ya toleo lake la kwanza, Udhamini huo ulipata ufadhili wa heshima kutoka kwa Rais Mheshimiwa Abdel Fattah El-Sisi katika matoleo yake ya pili, tatu, na nne yaliyofanyika mnamo miaka ya 2021, 2022, na 2023. Udhamini huo umepanuka na kujumuisha mabara ya Asia, Australia, Amerika ya Kilatini, na Ulaya, pamoja na bara la Afrika ambalo limekuwa msingi tangu kuanzishwa kwake.