Abdulrazak Gurnah

Abdulrazak Gurnah

 Ni mwandishi wa riwaya Mtanzania, anayeishi nchini Uingereza. Alizaliwa Disemba 20, mwaka 1948 visiwani Zanzibar.

Alisafiri kwenda Uingereza mnamo mwaka 1968, miaka sabab baada ya nchi yake Tanzania kupata uhuru na mpaka sasa bado anaishi uingereza ambapo hivi karibuni amestaafu kama Profesa wa Fasihi katika Chuo Kikuu cha Kent. 

Mbali na kufundisha Gurnah amekuwa akifanya kazi za kuhariri nyaraka mbalimbali, vitabu na majarida na sasa ni mhariri wa jarida maarufu la ‘Wasafiri.

Apart from Nobel Prize, he has also won Booker Prize for Fiction award in 1994, Times Book Prize (Fiction), Los Angeles in 2001 and Commonwealth Writers Prize (Eurasia Region, Best Book) in 2006. 

Mbali na tuzo ya Nobel, pia amewahi kushinda tuzo ya Booker Prize for Fiction mwaka 1994, Times Book Prize (Fiction), Los Angeles mwaka 2001 na tuzo ya waandishi wa Jumuiya ya Madola (Eurasia Region, Best Book) mwaka 2006.

Abulrazak Gurnah anakuwa mmoja kati ya waafrika wachache kushinda tuzo za Nobel katika historia tangu kuanzishwa kwake mwaka 1901. 

Mpaka sasa ameshachapisha riwaya 10 ambazo ni; 

The Last Gift (2011), The Cambridge Companion to Salman Rushdie (2007), Desertion (2005), By the Sea (2001), Admiring Silence (1996), Paradise (1994), Essays in African Literature: A Re-evaluation (1993), Dottie (1990), Pilgrim’s Way (1998) na Memory of Departure (1987).

#AfricanYB #AUTalks #Africa #Tanzania  #African_Union #GlobalCitizen #GCTalk #Global_Citizen #NasserYouthMovement