Kisa cha mpiganaji risasi  "Muhammed Mahran" mkombozi mwana wa port Said 

Kisa cha mpiganaji risasi  "Muhammed Mahran" mkombozi mwana wa port Said 

Mkombozi MwanaPort Said , Shujaa Mohamed Mahran,  alizaliwa mnamo Septemba 6,1938 katika eneo la Waarabu cha mji wa Port Said.

Wakati  wa ukoloni wa  kiingereza kwa  Misri, walinzi wa Kitaifa wameshaundwa huko Port Said ili kukabiliana na ukoloni huo wa kuchukiza na kuutetea mji wa Port Said dhidi ya Waingereza na Shujaa huyo Muhammad Mahran alikuwa miongoni mwa vijana waliojiunga katika kambi ya mafunzo na kuchukua nafasi ya uongozi  wa kundi la  pili ya kikosi cha kwanza, na alikuwa na umri wa miaka 18 wakati huo.

Mahran na wenzake walipewa jukumu la kutetea Uwanja wa Ndege wa Port Said na eneo la Gemayel magharibi mwa mkoa huo mnamo Novemba 1956, ambapo eneo hilo lilikuwa likilengwa  na askari wa Uchokozi wa Tatu  ambao walishuka  kwa  purutangi  ili  kuingia Port Said. vilevile , adui alikuwa akishmbulia kwa mabomu na nabelm " Poda  ya moto "  na kushambulia kupitia ndege   madaraja  na barabara zinazoelekea Port Said na nyinginezo .

Adui aliongeza mashambulizi yake, yaliyo  na kifuniko cha anga na mabomu, kisha helikopta ilitua,  askari (5) wa Waingereza  wenye silaha  vyombo  visivyo na waya , na hapo juu  walilindwa  kwa  ndege 3 . Kisha helikopta iliruka na aliwaacha askari  ardhini mwa  Port Said  na Wakati huo shujaa Muhammad Mahran na wenzake walikuwa wamo ndani ya shimo  ili kufuatilia hali ilivyokuwa na Baada ya muda mfupi helikopta ilirudi tena kuwachukua askari, na wakati huo  mmoja wa wenza wa Mahran alitoka  shimoni akapigana vikali hadi aliuawa shahidi kwa risasi za adui. Adui aligundua eneo la shimo la mashujaa, kwa hivyo shujaa Muhammad Mahran aliharakisha  kurusha mabomu  anayo kwa adui pamoja na kupiga risasi  zinazofuatana katika pande zote   na aliweza kuua askari  wa maadui  kadhaa na shujaa akaanza kuelekea kutoka shimo moja hadi lingine. ghafla  shujaa  Muhammed Mahran alipigwa risasi kichwani na akaanguka ardhini  akizimia kisha alitekwa nyara .

 wakati ilipotangazwa saa sita mchana Novemba 5, 1956, Shujaa Muhammad Mahran alikuwa  katika eneo la Al-Gamil, Magharibi kwa  Uwanja wa Ndege wa Port Said, akaona kundi la askari wa Uingereza wakikunywa vinywaji na kucheka kwa kejeli, kisha mmoja wao akamsogea shujaa akasema: Nataka kunywa maji 

askari akamwambia shujaa Muhammad Mahran: Abd El Nasser hakukuletea maji hapa ili unywe? .

Shujaa Muhammad Mahran alisema: Maji uliyo nayo ni maji ya Misri yaani  ni maji ya Wamisri wote.

Askari huyo alimpiga teke shujaa Muhammad Mahran kwa mguu wake, na hapa shujaa alijaribu kumpokonya bunduki kutoka askari, na kweli aliweza kufanya hivyo, isipokuwa askari   mwingereza mwengine nyuma ya shujaa huyo alirusha bomu juu ya mguu wa shujaa akakimbia kutokana na hiyo shujaa alijeruhiwa katika miguu yake.

Kesi  bandia  ilimeshafanywa  kwa  shujaa, wakamwambia: Chagua kinachokufaa,au  ujibu maswali utakayoulizwa, au kuadhibu adhabu ambayo hutadhanishwa? .

Shujaa akawauliza: maswali gani?

Wakasema: Tunataka kujua maelezo juu ya  Port Said na Misri yanayohusiana na wapiganaji wa Port Said na  wapi maeneo yao , idadi ya  vikosi na makundi , na aina gani  za silaha mlizo nazo?

Shujaa akajibu, "Sijui chochote."

wakati huo kiongozi wao alisema: Usipojibu na ukaendelea kupinga malipo utakayolipa  ni macho yako  . 

Shujaa Muhammad Mahran alisema: Sijui chochote.

Kabla hawajamng'oa macho yake , Waingereza walimhamisha hadi kwenye mojawapo ya ndege zilizokuwa juu ya jukwaa , kisha ndege ikaruka hadi Uwanja wa Larnaca huko Cyprus. Na Waingereza walimwita (mpiganaji  risasi), kwa sababu aliwapiga kwa bunduki yake makumi ya askari waingereza wa anga  kwenye pwani mwa Port Said, na alikuwa akiwalenga  kichwani na  machoni haswa, kwa hivyo walipanga kumng'oa macho yake . halafu Waingereza walisherehekea baada ya kumkamata kwani wakimzingatia, kama viongozi wao walivyosema, " pato lenye thamani."

Muhammad Mahran anasema: Tulipofika Cyprus, walinipelekea gari na kutoka hapo wakanipelekea  Hospitali ya Jeshi la Uingereza huko Cyprus, na kule nilidhani kwamba nitapata matibabu yangu kama mfungwa ila nilipofika walinitupia kwenye chumba na watu waingereza wanne walikuwa wamenisubiri  na walikuwa kama washenzi  Hawana huruma hadi daktari mwingereza alipokuja kuwaamuru wasitishe adhabu na kuniambia: Tutakung'oa macho ikiwa hutajibu maswali, na baadhi ya maswali kuhusu eneo na shughuli ya upinzani katika Port Said, na kwa sababu ya kukataa kwake kwa kujibu, macho yake yameshang'olewa .

 Na shujaa Muhammad Mahran anaelezea  kuwa Rais Gamal Abd El Nasser alimletea zaidi ya timu moja ya madaktari wahusika  kutoka nchi mbalimbali za ulimwenguni (Umoja wa Kisovyeti, Ujerumani Mashariki, Uhispania na Austria) kwa siku na miezi kadhaa  kwa ajili ya kunisaidia kupata uwezo wa kuona tena, lakini madaktari wote waliripoti kwamba Waingereza walikuwa wamemng'oa mshipa wa  macho  mpaka majaribio yoyote ya kuyatibu yalishindwa .. na sababu  ya kumkamata   bingwa huyo ni  kupambana kwa ushujaa  na kuwaua  kikosi na askari waingereza kadhaa karibuni  kwa uwanja wa ndege wa Al-gamel    na  Baada ya kujeruhiwa, alikamatwa na inatakiwa kutendwa  kama mfungwa wa vita , ila mtindo huo  wa  ukoloni mpya na ya zamani ambao  niliuzoea kutoka kwao  Wanajifanya wana   ustaarabu na ubinadamu,  na ndio wako mbali na hilo. 

Rais wa Misri Abd El Fatah El-Sisi alimzawadia kwa kumrejesha katika kazi yake katika mambo ya maadili kwenye Makumbusho ya Kijeshi kama tathmini yake baada ya kutengwa,  pamoja na kumpa Viza ya kuhiji kwa gharama ya jeshi,  kuweka mlinzi anayeandamana naye milele . kwa maisha yote, kumkabidhi zawadi na kuutaja mradi mojawapo ya  miradi  ya makazi   ya hivi karibuni kwa jina lake, kwa Shukrani na  uthamani kwa jukumu lake la Kishujaa na la kiukomboaji .

Shujaa  mpinzani wa Ukoloni kwa ajili ya Port Saidaliaga Dunia baada ya  kuandika jina lake katika historia ya kishujaa kwa  "Mji Shujaa" kwa kujitolea, mnamo Mei 10, 2021.